Elections 2010 Londa ampigia kampeni JK msikitini

Zak Malang

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2008
Posts
5,404
Reaction score
239

* Hamad Rashid apigwa butwaa

Katika hali ya kushangaza, aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam, Salum Londa, jana aliwagawa waumini wa dini ya Kiislamu, baada ya kupiga kampeni msikitini akiwataka waumini hao wamchague mgombea urais kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete.

Londa alitoa kauli hiyo mara baada ya kukaribishwa katika ibada ya sherehe za Idd el Fitr iliyofanyika katika Msikiti wa Al farouq, Kinondoni, Dar es Salaa na kusisitiza Waisilamu kutofanya makosa kwa kupigia kura, kama walivyofanya mwaka 2005.

Londa amabaye alikuwa mgeni rasmi katika swala hiyo, alisema ipo haja ya Waisilamu kutofanya makosa na wajue umuhimu wa kuchagua viongozi kama miaka yote iliyopita.

Baada ya kutoa kauli hiyo, kundi la Waisilamu lilinyanyuka na kuondoka huku wengine wakilalamika kitendo hicho na kusema hakiendani na utamaduni wao kutumia nyumba za ibada kufanya kampeni za uychaguzi kwa viongozi wa siasa………...


……….Akizungumza na Tanzania Daima mara baada ya kumalizika hotuba hiyo, Mbunge wa Wawi (CUF) amabaye pia ni kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni anayemaliza muda wake, hamad Rashid alisema hakupendezwa na kitendo cha kiongozi wa siasa kupiga kampeni msikitini, kwani kufanya hivyo ni kuharibu utaratibi katika nyumba za ibada.

“Mimi nilipigwa na butwaa kwa kitendo hiki, kitendo cha mwanasiasa kusimama kwenye nyumba za ibada kumpigia kampeni mgombea fulani, kamwe hakikubaliki,” alisema Hamad.


Wana JF: Hiyo ni sehemu tu ya stori ukurasa wa mbele katika Tanzania Daima ya leo.
 
Londa ana ma'frustrations ya ufisadi wa ardhi Kinondoni, sasa anajaribu kwa kila njia kuosha uso wake mbele ya JK na wanaccm, akitegemea KUKUMBUKWA mbele ya safari!
Sasa hivi ukimpa mtu jukwaa dogo tu utashangaa jinsi atakavyolitumia kujifaidisha!

All in all, amefulia huyu, hana jinsi ya kuondoa kashafa!
 


Wanaohubiri wananchi wasiwe na udini ndo haohao wanaohubiri udini.
 
Huyu Bwana kafanya hujuma na wizi mkubwa sana Manispaa ya Kinondoni kiasi kwamba ingekuwa kuna utawala bora na kuwajibika, wakati huu asingekuwa msikitini anafanya kampeni, bali lupango akila dona. Anamfanyia kampeni JK kwa sababu anajua fika kwamba ni yeye tu ndiye atakayemlinda kutokwenda jela, kama vile JK anavyowalinda wezi wengine wengi ndani ya CCM!

Nani katika mafisadi wakuu -- hasa wale papa -- wanaweza kuthubutu kumkampenia Dr Slaa? Hawawezi, kwani kufanya hivyo ni kujipalia makaa.
Lakini cha kushangaza zaidi ni jinsi tutakavyoona taasisi kuu ya kusimamia uchaguzi -- NEC -- itakavyokaa kimya kuhusu hili!
 
Baada ya kutoa kauli hiyo, kundi la Waisilamu lilinyanyuka na kuondoka huku wengine wakilalamika kitendo hicho na kusema hakiendani na utamaduni wao kutumia nyumba za ibada kufanya kampeni za uychaguzi kwa viongozi wa siasa………...
Safi sana ndugu zangu waislamu, mngempiga makofi kabisa ili iwe fundisho kwa wengine wanaongeuza Misikiti/makanisa sehemu ya kampeni hasa Lowasa,Rostam....
 
Safi sana ndugu zangu waislamu, mngempiga makofi kabisa ili iwe fundisho kwa wengine wanaongeuza Misikiti/makanisa sehemu ya kampeni hasa Lowasa,Rostam....

Nadhani haukuwa msikiti wa ndugu zangu answari sun, Laiti ingekuwa huko angetoka na manundu, lazima angechezea bakora!
 
Hivi ingekuwa ndo mchungaji mmoja kafanya hivyo kanisani, kina Malaria Sugu na aliases zake zote wangeibuka humu na ku-fire through all cylinders!!!
 
..Londa amefanya hivyo na inaonekana ni KOSA, je kitafuata nini kutoka kwa vyombo vinavyosimamia kanuni na sheria za uchaguzi? Au hadi mtu ajitokeze kutoa malalamiko?
 
Hongera Waislam

Mtume wetu alifanya msikiti nyumba ya ibada na pia kuendesha vikao!... SIASA MSIKITINI Ndio mahala pake waislamu wanajidili nani tuumchaguwe!! CUF ndio wanatupotezea! ..:mad2:
 
Kwani ndio wameanza au wameamua sasa kufanya live? na hutasikia mtu akikemea. Lakini thubutu lifanyike kanisani......zitaimbwa hadithi za amani na utulivu hizo? Haya bana ngoja na sisi twende kesho kanisani tukamwage ugali maana wamemwaga mboga
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…