M-PESA.TIGO PESA na MAHUSIANO...


Hii nayo gia, filled for future reference, thumbs up Smile.

 

na wengine zimewaponza
anatumiwa pesa hadi haamini...lol
siku ya pili mwenyewe anapeleka kitumbua lol
 
Kinga'sti sweetie
mimi simu yangu ni sasa tel
na benki yangu ni daresaalm community bank....
sijui nikutumie vipi honey ?lol

Mtumie kwa Western Union ha ha ha vigezo na masharti kuzingatiwa.

 
Hahahhahahahahhha!
Washukuriwe wagunduzi wa MPESA,TIGO PESA,
Maisha yangu sasa maisha yangu laaaaaaaaaaaaini!
Hata usiku wa manane salio likikata nabofya tu na kuendelea kuenjoy,
Wazee wangu kijijin hata nikipiga kidili cha elfu 10 na wapunguzia buku 5,
Dogo naye huko shule akibip nampunguzia jero yan raha km nn!
 
Binafsi sijawahi kutumia ila kwa ninavyosikia nadhani faida ni nyingi zaidi ya hasara kama zipo. Na kama hasara zipo nadhani zitakua za kujitakia zaidi maana hamna anaechunwa kwa lazima, mtu anatoa mwenyewe hata kama ananung'unika ndani kwa ndani.
 
binafsi sijawahi kutumia ila kwa ninavyosikia nadhani faida ni nyingi zaidi ya hasara kama zipo. Na kama hasara zipo nadhani zitakua za kujitakia zaidi maana hamna anaechunwa kwa lazima, mtu anatoa mwenyewe hata kama ananung'unika ndani kwa ndani.
achana na boss huyo.inaelekea ni bahili sana.ukiona mwanaume anapiga bajeti hadi nyumba ndogo hutomuweza.acha tuendelee na ma mpesa wetu yeye akibana wenzie wanaachia,and the life goes on? Register no yako mpesa au tigo pesa na uwe na urafiki na watu walio registered uinjoy maisha
 
Mmmmh, jamani mbona mie situmiwi hizi M-pesa
Sana ndo natuma tu

Ngoja niende maabara nikarekebishwe vitu fulani
Nikirudi hapa hadi wadada mnanitumia hela
 
Binafsi sijawahi kutumia ila kwa ninavyosikia nadhani faida ni nyingi zaidi ya hasara kama zipo. Na kama hasara zipo nadhani zitakua za kujitakia zaidi maana hamna anaechunwa kwa lazima, mtu anatoa mwenyewe hata kama ananung'unika ndani kwa ndani.

KILA KITU KINAPOAANZA KINAKUWA KWA FAIDA
hata simu ni kwa faida but still ndoa nyingi zimevunjika
au kuingia kwenye migogoro sababu ya simu
 
bora zifutwe tu, watu hatupumui sasahivi, imekuwa kero sana, hatuna pakukwepea aisee
 
bora zifutwe tu, watu hatupumui sasahivi, imekuwa kero sana, hatuna pakukwepea aisee

Yaani acha tu, hapa nilipo sasa hivi kuna mtu kanishtukiza eti nimtumie hela kapungukiwa na elfu 30 ya kusuka, namtafutia jibu la kimjibu hapa, wadada wanafikiri pesa hazina mipango mda wote, enzi hizo hakuna huu ujinga ilikuwa raha kweli, ngoja nimjibu mtandao haupatikani nazani wameblock my tigo pesa account
 

ha ha haa
we hamia sasa tel....lol
 
tena cku hizi mpaka kenya uganda na ulaya inakamata!!!duh!
 
KILA KITU KINAPOAANZA KINAKUWA KWA FAIDA
hata simu ni kwa faida but still ndoa nyingi zimevunjika
au kuingia kwenye migogoro sababu ya simu

Ndoa hazivunjiki kwa sababu ya simu, zinavunjika kwa watu kutumia vibaya simu. Huwezi ukamkuta mtu anaetumia simu yake ipasavyo anajikuta matatani kwajili ya simu.

Acheni kusingizia simu na hizo sijui MPESA. . .Kwani mtu anakulazimisha untumie mtu pesa?Kama una akili yako mwenyewe unafanyaje kitu ambacho hupendi tena bila ya kulazimishwa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…