Lori lililoibwa Ruvuma lapatikana Njombe

Pantomath

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2019
Posts
842
Reaction score
3,449
Lori aina ya Howo, Tiper lenye namba za usajili T 459 EBX, mali ya kampuni ya CRCG inayojishughulisha na uchimbaji wa makaa ya mawe, lenye thamani ya Tsh. Mil. 150/=, lililoibiwa mkoani Ruvuma, limepatikana katika Kata ya Ramadhan iliyopo mkoani Njombe.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Mkoa wa Ruvuma ACP Marco Chilya, amesema tayari wamemkamata Dereva wa lori hilo, ambaye pia alihusika na wizi huo, na kwamba upelelezi umekamilika na atafikishwa mahakamani kesho Juni 16, 2023.



Huyu kazidi, sasa dubwasha kubwa hivyo alitaka akalifiche wapi?
 
Wakinga banaa, Au kaiba kabla ya kuandaa location au kulengesha mteja?

Halafu unaiba njombe unaenda ruvuma?

Ukute pengine alikua anavusha mzigo wa magendo, jumba zima likamuangukia.

Nakumbuka kuna jamaa aliiba Semi, kufika njiani Mteja hafiki bei akalikimbia.
 
Mtu unaiba tipa lote hilo, likipata hata pancha unalikimbia.
 
Watu wabaya sana. Utakuta aliahidiwa akilifikisha sehemu anapewa chake na kupotea, bahati mbaya ndio hivyo tena🤣🤣
Watu wabaya sana
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]wanabadilisha Nini Sasa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…