Lunyungu ( JF member) is seriously ill ! - UPDATES


Madaktari wa Tanzania ni mzigo sana kama ulivyosema,najaribu kufikiria kama watu wenye access ya kukutana na best dooctors in the country hampati huduma nzuri najiuliza wale walioko pembezoni si ndiyo wanazikwa wakiwa wazima?

Nilipoteza mtoto kwa uzembe mkubwa wa hawa madaktari wetu kibaya zaidi walikuwa wabishi kutoa referral japokuwa walikuwa wanashindwa ku-establish pasipo na shaka tatizo hasa la mtoto.

Mimi nimewasamehe lakini ninapata wasiwasi sana na uwezo wao hata pale ambapo vifaa vya uhakika vya kitabibu wanavyo! Wanabahatisha kwenye maisha ya watu mhhh!
 

Mkuu mimi sina la zaidi la kusema zaidi ya kumshukuru Mungu na kukupa pole kwa maumivu uliyopitia.Mungu azidi kukutia nguvu.Nakuomba usiwe na hasira na mtu,yote wewe mshukuru Mola.Tunazidi kukuombea.Ila kusema kweli naomba nikusumbue kidogo cancer na AC ya gari wataalam wanasema vinahusiana vipi?
 

Pole Mpendwa wetu Lunyungu, bado uko katika maombi yetu

Hapo kwenye Red, kwa kweli nimetishika... Ukizingatia sisi tunadhani sifa tuweka Ac 24/7, kwenye gari, nyumbani, ofisini...

Mungu Tunusuru
 
Pole sana mkuu na hongera kwa kuweza kutembea tena........

Vipi umesharudi katika hali ya kawaida na kuendelea na shughuli zako za kila siku?

Nazidi kukuombea, Mungu mkubwa.
 
Ahsante sana Lunyungu Kwa taarifa. Naomba watu wote tumshukuru na kumtukuza Mungu...

Nilipata bahati ya kuongea na Lunyungu wakati anaendelea na matibabu na inatia moyo sana kupata mshindo nyumba (feedback) kutoka kwake mwenyewe.

Namwomba mhusika atuandikie walau makala ili tuweke kwenye kumbukumbu zetu. Naamini itasaidia kuokoa maisha ya watu wengi ambao wanafanyiwa au kupewa tiba isiyo sahihi na kuumizwa zaidi badala ya kuponywa...Ile kesi ya upasuaji wa kichwa vs mguu ilitakiwa kutustua. Kwa vile sisi tuna vichwa vya kuku, huwa hatukawii kusahau na kuendelea na mambo yetu ya kawaida huku tukusubir kusikia nani atakuwa next victim!!

Hongera na pole sana mkuu!
 
Mkuu sredi ya mwaka jana hii, stuka.

Swahiba ndo anatupa updates hapa!

Ndo nimeona hapa, ujue nilichangia kwa kukurupuka, kumbe mchizi alishaenda yuropa!! na hali yake inshallaah Mungu anasaidia.
 
Ndo nimeona hapa, ujue nilichangia kwa kukurupuka, kumbe mchizi alishaenda yuropa!! na hali yake inshallaah Mungu anasaidia.
Mkuu usichezee watu wengine kama unavyochezea ODM........... hilo neno hapo laweza zua kizungumkuti...........
 

Madaktari wa Tanzania ni mzigo sana kama ulivyosema,najaribu kufikiria kama watu wenye access ya kukutana na best dooctors in the country hampati huduma nzuri najiuliza wale walioko pembezoni si ndiyo wanazikwa wakiwa wazima?

Nilipoteza mtoto kwa uzembe mkubwa wa hawa madaktari wetu kibaya zaidi walikuwa wabishi kutoa referral japokuwa walikuwa wanashindwa ku-establish pasipo na shaka tatizo hasa la mtoto.

Mimi nimewasamehe lakini ninapata wasiwasi sana na uwezo wao hata pale ambapo vifaa vya uhakika vya kitabibu wanavyo! Wanabahatisha kwenye maisha ya watu mhhh!
 
lunyungu pole na asante kwa kuwa na fadhila ya kuja kutujulisha maendeleo ya afya yako.
 
kashapona jamani.
Ndio anatujulisha hivyo.

JF bana, watu huwaga wakati mwingine hawasomi hata michango ya wengine basi utakuta anarudia kile kile, au anaongelea jambo la zamani kama vile ndo linaendelea sasa. (hata tarehe ya bandiko hatusomagi) kuna siku watu walishobokea nafasi za kazi kumbe deadline ilikuwa mwaka jana! (great thinkers indeed)
 
Mungu akulinde na akuzidishie afya ya yako kila mshale uliorushwa na utakao rushwa kwako na abilisi na mawakala wake uwarudia wenyewe in Jesus name!
 
mama weeee...........pole sana lunungu ..na unaweza kukuta hao madaktari walisoma nje ya nchi...
like fisadi chenge ..kasoma chuo kizuri ,,lakini mwizi tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…