Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,509
- 3,756
Msemaji wa Timu ya Ruvu Shooting Masau Bwire amepelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) kwa kosa la kutoa taarifa za uongo kwenye vyombo vya habari na kauli za maudhi kwa viongozi wa timu ya Polisi Tanzania FC katika mchezo uliochezwa Februari 22, 2020 uwanja wa Ushirika mkoani Kilimanjaro.
Mechi namba 240- Coastal Union 0 FC vs Yanga SC 0: Kocha wa Yanga Luc Eymael ametozwa faini ya Tsh 500,000 (laki tano) kwa kosa la kukataa kufanya mahojiano (interview) na mdhamini wa Ligi Kuu Azam Media katika mechi iliyofanyika Februari 23, 2020 uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Adhabu imetolewa kwa uzingativu wa kanuni ya 41(2) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Mchezaji na nahodha wa timu ya Yanga SC Papi Tshishimbi ametozwa faini ya Tsh. 200,000 (laki mbili) kwa kosa la kukataa kufanya mahojiano (interview) na mdhamini wa Ligi Kuu Azam Media katika mechi iliyofanyika Februari 23, 2020 uwanja wa mkwakwani mkoani Tanga.
Adhabu imetolewa kwa uzingativu wa kanuni 38(18) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Wachezaji.
Mchezo namba 233 (Polisi Tanzania vs Yanga SC): Waamuzi waliosimamia mchezo namba 223 Polisi Tanzania vs Yanga SC Abel Willium na Martin Mwalyaje wamefungiwa miezi mitatu (3) kwa kosa la waamuzi hao kushindwa kutafsiri sheria mchezo huo tajwa uliofanyika Februari 18, 2020 uwanja wa Ushirika mkoani Kilimanjaro.
Adhabu hiyo imetolewa kwa uzingativu wa Kanuni ya 39(1A) ya Udhibiti wa Waamuzi.
Mechi namba 240- Coastal Union 0 FC vs Yanga SC 0: Kocha wa Yanga Luc Eymael ametozwa faini ya Tsh 500,000 (laki tano) kwa kosa la kukataa kufanya mahojiano (interview) na mdhamini wa Ligi Kuu Azam Media katika mechi iliyofanyika Februari 23, 2020 uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.
Adhabu imetolewa kwa uzingativu wa kanuni ya 41(2) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Makocha.
Mchezaji na nahodha wa timu ya Yanga SC Papi Tshishimbi ametozwa faini ya Tsh. 200,000 (laki mbili) kwa kosa la kukataa kufanya mahojiano (interview) na mdhamini wa Ligi Kuu Azam Media katika mechi iliyofanyika Februari 23, 2020 uwanja wa mkwakwani mkoani Tanga.
Adhabu imetolewa kwa uzingativu wa kanuni 38(18) ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti wa Wachezaji.
Mchezo namba 233 (Polisi Tanzania vs Yanga SC): Waamuzi waliosimamia mchezo namba 223 Polisi Tanzania vs Yanga SC Abel Willium na Martin Mwalyaje wamefungiwa miezi mitatu (3) kwa kosa la waamuzi hao kushindwa kutafsiri sheria mchezo huo tajwa uliofanyika Februari 18, 2020 uwanja wa Ushirika mkoani Kilimanjaro.
Adhabu hiyo imetolewa kwa uzingativu wa Kanuni ya 39(1A) ya Udhibiti wa Waamuzi.