Lowassa asimikwa kiongozi wa kimila wa wamasai

Lowassa asimikwa kiongozi wa kimila wa wamasai

Huduma

Member
Joined
Jan 26, 2008
Posts
68
Reaction score
2
Ndugu yetu, mwenzetu Bwana Lowassa ametawazwa rami kuwa kiongozi wa kimila wa jamaa zetu Wamasai.

Kusimikwa huko kutampa nafasi ya kufanya ziara Arusha, Arumeru, Monduli, Morogoro, Usangu na kadhalika ili kujitambulisha rasmi.

Shirika la Taifa la Habari Tanzania [TBC] lilitumia takriban dakika 2 na nusu nzima kutangaza habari hizi.

Tunategemea pia na wabunge wa Kihaya, Kichagga, Kipemba, Kimakonde, Kiluguru, Kimeru, Kipare, Kigogo, Kikiha, Kinyamwezi, Kisukuma, Kinyakyusa, Kihehe, Kingoni na kadhalika watakaochaguliwa kuwa viongozi wa kimila wa makabila yao nao watapewa fursa sawa na mwenzetu Lowassa mara muda wao wa kusimikwa utakapowadia!

WAKATI huo huo Bwana Mkubwa Yusufu Makamba anasema kwamba CCM hailei wala haiwafugi MAFISADI. Swali ambalo Watanzania wengi wamejiuliza pamoja na ngonjera za kufuata mkondo wa sheria ni kuwa vipi kama polisi ni wa CCM, Mahakama ni za CCM, TAKUKURU ni ya CCM na TBC ni ya CCM na kadhalika na kadhalika huo mkondo wa sheria utatoka wapi.

Wanachokiomba wao ni kwamba Kamanda Mkuu wa Polisi ateuliwe na Bunge, Jaji Mkuu ateuliwe na Bunge, TBC iwe shirika h uru la habari linaloendeshwa kwa ruzuku ya serikali na kiongozi wake kuchaguliwa na Bunge na sio rais na mambo kama hayo ndio tutajua kweli CCM haiwafugi wala kuwalea MAFISADI!
 
Ndugu yetu, mwenzetu Bwana Lowassa ametawazwa rasmi kuwa kiongozi wa kimila wa jamaa zetu Wamasai.

..hii haitakuwa mara ya kwanza!

Kusimikwa huko kutampa nafasi ya kufanya ziara Arusha, Arumeru, Monduli, Morogoro, Usangu na kadhalika ili kujitambulisha rasmi.

..kampeni zinapamba moto!

Shirika la Taifa la Habari Tanzania [TBC] lilitumia takriban dakika 2 na nusu nzima kutangaza habari hizi.

..kwasababu ya umuhimu wa habari yenyewe!

Tunategemea pia na wabunge wa Kihaya, Kichagga, Kipemba, Kimakonde, Kiluguru, Kimeru, Kipare, Kigogo, Kikiha, Kinyamwezi, Kisukuma, Kinyakyusa, Kihehe, Kingoni na kadhalika watakaochaguliwa kuwa viongozi wa kimila wa makabila yao nao watapewa fursa sawa na mwenzetu Lowassa mara muda wao wa kusimikwa utakapowadia!

..ukiiga tembo kunya utachanika msamba.

WAKATI huo huo Bwana Mkubwa Yusufu Makamba anasema kwamba CCM hailei wala haiwafugi MAFISADI. Swali ambalo Watanzania wengi wamejiuliza pamoja na ngonjera za kufuata mkondo wa sheria ni kuwa vipi kama polisi ni wa CCM, Mahakama ni za CCM, TAKUKURU ni ya CCM na TBC ni ya CCM na kadhalika na kadhalika huo mkondo wa sheria utatoka wapi.

..huu ni wakati wa ajabu katika historia ya tanganyika!

..tunasubiri ya firauni sasa, ya musa tushayazoea!
 
Kuishi kwingi ni kuona mengi.Ndio mana nasema, watanzania tumekwisha.Hivi hawa hawaelewi kwamba kufanya hivyo ni kujitambulisha na ufisadi wake.Haya ni maajabu ya Musa!
 
njaa kali hiyo, hakuna cha kusimikwa wala chochote, lowasa ameendelea kutumia zile pesa alizopata kwenye richmond kujijenga kimila na kisiasa, hatutamruhusu akanayage usangu labda huko morogoro watamruhusu kwa kuwa huwa wanaabudu sana vya kupewa, ndo maana wanawabunge maponjoli hadi leo
 
Haya mambo ya "kusimikana" mmh mie simo......
 
BAADA ya miaka takriban hamsini ya ubabaishaji wa ksiasa, je, huu si wakati wa Watanzania kurejeshewa uchifu na umangi.

Faida za viongozi wa Kikabila kama Adam Lusekelo anavyotuelezea kuhusu uchifu wake huko Unyakyusa ni kuwa karibu na wananchi.

Chifu Adam Lusekeleo pia analea watu wa kabila lake hususan katika masuala ya maendeleo ya jamii na kiuchumi.

Mila mbalimbali zilizowekwa toka enzi za mababu zinapotumika wanawake, watoto, wazee, walemavu, maalbino na kadhalika wanalindwa na haki zao kuangaliwa.

Matatizo ya maeneo, majimbo, kaya, ukoo na familia yanakuwa na watu wa kuyaangalia tofauti na hivi sasa ambapo hata kesi za kuku zinapelekwa mahakamani.

Uchifu utaleta ushindani katika masomo na hivyo kila eneo likijitahidi kuwasomesha watoto wao na hivyo kuchochea maendeleo ya elimu nchini.

Suala la huduma litaendelezwa na kuwafikia wananchi kwa ukaribu tofauti na hivi sasa. Aidha fedha za tiba hazitaliwa na ununuzi wa magari ya kifahari na unywaji wa peteroli na dizeli bali zitatumika kununua vifaa vinavyohitajika mahospitalini.

Madaktari na manesi kadhalika hawatakuwa na roho mbaya na wala rushwa kama ilivyo sasa.

Polisi wa chifu watakuwa ni watu walio karibu na sio mamluki wa fedha na wakubwa kiasi ambacho hupindishwa sheria mwenye hatia akawa ndio mwenye haki.

Mahakama za chifu zitakuwa wazi na hazitaruhusiwa kufanya vituko vya mahakama za wanasiasa.

Wawalishi wa machifu watakuwa ni koo za kabila husika na hawa watawatetea kwa dhati watu hao na sio kutafuta maslahi binafsi.

Kwa kuwa viongozi wa kisiasa wameshindwa kazi na sasa wameingia kwenye mashindano ya ufisadi na kushindana kwa kuwa na magari, ndege, majumba na milki nyingine za kifahari; kwa kuwa viongozi wa dini wanapigania fedha za sadaka na ruzuku toka serikalini badala ya kuendeleza dini zao; kwa kuwa wabunge wanapigania maslahi binafsi na ya jamaa zao; na kwa kuwa wasomi wetu wamekuwa kasuku wa kukariri na kuimba ya wengine badala ya kuja na ufumbuzi wa matatizo yetu ya maendeleo n inatoa wito wa herufi kubwa SASA TURUDISHIENI MACHIFU NA MANGI WETU. Na hongera Lowassa kwa kutawazwa Chifu wa Umasaini-Limbuginna!!!!
 
njaa kali hiyo, hakuna cha kusimikwa wala chochote, lowasa ameendelea kutumia zile pesa alizopata kwenye richmond kujijenga kimila na kisiasa, hatutamruhusu akanayage usangu labda huko morogoro watamruhusu kwa kuwa huwa wanaabudu sana vya kupewa, ndo maana wanawabunge maponjoli hadi leo

Na hasa afie kwingine lakini siyo Usangu Haki ya Mungu! Naanza kupiga kampeni ili asipokelewe akienda! Fisadi huyu asije ambukiza kizazi chetu! Aende hukohuko Arumeru na arusha wanakomuabudu!
 
Naomba tuanze petition kumfanya Lowassa awe Rais au mgombea wa Urais kupitia CCM 2010!

It is about time we allow him to be the president and prove everyone wrong!
 
Kuna kijana mmoja kule kijijini kwetu,alienda kujisaidia haja kubwa porini.(si mnakumbuka mambo ya huko kwetu majita).Basi kama kawaida akachuma majani ili kujisafisha baada ya shughuli yake hiyo.Huyo bwana alikuwa hakwenda mbali na njia toka pale alipochuchumaa.Mara ghafla mtumeee!! ile yuko katikati ya shughuli akamwona mama mkwe wake anakuja.Guess what??? Jamaa ilibidi ajifiche usoni kwa kutumia yale majani aliyokuwa amechuma ili ajichambie akidhani kuwa mama mkwe hatomuona.
Anyaway sina uhakika kama jamaa alifanikiwa kujificha na mama mkwe wake hakumjua sura au ndo ile kuonyesha jinsi mishipa ya aibu ilivyokatika.

Kaazi kwelikweli
 
Duuh aisee huyu Lowasa sasa jamani cheo alichobakiza ni Urais tu...!

Vyeo vyote vya kisiasa vya Ardhi ya Tanzania amevikalia au aliwahi kuvipitia...!

Sasa ameamua kutoka kikabila...!

Huyu mtu analake jambo, hapo bado, kwa vile kaoa singida, utasikia wiki ijayo kateuliwa kuwa Mkuu wa kabila la kinyaturu...! (kwa mashemeji)

Kwa vile mwanae kaolewa na Mchaga utasikia mwezi ujao kateuliwa kuwa mkuu wa kabila la wachaga...! (kwa wakwe)

Kimya kimya...! 2010 RAIS LOWASA kupitia Chama Cha Makabila (CCM)
 
Duuh aisee huyu Lowasa sasa jamani cheo alichobakiza ni Urais tu...!

Vyeo vyote vya kisiasa vya Ardhi ya Tanzania amevikalia au aliwahi kuvipitia...!

Sasa ameamua kutoka kikabila...!

Huyu mtu analake jambo, hapo bado, kwa vile kaoa singida, utasikia wiki ijayo kateuliwa kuwa Mkuu wa kabila la kinyaturu...! (kwa mashemeji)

Kwa vile mwanae kaolewa na Mchaga utasikia mwezi ujao kateuliwa kuwa mkuu wa kabila la wachaga...! (kwa wakwe)

Kimya kimya...! 2010 RAIS LOWASA kupitia Chama Cha Makabila (CCM)

Yale yaleeee go on....
 
Back
Top Bottom