Lulu: Wanaume wote huzaliwa wakiwa na usaliti

Lulu: Wanaume wote huzaliwa wakiwa na usaliti

Money Stunna

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2011
Posts
13,053
Reaction score
6,304


Mrembo na mwigizaji wa filamu mwenye mvuto zaidi hapa Bongo (kwa mujibu wa mtandao wa yourbesttop10.com), Elizabeth Michael ‘Lulu' jana usiku aliandika bandiko mtandaoni ambalo liliwaacha midomo wazi baadhi ya mashabiki wake akiwashutumu wanaume wote kuwa wamezaliwa wakiwa tayari wanausaliti na kuwa ni swala la kusubiri ni lini tu atafanya na kuwatahadhalisha wanawake wakaechonjo kwenye mahusiano yao.

Lulu aliandika ujumbe huo kwa lugha ya ‘KIMOMBO' "All men are born hardwired to betray, it's just a question of when! don't get too comfortable".

Kwa wale wafuatiliaji wa tamhilia ya REVENGE ya huko majuu , haya maneno sio mgeni kwao kwani mwanadada Victoria alishawahi kuyatamka. Kutokana na picha ya sura ya upole aliyoibandika kabla ya kuandika maneno haya ilipelekea mashabiki kumuuliza kama amefanyiwa usaliti au.

Huku wengine wakimpa pole, mbali na mashabiki wake kumtaka afunguke zaidi juu ya kile kilichompata mwanadada Lulu hakujibu chochote. Hivi jamani kauli hii ya wanaume wote kujawa na usaliti ndani ni kweli.
 
Hayo ni matokeo ya kuumizwa au kusalitiwa.
 
Kwa hiyo na Babake nae ndio yuko kwenye fungu hilo hilo au yeye sio mwanamme?
 
Hiyo ni tafisiri hasi tu,huo siyo usaliti bali ni suala la maumbile. Mwanaume siyo rahisi kuwa na mwanamke mmoja tu. Nakumbuka baada ya kuoa mwaka 1997,nilikaa kwa baba mwaka 1 mwaka uliofuata nikajitegemea. Baba alinipa ng'ombe 10,majike saba na madume 3,ktk hayo madume 3 mawili yalikuwa yamehasiwa. Dume la kuyapanda majike 7 nilipewa moja tu(tunaita Nzagamba). Huwezi kuamini pamoja na kuwa na majike 7 ktk zizi moja,bado nzagamba lilikuwa linatoroka kwenda zizi la jirani! Na wanaume binadamu wote wako hivyo. Wanaweza kujifanya kuandika porojo tu hapa lkn huo ndo ukweli!
 
Si kweli na si wote ,shida watu wanataka kualalisha uzinzi tu hapa.Mimi sijakutana nao na kula siku naomba Mungu nisikutane nao na wasiwe hata ndugu zangu wala watoto wangu.Vitu vingine vipo kwa sababu mnaviumba wenyewe na midomo yenu na fikra zenu.Binadamu alipewa uwezo mkubwa na Mungu ukitamka udhaifu juu yako utakua dhaifu kweli,ukijiaminisha hiki kitu siwezi fanya utafanya kweli
 
Kwenye familia au jamii mkianza kusema hiki kitu hakiwezekani au lazima wanaume wote wadanganye basi unaumba laana hiyo kwa jamii yako na hata ndoa yako.Lulu hatakaa apate mwanaume asiye danganya kwa sababu ameshaweka kwa kichwa yake na kuumba maisha yake ya mahusiano that way
 
Huenda ni kweli coz wafugaji wa kuku wanajua kuwa
uwiano wa majogoo na matetea ni 1:5
kama ndivyo,no wonder hata kwa binadamu ikawa hivyo
japokuwa sina uthibitisho wa kisayansi.
 
Uzinzi mtupu!!!!!!!!!! Shida kalianza mapema!
 
Huyo lulu yeye anausafi gani? ulitendalo ndiyo likurudialo! ameanza bado mtoto mdogo sana! ukweli inasikitisha sana, ukisimama kwa upnde wa mzazi...ajiangalie yeye kwanza matendo yake
 
WHAT IF I SAY.."All women are born to ''kill'', it's just a question of when….! don't get too comfortable"
..generalization aint good,especially when it comes to such aspects(gender)

Mh! hapa mkuki mtamu kwa nguruwe kwa binadamu .......
 
All men and women are born to betray and kill. That's all.
 
Back
Top Bottom