Lowassa amtunishia misuri Kikwete?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513

Hii Inaonesha ni jinsi gani UROHO wa madaraka unaweza kumtia mtu upofu mpaka akawa haoni hata zile rangi za msingi.
Ifuatilieni hii news kama source inavyoonesha.

Ila kwa taarifa tu, ni kuwa shughuli imeanza na hakuna kulala mpaka wapate wanachokitaka...
 

Huyu Lowasa hajui kuwa anapambana nguvu anayopambana nayo. Naona nifuate alichosema Mkulu FMES, ngoja angalau atumie mapesa yake ambayo ameyakusanya kwa wizi miaka yote hii.
 
Na ole wao Waandishi waliopowa hongo kumsafisha. Ina maana ile sheri ya MoneLoundry inakuwa active kwa wauza unga tu?? nadhani hapa ndio wangechangamkia kuchunguza akaunts za hawa watuhumiwa wa ufisadi kisha na wao tungewapa credit kama PRA.

Ah maskini mmasai wa watu, anakuja na mkuki huku tumejiandaa na AK47 kalashikov
 
Kazi ipo!

Nadhani hii ni ile biashara ya Mbwa kala Mbwa!!!!
 
Hivi umekosa kichwa kingine cha mada yako? au umeshaathirika na kukopi nakuapaste ....!
 
Niajiuliza kuwa hivi kweli nchi hii ina wenye nchi au wananchi?
Kama huyu white head ataachwa kuendelea kulikashifu Bunge kwa kuikosoa Kamati Teule iliyoteuliwa na kutumwa na Bunge, na kama anaachiwa kutumia vyombo vya serikali kukanusha kuwa kahusiki na Richmond hii inaonesha kuwa kuna mkakati nyuma ya pazia kurudisha darajani.

Nina maswali mengi bila majibu
 
Kwanza huyu Lowassa ana kesi ya kujibu mahakamani, na akipandishwa kizimbani amekwisha halafu analeta jeuri. The fool is fighting a losing battle.
 
Huyu mamvi anafikiri kuwa tupo kwenye the old stone age hivi sasa tupo kwenye kizazi kingine cha dotcom where we dare to talk openly kwanini anafikiri kuwa he is only man deserved to led Tanzanians?Ushauri wa bure kwani asikubali yaishe tu kwa kukaa kimya na kuendelea na maisha ya yake ya kila siku.Another thing ni kwamba what is so special hadi anata kuwa kuwa Rais ikiwa Uwaziri mkuu umemshinda?Akiwa rais si ndio atatupiga mnada?
 
Msamee Lowasa naona hajui kama ameisha toka katika kiti cha uwaziri mkuu.

Asipo angalia atapagawa tu. Tumuombee anaweza kutembea........
 
Kama ni kweli wanajiandaa basi wote inafaa wakanyie debe ,na tatizo hapa ni kwa Muungwana kutaka wawepo karibu na ile kucheka cheka nao ndio itakayomliza asipoangalia na akitahamaki atakuwa amechelewa Waswahili wana msemo unasema udongo upate ungali mbichi na kwa msemo huo hawa baadhi ya mafisadi inafaa wafikishwe mahakamani bila ya kuoneana haya wala yale na wakitahamaki kila mmoja anachezea kifungo cha miaka hamsini kwa kusababisha maafa na shida mbali mbali kwa waTanzania hapo Muungwana na watu wake ndio watakuwa salama lakini kuwaachia wakipeta kwenye mitaa wanaweza kabisa kufanya mambo yenye uamuzi mchafu kama ilivyosenwa katika hiyo dili.
Kwa ushauri wa bure inapotokea kukamatwa au kujulikana kuwa wakuu fulani wamehusika katika ufisadi basi haifai kabisa watu hao kupewa mida ya kujipanga kwani inakuwa ni kama wanapanda mbegu ambayo itatoa mizizi na kukuwa kwa haraka.
Sioni sababu kwa nini serikali haijawapandisha mahakamani hadi leo ,hivi kuna wanalolingojea ,yaani unawapandisha mahakamani halafu unawaweka mahakimu wenye uchungu na nchi yao nisikilizie hakuna tufani wala zamana ,utasikia kesi imekwisha wamehukumiwa kunyongwa kwa kuhujumu uchumi wa Inchi na rufani inatupiliwa mbali ,maana ushahidi kwamba walikwiba ni wa wazi .si tunasikia feza wanailudisha ,hivi mlala hoi angeruhusiwa kurudisha feza ,mambo gani haya wanayafanya serikali hii kwa kweli hayajulikani na ndio kuchezea shilingi chooni ,yaani Muungwana alikuwa afunge kazi nao watu hawa tena kijeuri ukishawasweka jela ,itakuwa wamekwisha na hizo hujuma zao itabidi wapange na maafande wa magereza maana anakwambia katika jiwe hili kuna zahabu chukua nyundo na tindo uitafute ,kinachotakiwa kufanywa ni watu hawa wasikae uraiani zaidi ya miezi sita na huku wanakoanza kufanya ni kujijenga kwa haraka ili kuirudisha imani.Take care !!!
 
..taratibu. una uhakika na hili?

It is so ironic that, something so obvious to everyone in this world it is so oblivious to you. Guess what? Your guy has a case to answer sooner rather than later; in that case, don't set yourself up for surprises.
 
let me ask--how come ur 100% sure that 'ikulu' is free of richmond saga??
But if u know what i mean!!
 
Mimi nabashiri kuwa siku ya Lowassa kupandishwa kizimbani itajulikana atakapoanzisha chama cha siasa au kujiunga na chama kingine kwa lengo la kupambana na JK katika urais wa 2010. Hapo yale yanayofichwa yote yataibuka, na uchaguzi ukishaisha yanarudishwa yalikokuwa!

Yametokea kwa kina Atiku Abubakar (alikuwa mshkaji tena makamu wa Obasanjo, lakini ona alivyomgeuka!), Nawaz Sharif (Pakistan), hata Benazir Bhutto (Mungu apishe mbali lakini janga kama lile) alijulikana kwa ufisadi katika awamu zote mbili alizokaa madarakani lakini bado alikuwa "tishio" katika siasa za upinzani!

Col. Dr Kiiza Besigye (actually ni medical Lab technician) alikuwa rafiki mkubwa wa Museveni wakati wakiwa msituni wakipambana na Obote, na ndiye aliyekuwa daktari wake huko. Lakini alipotaka kupingana nae kwenye urais ziliibuka tuhuma kibao na kesi mahakamani akafunguliwa, mojawapo ikiwa ya ubakaji, kwamba ati walipokuwa msituni Besigye alibaka wapiganaji wa kike na wanawake wengine raia waliokuwa wanawakamata wanapoteka eneo! Lakini makosa hayahaya waliyafanya pamoja na Museveni, ndio iliyokuwa tabia yao porini! Tofauti ni kuwa wakati wa mashtaka mmoja ni rais na mwenzie ni mpinzani, kwa hiyo hakuna aliyeko tayari kuja kutoa ushahidi dhidi ya rais hata kama Besigye angeyasema, na zaidi kikatiba rais ana immunity!

Sasa hivi ingawa yapo mengi anayotuhumiwa Lowasa mintarafu ufisadi, na mengi ukweli wake umeonekana katika matukio ya hivi karibuni yaliyomfanya ajiuzulu, bado dalili zinaonesha hakuna atakayemshitaki bila JK kuridhia. Na akitamani sana kushitakiwa, basi amchokonoe JK kiasi cha kutosha, wakichokana tutayaona tu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…