Lucy Lameck: Mwanamke wa kwanza kuwa Waziri Tanganyika na Tanzania

Lucy Lameck: Mwanamke wa kwanza kuwa Waziri Tanganyika na Tanzania

Influenza

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2018
Posts
1,509
Reaction score
3,756
Lucy Lameck amezaliwa huko mkoani Kilimanjaro mnamo mwaka 1934, alikuwa Mwanamke msomi ndani ya TANU, aliyehimu Vyuo Vikuu vya Oxford Nchini Uingereza na Michigan, Marekani

Alikuwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya Uwaziri Serikalini na kwa mara ya kwanza aliingia Bunge la Tanganyika mwaka 1960 kabla ya kuchaguliwa kwenye Bunge la Tanzania mwaka 1965

Alisoma mafunzo ya Unesi na baada ya kumaliza mwaka 1950 hakutaka kufanya kazi Mfumo wa Afya wa Kikoloni wa Uingereza na badala yake alianza kufanya kazi kama Katibu Mukhtasi

Kati ya mwaka 1955 na1957, alifanya kazi ‘Kilimanjaro Native Cooperative Union, na alianza kuingia kwenye siasa akifanya kazi na TANU. Akiwa TANU alikuwa Kiongozi wa Kitengo cha Wanawake na alisanifu vazi la Kitaifa la Wanawake wa Tanganyika

Kati ya Mwaka 1962 na 1965 alikuwa Waziri wa Ushirika na Maendeleo ya Jamii ikiwa ni nafasi ya kwanza ya Uwaziri kushikwa na Mwanamke kwa Tanganyika na Tanzania

Baada ya Tanzania kuundwa ashika nafasi ya Naibu Waziri wa Ushirika na Maendeleo ya Jamii kati ya mwaka 1965 na 1970 na pia Naibu Waziri wa Afya kati ya mwaka 1967 na 1972

Akiwa amezaliwa katika familia ya wakulima, amefanya kazi maisha yake yote kuimarisha hali za Wanawake nchini hadi alipofariki Machi 1993 kutokana na Magonjwa ya Figo.

- Barabara ya Ujerumani kupewa jina la mwanaharakati wa Tanzania, Lucy Lameck. Alikuwa Waziri wa 1 mwanamke wa Tanzania

- Mashujaa wa Mlima Kilimanjaro: Lucy Lameck na Yusuf Olotu

1606459230615.png

1606459162736.png

0CF1D2A1-C442-491E-BD93-93CBCE59C9AC.jpeg
 
Aliwahi sana kuja duniani...wasomi na wanasiasa wanawake kama hawa walitaka tuwenao leo...kwa sasa tunao hawa waimba Mapambio ni kusifu tu asbh hadi jioni...bila hata kuhoji why?
 
Baada ya Tanzania kuundwa ashika nafasi ya Naibu Waziri wa Ushirika na Maendeleo ya Jamii kati ya mwaka 1965 na 1970 na pia Naibu Waziri wa Afya kati ya mwaka 1967 na 1972
Hapo sijaelewa ina maana alikuwa naibu waziri wa wizara mbili kwa wakati mmoja.
 
Tumkumbuke Mwanamke wa kwanza kuwa Waziri,Tanganyika,ambayo sasa ni Tanzania.Jina lake liko kwenye barabara ya nchini Ujerumani.Mwenye zaidi kuhusu huyu Mama,atuletee makala,inayomhusu kwa urefu.
 
Aliwahi sana kuja duniani...wasomi na wanasiasa wanawake kama hawa walitaka tuwenao leo...kwa sasa tunao hawa waimba Mapambio ni kusifu tu asbh hadi jioni...bila hata kuhoji why?
Kusifu na kuabudu
 
Kisa ni mweusi ndo maana hamtaki kuuendeleza uzi kuhusu, angekuwa mweupe............

Hebu kuweni na huruma jameni
 
Ninachojua kuhusu huyu Lucy Lameck ni kwamba alikuwa anatembezewa rungu na mwalimu J K Nyerere.

Hayo tu.
 
Back
Top Bottom