Kidagaa kimemwozea
JF-Expert Member
- Jul 13, 2018
- 3,680
- 6,554
Kuna wadau waliomba kujua toafuti ya M-wekeza, ipi bora , n.k
Nitaeleza kwa ufupi kwa wale wanaohitaji kupata hivyo visenti basi wanufaike.
UMILIKI
UTT AIMS nishirika la umma
M-wekeza ni mradi wa Vodacom na Sanlam ambayo ni mashirika ya kibinafsi
FAIDA NA HASARA
Faida ya M-wekeza ni hadi 13.% kwa mwaka japo kuna kipindi (siku) inaweza kiwa 12% kutegemeana na soko
Mfuko wa bond UTT una wastani wa faida ya 12% kwa mwaka na hutoa gawio kila mwisho wa mwezi . Compaund interest ya gawio hakuna.
Mfuko wa ukwasi unatoa faida 12% na inaweza kuzidi hapo lakini M-wekeza haizidi 13%
M-wekeza haina compound interest kwakuwa faida huwekwa kwenye mtaji tarehe 2-5 ya mwezi unaofuata. Lakini mfuko wa ukwasi na Bond faida huwekwa kila siku hivyo faida nayo inatengeneza faida.
Masuala ya usalama
Yote ni mifuko salama kwa kuwa inaendeshwa kwa mujibu wa sheria. Labda nchi isambaratike ndio sijui nini kitatokea.
Usalama wa kibinafsi wewe mwenyewe.
Kwakuwa M-wekeza unaweza kutoa pesa muda wowote , ikiwa mtu ana namba yako ya siri anaweza kukuibia. Na pia wale wazee wa kubeti unaweza kushawishika kuchomoa huko unaleta kwa muhindi anakupiga , mara umenunua vocha. Kwahiyo hapa inahitaji nidhamu ya hali ya juu.
Mifuko ya UTT ukitaka kutoa pesa huchukua siku 2-5 za kazi kutegemea na mfuko hivyo sio rahisi fedha kutolewa hovyo
Mwisho. Biashara nibora zaidi
Nitaeleza kwa ufupi kwa wale wanaohitaji kupata hivyo visenti basi wanufaike.
UMILIKI
UTT AIMS nishirika la umma
M-wekeza ni mradi wa Vodacom na Sanlam ambayo ni mashirika ya kibinafsi
FAIDA NA HASARA
Faida ya M-wekeza ni hadi 13.% kwa mwaka japo kuna kipindi (siku) inaweza kiwa 12% kutegemeana na soko
Mfuko wa bond UTT una wastani wa faida ya 12% kwa mwaka na hutoa gawio kila mwisho wa mwezi . Compaund interest ya gawio hakuna.
Mfuko wa ukwasi unatoa faida 12% na inaweza kuzidi hapo lakini M-wekeza haizidi 13%
M-wekeza haina compound interest kwakuwa faida huwekwa kwenye mtaji tarehe 2-5 ya mwezi unaofuata. Lakini mfuko wa ukwasi na Bond faida huwekwa kila siku hivyo faida nayo inatengeneza faida.
Masuala ya usalama
Yote ni mifuko salama kwa kuwa inaendeshwa kwa mujibu wa sheria. Labda nchi isambaratike ndio sijui nini kitatokea.
Usalama wa kibinafsi wewe mwenyewe.
Kwakuwa M-wekeza unaweza kutoa pesa muda wowote , ikiwa mtu ana namba yako ya siri anaweza kukuibia. Na pia wale wazee wa kubeti unaweza kushawishika kuchomoa huko unaleta kwa muhindi anakupiga , mara umenunua vocha. Kwahiyo hapa inahitaji nidhamu ya hali ya juu.
Mifuko ya UTT ukitaka kutoa pesa huchukua siku 2-5 za kazi kutegemea na mfuko hivyo sio rahisi fedha kutolewa hovyo
Mwisho. Biashara nibora zaidi