Lucile Randon: Binadamu mpweke zaidi duniani

Lucile Randon: Binadamu mpweke zaidi duniani

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
4,805
Reaction score
17,850
Huyu ni Mtawa wa Kifaransa, Lucile Randon. Ana umri wa miaka 118 na ndiye mtu mzee zaidi ulimwenguni. Alizaliwa tarehe 11.02.1904.

Marafiki zake wote, na jamaa aliowajua wameshakufa. Yeye ni kipofu na anatembelea kiti cha magurudumu.
Kwa sababu ni mtawa, hivyo hana watoto wala wajukuu. Mnamo 2021, alisema anatamani angejiunga na jamaa zake mbinguni.

Randon alipokea zawadi kutoka kwa Emmanuel Macron katika siku yake ya kuzaliwa ya miaka 118 mnamo Februari 2022. Lakini aliona kuwa "heshima ya kusikitisha" kwani "ingekuwa bora zaidi kama angekuwa ameshaenda mbinguni".

Unaweza kuwa mpweke sana katikati ya watu. Mwili wake uko katika ulimwengu huu lakini moyo wake haupo tena hapa.

IMG_20221011_133906.jpg
 
Maskin [emoji2301][emoji2301] pole zake
Uzee mbaya sana hasa ukiwa huna hata wajukuu au mume
 
Maskin [emoji2301][emoji2301] pole zake
Uzee mbaya sana hasa ukiwa huna hata wajukuu au mume
Inategemea,

Kwa mfano masista na mapadre wanaamini watawa wenzao wanaowazunguka ndiyo dada zao, kaka zao, mama zao, baba zao nk.

Na wote wanaunganishwa na KRISTU katika familia yao.

Kwa hiyo kwao kutokuwa na familia kama zetu siyo tatizo, sababu ya uchaguzi wao kwa kuwa wana wito huo.
 
Huwezi kosa ndugu duniani huo ni uongo

Let's assume Nina miaka 40 sina uzazi watoto wa Kaka yangu Wana 3month up to 15yrs Hadi niwe na 80 yule wa 3month tayari Ana 40yrs plus muda huo ana watoto kadhaa ambao wale badae kidogo Wana wajukuu ambao pia ni ndugu zangu
 
Hivi waliozeeka sana wale mke na mume huwa wanauwezo wa kufanya tendo la ndoa au ndo wanakuwa hawana nguvu??
Hata kama wasiposhiriki tendo lakin wanakuwa pamoja wanapiga stori ,wanakula pamoja hiyo ni tosha kabisa inasaidia kukufanya usiwe mpweke,ile akili tu kujua tu ndani kuna mwenzangu ni tiba tosha ya upweke
 
Inategemea,

Kwa mfano masista na mapadre wanaamini watawa wenzao wanaowazunguka ndiyo dada zao, kaka zao, mama zao, baba zao nk.

Na wote wanaunganishwa na KRISTU katika familia yao.

Kwa hiyo kwao kutokuwa na familia kama zetu siyo tatizo, sababu ya uchaguzi wao kwa kuwa wana wito huo.
Lakin upweke lazima utapata tu
 
Back
Top Bottom