Lugha maridhawa. KISWAHILI

Lugha maridhawa. KISWAHILI

Mwanahisa

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2012
Posts
1,382
Reaction score
513
Msaada tutani tafadhali.

Kandambili, hilo neno mbili linahusiana na tarakimu ya namba 2?

Je (sandals) au Open shoe kwa lugha yetu sanifu ni nini?
 
sandals...open shoes = makobasi.....
 
Mwanahisa kwa mujibu wa Kamusi ya TUKI

sandal n = ndara; makubadhi, kandambili, malapa.

~led
adj liovaa ndara.
 
Preta aksante, Dotworld je TUKI wanasemaje juu ya neno mbili, kwasababu ziko mbili nikimaanisha JOZI au ni kushabihiana kwa maneno tu?
 
Last edited by a moderator:
kUMEKUWA NA MCHANGANYO WA TAFSIRI TOFAUTI KWA MANENO HAYA,
AGHALABU.......?
YUMKINI...........?
UPEMBUZI YAKINIFU.........?
MARIDHAWA....................?
MURUA............................?
 
kUMEKUWA NA MCHANGANYO WA TAFSIRI TOFAUTI KWA MANENO HAYA,
AGHALABU.......?
YUMKINI...........?
UPEMBUZI YAKINIFU.........?
MARIDHAWA....................?
MURUA............................?

Aghalabu====Mara nyingi
Upembuzi yakinifu===Mchanganuo
Maridhawa=====Maridadi, nzuri, yakupendeza,Safi,Njema,siha nzuri
Murua======Safi , njema, maridadi,pendeza,enye afya.

Masahihisho nayapokea
 


Aghalabu====Mara nyingi
Upembuzi yakinifu===Mchanganuo
Maridhawa=====Maridadi, nzuri, yakupendeza,Safi,Njema,siha nzuri
Murua======Safi , njema, maridadi,pendeza,enye afya.

Masahihisho nayapokea
Asante kwa kupembua ipasavyo ndugu!
 
Preta aksante, Dotworld je TUKI wanasemaje juu ya neno mbili, kwasababu ziko mbili nikimaanisha JOZI au ni kushabihiana kwa maneno tu?

Hiyo mbili kwenye kanda mbili, ni zile kanda mbili zinazounganika kwenye kidole.

Yaani unakuwa na sehemu ya flat unapoweka unyayo wako, na zile kanda [mbili] zinazoshikulia unyayo wako usiondoke kwenye kiatu

Hiyo ndio asili ya mbili kwenye kandambili, na sio maana ya jozi
 
Hiyo mbili kwenye kanda mbili, ni zile kanda mbili zinazounganika kwenye kidole.
Hiyo ndio asili ya mbili kwenye kandambili, na sio maana ya jozi
Shukrani Gaijin
 
kanda mbili...ile mikanda miwili...Sandals ndo open shoes ambazo ndo makobasi.... Preta umenikumbusha mbali....:eek2:
sandals...open shoes = makobasi.....
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom