Look alike. . .

Dr Lizzy

Platinum Member
Joined
May 25, 2009
Posts
31,009
Reaction score
60,629
Wapo watu ambao hua tunawafananisha kwa muonekano, namna ya kuongea, kifikra au walivyo tu kiujumla na watu wetu wa karibu au tunaowafahamu tu.

Hii inaweza ikasababisha mtu akawa na hisia mbaya au nzuri sana na mtu asiemfahamu kwasababu tu anamkumbusha mtu ambae hayuko nae vizuri/yuko/alikua nae vizuri sana kimahusiano, awe rafiki, ndugu au hata mpenzi.

Swali langu ni je, umewahi kujikuta unampenda mtu kwakua anakukumbusha mtu fulani ambae inawezekana yuko mbali sana na ulipo wewe au hata alishaaga dunia hii?
 
Navutiwaga sana na vituko na shepu ya Anti Ezekieli (muigizaji). Mtaani kuna baa medi kafanana nae almost 95%, nimejikuta siichoki hiyo baa, na nikienda lazima nihudumiwe na yeye. Kama hayupo job namfatuta...
 
Ndio Lizzy, kuna wakati mtu anakukumbusha mtu fulani, hata kama ulikuwa hujamzoea, unaanza kum-accept kidogo kidogo.

Ila kufanananishwa napo kuna taabu yake, nilishajikuta nataka kuingia matatani.
 
Ndio Lizzy, kuna wakati mtu anakukumbusha mtu fulani, hata kama ulikuwa hujamzoea, unaanza kum-accept kidogo kidogo.

Ila kufanananishwa napo kuna taabu yake, nilishajikuta nataka kuingia matatani.
Hahahahha. . . Konnie ukute umefananishwa na mdeni wa mtu au jambazi mbona utakoma. We ilikuaje. . . ?
 
Kwahiyo wewe unavyompenda mama,dada na kaka zako kunakufanya kicheche? Maana kupenda sio lazima ngono ihusike.

Upendo wa kwa mama ako na upendo wa kwa mpenzi wako unafanana?
 
hapana, nimewahi kukutana na mtu ambaye automatik nafsi yangu imemchukia, sikuwa na sababu ya kumchukia........mbaya zaidi kuna siku aliniambie ujinga fulani nikazidi kumchukia......

Siku hizi najitahidi nikimuona nimsalimie, nimpungi, nimchekee ili chuki ipungue.....
 
Ni ukweli kabisa

Huwa kuna watu wanafanana vitu fulani, kisha une vijua ukamkumbuka mtu mwenye kufanana nae

Kuna mtu nilimuona nafanana na mwalimu wangu wa Primary, nilimkumbuka sana mwalimu
 
Umewahi mwona mtu kafanana na mzazi wako?
 
BT inawezekana kuna kitu anakukumbusha kama yeye binafsi hamna baya alilokutendea.
 
Kuna dada hadi leo nampenda... anafanana mno na marehemu mamangu mdogo alikufa really young. Hata hatujazoeana nae na wala siwezi thubutu kumwambia afanana na marehem, but I like her.
 
BT inawezekana kuna kitu anakukumbusha kama yeye binafsi hamna baya alilokutendea.

inawezekana Lizzy, na kama kipo hicho kitu sijakijua bado, ila namchukia huyo mtu jamani hadi najishangaa.... Na sina mazoea nae, wala hatupo karibu kihivyo.....mbaya zaidi kila siku asubuhi nitakutana nae kama sio parking basi koridoni......

Ni mbaya sana kwa kweli, mpaka najisikia vibaya kumchukia mtu bila sababu.....

Sijui kama amenotice au vipi..........
 
Yeap!!
Even humu jamvini kuna mtu nampenda, tokana na kwamba ananikumbusha mtu flani ambae nahisi kumfananisha nae!!
 

mabwaku kumbe ndio wewe nshakujua poa bwana one day yes BT..
 
BT inawezekana kuna kitu anakukumbusha kama yeye binafsi hamna baya alilokutendea.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…