Luiz Suarez asahau Passport Yake, Kuelekea London

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,277
Reaction score
8,860
Arsenal karibia ibahatike na zawadi ya kushangaza kutoka kwa mshambuliaji wa kilabu ya Barcelona Luis Suarez baada ya mchezaji huyo kuwacha pasipoti yake nyumbani kabla ya timu yake kuondoka kuelekea mjini London.

Haijulikani iwapo alisahau cheti hicho cha kusafiria kwa kusahau au la lakini ni bahati mbaya kwa mashabiki wa Arsenal, mtu mmoja kutoka kilabu hiyo alitumwa kwa nyumba ya raia huyo wa Uruguay ili kuichukua na mchezaji huyo alifanikiwa kuondoka na kikosi kizima cha Barcelona.

BBC
 
Leo washika mitutu wa London wanapumua chini chini kama paka aliyeona panya, sijui kama watanusurika kupigwa chini ya tatu maana combination ya Messi, Neymar na Suarez ni hatari haijawahi kutokea!
 
Afadhari wawepo wote!
Akikosekana mmoja na tukawapiga mtaanza oooh Fulani hakuwepo, sijui nini!
Waje kamili tuwapige wakiwa kamili!!
 
Bahati kivipi?
Alafu europe sio kama Dar kwenda China, ni mwendo wa Private Jet.
WASITAFUTE VISINGIZIO, LEO LAZIMA WAKAE.
Hamna cha Ooooh, sijui tuko na jet leg mara Suarez amechoka ilibidi akimbie tena nyumbani kuchukia passport, DOZI IKO PALE PALE! 3-1 in favor pf the gunners.
 
Huyo aliyetumwa nae mjinga sana angepotea na yeye.....
 
Ngojeni awang'ate maana mnamsema Sana.... ng'atu
 
Tuombe isitokee kadi nyekundu bdae ikawa ooooh sababu ya ile kadi ndio maana ikawa vile.......
 
kwa akili yako unadhani ukitumia private jet huhitaji passport!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…