Lulu asema umasikini ulipaswa kuwa dhambi

Msanii maarufu wa Bongo Movie Elizabeth Michael "Lulu" wakati akifanyiwa interview nyumbani kwake,amesema kuwa anachukia umasikini na amedai kuwa umasikini ulipaswa kuwa sehemu ya dhambi.

Mbona dhambi ya Usi#e na Usizini amezitenda? kwahiyo hata hiyo ya umasikini nayo anaendelea kuitenda.
 
ila lulu huwa anajielewa hayo mengine makosa ya kawaida...mdogo ila ana akili
 
Na Afahamu pia kuwa Tajiri haingii Mbinguni
 
Usikariri kusoma ndio kufanikiwa, kuna watu walioendelea dunia hawajasoma. kama wachezaji wa mpira, waimbaji n.k

Kuna mtu aliwadanganya watanzania kuwa ktk dunia hii ya ushindani unaweza kutoboa bila elimu matokeo yake jitu lina miaka 50 linaishi kwa wazazi na bado linaona ni sawa tu.
 
Kumbe pamoja na uchangu una Akili pia!


Sijaona akili hapo maana yeye mwenyewe anajua kabisa uzinzi ni dhambi lakini hajaacha bado tunaambiwa kua tajiri kuona ufalme wa mbingu ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano labda kama anataka kubadili tamko la Mungu.
 
Kuna amri za Mungu zinasema 'Usiue, Usizini'...hakuna inayosema 'Usiwe Masikini'!

alisema ulipaswa.....kwamba Mungu katika amri zake angeweka na amri hiyo....
 
Akiolewa atasema kuishi singo ilipaswa kuwa dhambi....akipata mtoto atasema kukosa mtoto ilipaswa kuwa dhambi....akipata watoto wanne atasema kufa umezaa mtoto mmoja ilipaswa kuwa dhambi.

Hapo tuombe tu asije kuwa MUNGU coz lazima ataDELETE dhambi ya kuua na kuzini kwenye zile amri kumi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…