Lugha ya Kiswahili ilitakiwa iwe chaguo la pili nchini kwetu

Lugha ya Kiswahili ilitakiwa iwe chaguo la pili nchini kwetu

code4494

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2014
Posts
813
Reaction score
1,227
Habari za majukumu ndugu zangu,

Nimekuwa nikijiuliza faida ya vitendawili, ngano, methali na lugha nzima ya kiswahili kwa ujumla ni nini mpaka imekuwa lugha ya taifa? Amini usiamini lugha ya kiswahili imekuwa ni mojawapo ya sababu kubwa ya kurudisha nyuma maendeleo ya taifa letu. Ni lugha changa sana haina misamiati ya kutosha..

Inatusababisha kutokujiamini, kukosa ubunifu, upungufu wa maarifa, kutokujua dunia inataka nini kwa sasa, kutokuwa na wataalamu thabiti wenye ushindani katika soko la ajira.

Kwa mtazamo wangu bora lugha ya kiswahili ingekuwa ya pili, kiingereza iwe lugha ya kwanza. Mitaala ibadilishwe watoto waanze kufundishwa tokea shule za msingi hii itajenga taifa bora na lenye ushindani.

Asanteni
 
Wakati Keny wanaifanya kiswahili kiwe cha kwanza
 
Sidhani kama kutojiamini kunaletwa na lugha. Kutojiamini ni mentality tu. Unaweza kujiamini kama ukibadili mentality yako hata kama hujui Kiswahili. Nafikiri tatizo letu la siku nyingi ni kwamba hatuna dira thabiti kwamba tunaenda wapi kwenye kila eneo. Long term plan ambayo imevunjwavunjwa kwenye sub-plans hakuna.
 
Sidhani kama kutojiamini kunaletwa na lugha. Kutojiamini ni mentality tu. Unaweza kujiamini kama ukibadili mentality yako hata kama hujui Kiswahili. Nafikiri tatizo letu la siku nyingi ni kwamba hatuna dira thabiti kwamba tunaenda wapi kwenye kila eneo. Long term plan ambayo imevunjwavunjwa kwenye sub-plans hakuna.
Nimeongea kutokujiamini kwa sababu huwa naona kwenye interview pale lugha ikitumika ya kiingereza..inakuwa ngumu kujieleza kwa kujiachia kama endapo ungeulizwa kwa kiswahili...mf angalia wasanii wetu wakihojiwa kwenye tv za kimataifa kwa kiingereza linganisha wakihojiwa hapa kwetu kwa kiswahili..na sio wasanii tu..hata baadhi ya viongozi wetu...
Amini ndugu yangu kiswahili kinaturudisha nyuma sana
 
Wakati Keny wanaifanya kiswahili kiwe cha kwanza
Wanakifanya hvyo kwakuwa tayari kiingereza sio tabu...ni sawa na mtu anakuambia ajira sio ishu bora kujiajiri mwenyewe wakati yeye ana degree we umeishia form four...yeye tayari anamachaguo mengi
 
Nimeongea kutokujiamini kwa sababu huwa naona kwenye interview pale lugha ikitumika ya kiingereza..inakuwa ngumu kujieleza kwa kujiachia kama endapo ungeulizwa kwa kiswahili...mf angalia wasanii wetu wakihojiwa kwenye tv za kimataifa kwa kiingereza linganisha wakihojiwa hapa kwetu kwa kiswahili..na sio wasanii tu..hata baadhi ya viongozi wetu...
Amini ndugu yangu kiswahili kinaturudisha nyuma sana
Hicho unachokisema code4494 nakubalina nawe kabisa. Labda tu mimi nimelitazama kwa mbali zaidi kwamba kama tungekuwa na malengo ya muda mrefu, tungeandaa walimu wazuri na kukawa na judhudi za kubadili mentality ya watu kitaifa (tuache kujiona hatuwezi) basi shida hii ingeondoka. Amini usiamini watz wanaojua Kiingereza wanaongea vizuri sana, tena bila accent kama mataifa mengine.
 
Habari za majukumu ndugu zangu,

Nimekuwa nikijiuliza faida ya vitendawili, ngano, methali na lugha nzima ya kiswahili kwa ujumla ni nini mpaka imekuwa lugha ya taifa? Amini usiamini lugha ya kiswahili imekuwa ni mojawapo ya sababu kubwa ya kurudisha nyuma maendeleo ya taifa letu. Ni lugha changa sana haina misamiati ya kutosha..

Inatusababisha kutokujiamini, kukosa ubunifu, upungufu wa maarifa, kutokujua dunia inataka nini kwa sasa, kutokuwa na wataalamu thabiti wenye ushindani katika soko la ajira.

Kwa mtazamo wangu bora lugha ya kiswahili ingekuwa ya pili, kiingereza iwe lugha ya kwanza. Mitaala ibadilishwe watoto waanze kufundishwa tokea shule za msingi hii itajenga taifa bora na lenye ushindani.

Asanteni
Sifa mojawapo lugha ni hiyo. Hakuna lugha bora zaidi ya nyingine. Ndiyo maana kila lugha ina tabia ya kukupa misamiati toka lugha nyingine.
 
  • Thanks
Reactions: ywf
Umeandika tu. Hujatoa sababu kwa vielelezo.
 
Kitu cha msingi hapa si kubadili Lugha....
Tuiweke mitaala katika kiwango kimoja, pia kupunguza idadi ya masomo kwa mwanafunzi mmoja..
 
Hicho unachokisema code4494 nakubalina nawe kabisa. Labda tu mimi nimelitazama kwa mbali zaidi kwamba kama tungekuwa na malengo ya muda mrefu, tungeandaa walimu wazuri na kukawa na judhudi za kubadili mentality ya watu kitaifa (tuache kujiona hatuwezi) basi shida hii ingeondoka. Amini usiamini watz wanaojua Kiingereza wanaongea vizuri sana, tena bila accent kama mataifa mengine.
Mfano hapa kwetu niwatumiaji wazuri sana wa mitandao ya kijamii...lakini tunaitumia kwa tija?tuwe tu wakweli jamani...asilimia kubwa hatutumii kwa manufaa na maendeleo...Ndio maana jambo dogo tu ambalo mtu angeweza ku-Google akapata maelezo kamili..nakuja kuuliza huku...mwisho wa siku mtu anamezeshwa uongo..nae anaenda kuusambaza kwa wengine...ndio maana hapa kwetu vitu vya uzushi ni viingiii mno!
Na wala silaumu hilo hiyo ni kutokana vitu vingi ambavyo ni productive viko katika lugha ngeni....
Imefikia hatua tumeishiwa misamiati tumeamua kuchukua maneno ya kiingereza mf kama "stress","share", "inatreand" kuyaweka sehemu ambapo hata haistahili...kwa nini tusiingie moja kwa moja kwenye kiingereza kuliko kuchovya chovya?
 
Tukubali hii lugha sio rafiki kwa mazingira ya dunia ya Leo ..
Kama huamini nenda kawaulize mafundi gereji kama kuna spea yoyote ya gari wanayoitamka kwa kiswahili
 
Ongea basi unachokijua
hamna lugha bora kuliko lugha nyingine duniani,kila lugha inakidhi mahitaji ya mawasiliano kwa watumiaji wa lugha hiyo na lugha hukua na kuduma ndomaana kiswahili cha zamani ni tofauti na chasaivi(badhi ya misamiati imepotea) na lugha inakua kwa kupata misamiati mipya ambayo husanifiwa na kuingizwa kwenye lugha rasmi,kiswahili kilisanifiwa 1930(kama sijakosea)mpaka leo,kiswahili hakija sanifiwa tena,kwaio kinachotakiwa kufanyika ni kiswahili kisanifiwe ili lugha iweze kupata misamiati mipya ili kuondokana na matumizi ya misamiati yakigeni(kingereza)ambao hudhoofisha lugha na sio kufanya kingereza kuwa lugha ya kwanza tz.na kama unavyojua lugha hubeba utamaduni wa watumiaji wake,suala kama la ushoga ambalo limeenea sana marekani na baadhi ya nchi zinazotumia kingereza linaweza likavamia nchi yetu na kuharibu utamaduni wetu.kiufupi kuna matokeo hasi mengi sana ambayo yatatokea endapo kingereza kitatumika kama lugha ya kwanza katika nyanja zote,kiuchumi,kisiasa na kijamii
Ongea basi unachokijua
 
Mfano hapa kwetu niwatumiaji wazuri sana wa mitandao ya kijamii...lakini tunaitumia kwa tija?tuwe tu wakweli jamani...asilimia kubwa hatutumii kwa manufaa na maendeleo...Ndio maana jambo dogo tu ambalo mtu angeweza ku-Google akapata maelezo kamili..nakuja kuuliza huku...mwisho wa siku mtu anamezeshwa uongo..nae anaenda kuusambaza kwa wengine...ndio maana hapa kwetu vitu vya uzushi ni viingiii mno!
Na wala silaumu hilo hiyo ni kutokana vitu vingi ambavyo ni productive viko katika lugha ngeni....
Imefikia hatua tumeishiwa misamiati tumeamua kuchukua maneno ya kiingereza mf kama "stress","share", "inatreand" kuyaweka sehemu ambapo hata haistahili...kwa nini tusiingie moja kwa moja kwenye kiingereza kuliko kuchovya chovya?
Kila lugha inakopa, niambie "ugali" kwa kiingereza unaitwaje?
 
Tukubali hii lugha sio rafiki kwa mazingira ya dunia ya Leo ..
Kama huamini nenda kawaulize mafundi gereji kama kuna spea yoyote ya gari wanayoitamka kwa kiswahili
Uvivu wa kujisomea, nunua kamusi ya TUKI English-Kiswahili utakuta majina mengi ya spana nk, pia KAMUSI KUU YA KISWAHILI hata bei yake huijui. Punguza jazba uje na hoja.
 
Habari za majukumu ndugu zangu,

Nimekuwa nikijiuliza faida ya vitendawili, ngano, methali na lugha nzima ya kiswahili kwa ujumla ni nini mpaka imekuwa lugha ya taifa? Amini usiamini lugha ya kiswahili imekuwa ni mojawapo ya sababu kubwa ya kurudisha nyuma maendeleo ya taifa letu. Ni lugha changa sana haina misamiati ya kutosha..

Inatusababisha kutokujiamini, kukosa ubunifu, upungufu wa maarifa, kutokujua dunia inataka nini kwa sasa, kutokuwa na wataalamu thabiti wenye ushindani katika soko la ajira.

Kwa mtazamo wangu bora lugha ya kiswahili ingekuwa ya pili, kiingereza iwe lugha ya kwanza. Mitaala ibadilishwe watoto waanze kufundishwa tokea shule za msingi hii itajenga taifa bora na lenye ushindani.

Asanteni
you are dingy floozy
 
Habari za majukumu ndugu zangu,

Nimekuwa nikijiuliza faida ya vitendawili, ngano, methali na lugha nzima ya kiswahili kwa ujumla ni nini mpaka imekuwa lugha ya taifa? Amini usiamini lugha ya kiswahili imekuwa ni mojawapo ya sababu kubwa ya kurudisha nyuma maendeleo ya taifa letu. Ni lugha changa sana haina misamiati ya kutosha..

Inatusababisha kutokujiamini, kukosa ubunifu, upungufu wa maarifa, kutokujua dunia inataka nini kwa sasa, kutokuwa na wataalamu thabiti wenye ushindani katika soko la ajira.

Kwa mtazamo wangu bora lugha ya kiswahili ingekuwa ya pili, kiingereza iwe lugha ya kwanza. Mitaala ibadilishwe watoto waanze kufundishwa tokea shule za msingi hii itajenga taifa bora na lenye ushindani.

Asanteni


Kwanini umetumia neno chaguo? Hatujachagua kuongea Kiswahili bali ni Lugha yetu ni kama vile kuuliza kwa nini umezaliwa na Mzazi xyz na siyo abc!
Fanya kazi kijana, Lugha haijawahi kumzuia mtu kufanikiwa, haijawahi kutokea Dunia hii!
 
Nimeongea kutokujiamini kwa sababu huwa naona kwenye interview pale lugha ikitumika ya kiingereza..inakuwa ngumu kujieleza kwa kujiachia kama endapo ungeulizwa kwa kiswahili...mf angalia wasanii wetu wakihojiwa kwenye tv za kimataifa kwa kiingereza linganisha wakihojiwa hapa kwetu kwa kiswahili..na sio wasanii tu..hata baadhi ya viongozi wetu...
Amini ndugu yangu kiswahili kinaturudisha nyuma sana
Hapana cha msingi kiswahili kikazaniwe kiwe ni lugha ya kujifunza na kufundishia mpaka vyuoni na asasi mbalimbali hapa nchini hatuwez kuwa mtumwa wa mwingereza mpaka lini?.
 
Back
Top Bottom