Lwandamina jiheshimu, tukuheshimu usianze kwa kutusi watu

mwalukuni mchanyato

JF-Expert Member
Joined
May 15, 2013
Posts
404
Reaction score
230
Ndugu wana Jf.

Nimeona nianze kuwa na wasiwasi na huyu mgeni wetu klabuni yaani namaanisha kocha wetu Lwandamina kutokana na kauli yake kuwa wachezaji wa kibongo ni legelege.Hii kauli naiona kama inaukakasi au kama si hivyo inamaanisha ni tusi au kejeli kwa kizazi hiki cha soka la Tanzania.

Nijuavyo Mimi wachezaji wote ni ngangari kwa kuwa ni wanamichezo na wanafanya mazoezi kila siku.Hivyo ulegelege hamna.Yeye alitakiwa kusema wachezaji wa kibongo wanahitaji mazoezi ya ziada kuwajengea stamina, hususan katika timu yake ya Yanga kwani ndio timu inayomuhusu zaidi.Kutoa majumuisho ya wachezaji wote ni kukosa busara na weledi na kuwakosea heshima watanzania kwa muono wangu.

Angekuwa muungwana kwa kauli hii,inabidi awaombe radhi wachezaji wa Tanzania kwa hili. Amepewa Yanga aifundishe na sio timu ya taifa,hivyo tathmini ya ulegelege aitoe kwa yanga na si kwa wachezaji wa vilabu vyote Tanzania.

 
Hata cheza yeye amini huyu kocha achukui mda yanga,Mimi nina imani wachezaji wanampenda plujin sana Watamfanyia lwandamila kama Morinyo wa chelsea
 
Mkisemwa ukweli mnatoa mapovu na ndo maana Trump naye kawachana waafrika ...huo ni kweli kama hutaki we fungua kesi, mbona waliwahi kuhonywa waachane na mitindo ya nywele? si aliwachana kondic ama hukuwepo?

Kazi ni kujituma na kuwa focused vinginevyo utaitwa legelege na usianze kurusha ngumi
 
Hayupo sahihi kabisa.
 
wachezaj wa bongo ni legelege haina mjadala km sio hivyo nipe orodha ya wachezaj saba wanaocheza nje kuonesha mnajituma hadi kuwa professional players
 
Jifunze kutofautisha kati ya ukweli na tusi, mnapenda sana sifa za marehemu acha ujinga hii ilitaliwa iwe changamoto kwa wachezaji wa kibongo kukaza zaidi na zaidi, hebu angalia ranking za fifa au ni wachezaji wangapi wa bongo wanaocheza nje mpira wa kulipwa hivi unajua ni kwanini? pumbavu sana acha ujinga
 
Tatizo mkiambiwa ukweli povu linawatoka mnataka mreeembwe na misamiati ndio mumuone muungwana. huyu ni mkweli kama makocha wa ulaya haina kuremba
 
DONA na PIZZA wapi na wapi....Wenzetu wanakula vitu laini laini na mazoezi kwa wingi ndio maana hata wepesi uwanjani....
 
Kama Una taaluma ya ukocha na unaifundisha Yanga Una haki kabisa kum challenge kocha mpya Kama huna wewe ni debe tupu kamwe haliachi kutoa mlio
 
Sasa tusi liko wapi?legelege ndio maana mpira wetu haufiki popote,ngoja awakomaze uone mafaniko yake
 
Inaamaama hujui kama wachezaji wa TZ ni legelege?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…