Lucia Pande ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Mtendaji Red Cross Tanzania

Lucia Pande ateuliwa kuwa Katibu Mkuu Mtendaji Red Cross Tanzania

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
IMG-20230108-WA0065.jpg
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania (TRCS) chini ya Mwenyekiti wake David Kihenzile, imemteua Lucia Pande kuwa Katibu Mtendaji wa shirika hilo.

Awali, Lucia alikua Makamu wa Rais wa shirika hilo.

Taarifa iliyotolewa ya Januari 8, 2023 inasema kuwa uteuzi wa Lucia kuwa Katibu Mtendaji kwa miaka mitatu umeanza rasmi

Uteuzi huo ni kwa mujibu wa sheria kipengele cha 37 (1) cha Kamati Kuu ya Taifa ya Shirika hilo (NEC)

Lucia, ambae ana uzoefu wa miaka 17 katika masuala ya uongozi, amewahi kufanya kazi katika Kampuni mbalimbali mbali kama Meneja Rasilimali Watu na usimamizi wa vifaa.

Baadhi ya Kampuni alizowahi kufanya kazi ni Tata Holding Ltd, Logistics, Dar es Salaam Corridor group, Kampuni ya madini ya Tanzanite One, Accasia na Barrick.
 
Young, beautiful, wild and single, mwenye namba anijuze 😎 😎
 
Huyu hateuliwi na Rais?, maana mpaka wenyeviti wa petrol station wanateuliwa na huyu bibi
 
Back
Top Bottom