Papaa Kinyani
JF-Expert Member
- Feb 25, 2013
- 1,459
- 699
Edward Lowassa, amesema matumizi ya fedha zilizorudishwa nchini, baada ya ununuzi wa rada, maarufu chenji ya rada, hayaeleweki vizuri.
Alisema hayo juzi katika mkutano uliojumuisha wadau wa elimu, unaofanyika kila mwaka wilayani Monduli mkoani Arusha ili kuangalia changamoto na mafanikio ya elimu wilayani humo. Lowassa alisema moja ya mambo yanayomsikitisha ni kuona fedha hizo, zikielekezwa kwenye ukarabati wa majengo, badala ya kujenga majengo mapya. Mara nyingi ukarabati unatumia fedha nyingi, bila kuwa na maelezo mazuri, tofauti na ujenzi wa majengo mapya. Ningefurahi kuona fedha za rada zikitumika kujenga jengo la maktaba, maabara au basi nyumba za walimu. Lakini ukisema unazipeleka kwenye ukarabati, fedha zitapotea,alisema Lowassa.
Tunamshangaa Lowassa kama mbunge na walishaelezwa bungeni kuwa fedha hizo zimeelekezwa kununua vitabu ambavyo mchakato wake unaendelea na kununua madawati ambayo tamisemi wametangaza zabuni wiki iliyopita magazetini. Sasa kwa nini awapotoshe wadau hawa wa elimu? Haoni anachonganisha serikali na wapiga kura? Je ni jengo lipi limekarabatiwa kwa fedha ya chenji ya rada? Toa takwimu sahihi mheshimiwa.
Alisema hayo juzi katika mkutano uliojumuisha wadau wa elimu, unaofanyika kila mwaka wilayani Monduli mkoani Arusha ili kuangalia changamoto na mafanikio ya elimu wilayani humo. Lowassa alisema moja ya mambo yanayomsikitisha ni kuona fedha hizo, zikielekezwa kwenye ukarabati wa majengo, badala ya kujenga majengo mapya. Mara nyingi ukarabati unatumia fedha nyingi, bila kuwa na maelezo mazuri, tofauti na ujenzi wa majengo mapya. Ningefurahi kuona fedha za rada zikitumika kujenga jengo la maktaba, maabara au basi nyumba za walimu. Lakini ukisema unazipeleka kwenye ukarabati, fedha zitapotea,alisema Lowassa.
Tunamshangaa Lowassa kama mbunge na walishaelezwa bungeni kuwa fedha hizo zimeelekezwa kununua vitabu ambavyo mchakato wake unaendelea na kununua madawati ambayo tamisemi wametangaza zabuni wiki iliyopita magazetini. Sasa kwa nini awapotoshe wadau hawa wa elimu? Haoni anachonganisha serikali na wapiga kura? Je ni jengo lipi limekarabatiwa kwa fedha ya chenji ya rada? Toa takwimu sahihi mheshimiwa.