Lwakatare anaruhusiwa kuitisha press confrence kueleza umma kilichotokea baada ya kupata dhamana?

Lwakatare anaruhusiwa kuitisha press confrence kueleza umma kilichotokea baada ya kupata dhamana?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Mtu pekee ambae bila shaka umma una hamu ya kusikia kauli yake kuhusu ukweli wa ile video ambayo baadhi wamedai ni fake na wengine kudai ni ya kweli ni Lwakatare mwenyewe.

Maelezo ya nini kilitokea na ilikuwaje akaonekana kwenye hiyo video kutoka kwenye kinywa chake kitatusaidia kubaini ukweli hasa wa nini kilitokea.Japokuwa nae ni mtuhumiwa na kwa vyovyote vile ataeleza kwa namna ya kujilinda ila kwa kuzingatia taarifa zilizopo mpaka sasa kuhusu swala hili na ukweli kuwa wengi wetu tumeshuhudia hiyo video basi vyovyote vike atakavyoongea itakuwa ni swala la sisi kuunganisha dots tu kupata ukweli wa ni nini hasa kilitilokea.

Tumeshasikia na kusoma mengi juu ya jambo hili,kuanzia kauli za wanasiasa na watu wengine wakiwemo wataalam wa video,mtu pekee na pengine muhimu kuliko wote ni Lwakatare mwenyewe.Kauli ya Lwakatare,kwa vyovyote vile,itajibu maswali yaliyomo vichwani mwetu kuhusu tukio hili ambao wengi tunaliona ni kama mchezo wa kuigiza.

Sasa swali,Je, iwapo ataachiwa kwa dhamana baada ya kukamatwa kwa mara ya pili ataruhusiwa kuongelea jambo hilo?Au ndio itakuwa kama kawaida kwamba kesi iko mahakamani na hivyo jambo hiliol haliwezi kujadiliwa popote pale au hata kulitolea taarifa yoyote ile?

Wataalamu wa sheria mtusaidie ni nini Lwakatare anachoweza kufanya na nini haruhusiwa kukifanya kwa sasa endapo atapata dhamana.
 
Kama amekamatwa tena hiyo press conference itafanyikia wapi, Central Police?
 
ameachiwa huru kwa tuhuma za uchochezi na akakamatwa tena kwa tuhuma za ugaidi. chanzo ni itv. mia
 
Mkuu, inashauriwa kuwa unapokua kesi Mahakamani sio vizuri kuizungumzia kwa maana utakuwa unampe mshitaki wako nafasi nzuri ya kujipanga ktk kuandaa nondo zaidi.
 
Hapa kuna kitu sijakieelewa vizuri, yawezekana labda kwa kuwa mimi siyo mtalaam wa sheria. Kwa taarifa tulizopata ni kuwa makosa yote 4 aliyoshitakiwa nayo yalikuwa yanahusu ugaidi. Sasa inakuwaje kaachiwa huru harafu kakamatwa tena kwa makosa ya ugaidi!!!!?. Au kuna makosa mengine zaidi ya ugaidi tofauti na ya mwanzo?.

Hapa kweli kazi ipo na ina maana walijua mapema kabisa kuwa kwa makosa waliyotoa mwanzoni lazima Lwakatare ataachiwa huru hivyo ikabidi wajiandae tena upya/ au wamemkamata harafu wakaendelee kumtafutia makosa mengine ambayo hayapo.
 
Bado mwisho wa MWEZI................jitahidi:bange:
 
Sasa swali,Je, iwapo ataachiwa kwa dhamana baada ya kukamatwa kwa mara ya pili ataruhusiwa kuongelea jambo hilo?Au ndio itakuwa kama kawaida kwamba kesi iko mahakamani na hivyo jambo hiliol haliwezi kujadiliwa popote pale au hata kulitolea taarifa yoyote ile?

Wataalamu wa sheria mtusaidie ni nini Lwakatare anachoweza kufanya na nini haruhusiwa kukifanya kwa sasa endapo atapata dhamana.

masuala yalioko mahakamani hairuhusiwi kujadiliwa nje ya mahakama kwa sababu tafsiri yake huwa unataka mhusika kutumia nguvu ya umma kuishinikiza mahakama kuyafanya yale uyatakayo!
 
Back
Top Bottom