Ncha Kali
JF-Expert Member
- Sep 19, 2019
- 15,335
- 29,114
Je, wajua ni ipi lugha yako ya kimahaba?
Japo tunaweza kusema kuwa haya ni mambo ya wazungu. Lakini kihisia binadamu wote tupo sawa huku tukiwa na tofauti ndogo ndogo zinazotutofautisha na wengine.
Zipo lugha kadhaa zilizothibitishwa kutumika kati ya mtu mmoja na mwingine linapokuja suala la mahaba. Nazo ni kama ifuatavyo:
1. Maneno ya pongezi au sifa (Words of affirmation).
Wapo watu wanaopenda kusikia maneno mazuri mazuri muda wote ili wajisikie kupendwa, we wasifie tu utaona matokeo.
2. Muda mzuri kukaa pamoja (Quality Time).
Ukisikia kuna watu wanafungiwa ndani wasiende kazini ilimradi tu washinde pamoja ujue ndo hawa. Na zile za kupenda mitoko (outings)ili kufurahia muda mzuri wakiwa pekee yao bila bughudha.
3. Kukumbatiana (Physical Touch).
Hawa ni wale wanaosisimuliwa na miguso kutoka kwa wenza wao. Maneno buku bila kumgusa mwenzio ni kazi bure, hata wakiwa barabarani utaona wameshikana mikono huku wakitembea kwa raha zao.
4. Kusaidiana Kazi (Acts of service).
Hapa ni wale wa kupenda kusaidiwa kazi. Msaidie kubeba hata mkoba tu uone anavyofurahi, ukimsaidia kupika ama usafi wa nyumba utapewa hata vile hujawahi kupewa.
5. Kupokea Zawadi (Receiving Gifts).
Hili kundi limekuwa la mkumbo, wengi hata wale wasiojua wanahitaji nini wamekuwa wakijiunganisha na kundi hili kwa kuonesha wanapenda kupokea zawadi. Jukumu la kutoa hizo zawadi sijui wanamwachia nani.
Ni mara chache sana mtu mmoja kuwa kwenye makundi zaidi ya moja. Ila wengi wetu kwa kutokujua au kwa kujiongopea tunatamani kundi lisilo letu, ndiyo sababu hata hatujisikii kupendwa na wenza wetu kwa sababu hatujui ni kwa namna gani tunapaswa kuoneshwa upendo huo.
Hebu basi karibuni tutiririke lugha ya kila mmoja wetu hapa.
Karibuni.
Japo tunaweza kusema kuwa haya ni mambo ya wazungu. Lakini kihisia binadamu wote tupo sawa huku tukiwa na tofauti ndogo ndogo zinazotutofautisha na wengine.
Zipo lugha kadhaa zilizothibitishwa kutumika kati ya mtu mmoja na mwingine linapokuja suala la mahaba. Nazo ni kama ifuatavyo:
1. Maneno ya pongezi au sifa (Words of affirmation).
Wapo watu wanaopenda kusikia maneno mazuri mazuri muda wote ili wajisikie kupendwa, we wasifie tu utaona matokeo.
2. Muda mzuri kukaa pamoja (Quality Time).
Ukisikia kuna watu wanafungiwa ndani wasiende kazini ilimradi tu washinde pamoja ujue ndo hawa. Na zile za kupenda mitoko (outings)ili kufurahia muda mzuri wakiwa pekee yao bila bughudha.
3. Kukumbatiana (Physical Touch).
Hawa ni wale wanaosisimuliwa na miguso kutoka kwa wenza wao. Maneno buku bila kumgusa mwenzio ni kazi bure, hata wakiwa barabarani utaona wameshikana mikono huku wakitembea kwa raha zao.
4. Kusaidiana Kazi (Acts of service).
Hapa ni wale wa kupenda kusaidiwa kazi. Msaidie kubeba hata mkoba tu uone anavyofurahi, ukimsaidia kupika ama usafi wa nyumba utapewa hata vile hujawahi kupewa.
5. Kupokea Zawadi (Receiving Gifts).
Hili kundi limekuwa la mkumbo, wengi hata wale wasiojua wanahitaji nini wamekuwa wakijiunganisha na kundi hili kwa kuonesha wanapenda kupokea zawadi. Jukumu la kutoa hizo zawadi sijui wanamwachia nani.
Ni mara chache sana mtu mmoja kuwa kwenye makundi zaidi ya moja. Ila wengi wetu kwa kutokujua au kwa kujiongopea tunatamani kundi lisilo letu, ndiyo sababu hata hatujisikii kupendwa na wenza wetu kwa sababu hatujui ni kwa namna gani tunapaswa kuoneshwa upendo huo.
Hebu basi karibuni tutiririke lugha ya kila mmoja wetu hapa.
Karibuni.