Kiukweli duka la rejareja lina faida ndogo esp ukiwa na mtaji mdogo kama huo. Na linahitaji umakini wa hali ya juu. Bidhaa nyingi sina faida ndogo bila kutegemea mzunguko wake. mostly faida yake ni Tsh 200-500 kutegemea na bidhaa.
Lets say unanunua kilo 50 ya sukari unapata faida ya Tsh200-500 kwa kila kilo ukaweza kuchukua muda wa siku 15-30 kulingana na eneo uliopo. Hapo utagundua faida ya (200*50=10000 hadi 500*50=25000) hapo ukila hata 5000 tu hutajiongeza kimtaji kwa kuwa hilo kilo 50 ya sukari inachukua muda kidogo kutoka n mengi hutokea in between ukiwa na mkono wa kuchukua mtaji utakufa au utadumaa (kutokuwa mkubwa).
Sokila senti inayojizalisha ni muhimu kuiweka kimtaji either kwa kununua bidhaa nyingine ili mtaji ukue mfano lets say leo mauzo yamekuwa 25000 kwa bidhaa za mauzo. Nenda kanunua bidhaa zingine ambazo hakuna dukani kuliko kukaa na hiyo pesa mkononi kuila ni rahisi.
Niliwahi kufanya hii biashara bila research ya kutosha ikafa pamoja ya kuwa niliibiwa. Nakushauri ukitaka kwa mtaji huo weka tigopesa ndio ambayo inatoka zaidi mtaji wa angalau 500,000 na duka la mtaji wa angalau 500,000 utakuwa unajitegemea wenyewe esp ukiwa uswahili.
Uswahilini wengi hawa save pesa ni hand to mouth kwa hiyo kuja dukani ni lazima kwa vitu vidogo dogo kama mafuta ya chakula, ya taa, sabuni za unga, unga sembe, unga ngano, chumvi, mchele, sukari nk wakati huo huo unajiongeza kwa vingine kama mafuta ya kujipaka n mengine.
Ukiweka na hiyo tigopesa hapo hapo mtu anakuja kutoa hela kwako n kununua bidhaa hapo hapo. Na wengi itakuwa ni kutoa helq ndogo elfu 10-50 mzunguko wake ni mkubwa uswahilini.
Nasema uswahilini cz sioni kuwa na mtaji wa hela uliyosema kwa eneo la kishua.
Sent using
Jamii Forums mobile app