SoC02 Maabara za Sayansi ni muhimu katika shule za msingi ili kumjenga mtoto katika masomo ya Sayansi

SoC02 Maabara za Sayansi ni muhimu katika shule za msingi ili kumjenga mtoto katika masomo ya Sayansi

Stories of Change - 2022 Competition

HIBISCUS 80

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2020
Posts
1,058
Reaction score
1,218
Habari za kazi wanajamvi,

Leo hii nimeona niandike kuhusiana na umuhimu wa kuwepo kwa MAABARA za kufanyia majaribio mbalimbali katika Somo la sayansi kwa shule za msingi hapa nchini kwetu Tanzania.

Sayansi ni Somo ambalo mwanafunzi anatakiwa kujifunza kwa vitendo zaidi kuliko kwa maelezo (theory)
MAABARA ni chumba maalumu kimetengwa katika shule kwa ajili ya majaribio ya kisayansi.

Katika shule za secondari sayansi imegawanyika katika sehemu tatu nazo ni Physics, chemistry na Biology
Shule za msingi wanafunzi Wana Somo la sayansi ambalo ndani yake limebeba masomo hayo matatu yaani Physics,chemistry na Biology.

Katika shule za msingi hakuna kabisa MAABARA ili kuruhusu watoto wetu kufanya majaribio mbalimbali ya kisayansi.

Lakini kama kweli tunataka Kumjenga mtoto awe mahiri katika masomo haya basi majaribio hayo ya kisayansi yanatakiwa yaanzie shule za msingi .

Katika level ya shule ya msingi wanafunzi wanasoma topics mbalimbali ambazo zinahutaji majaribio badala ya kusoma kwa kumsikiliza mwalimu tu.Wanafunzi wanatakiwa kufanya zaidi wao wenyewe. kusoma kwa vitendo kunasaidia sana katika kumkuza mtoto katika mambo yafuatayo
1. CURIOSITY(UDADISI)
2. CREATIVITY(UBUNIFU)
3. CRITICAL THINKING

Kabla sijaelezea ni majaribio Gani wanafunzi wa shule za msingi wanapaswa kuyafanya katika masomo Yao ya sayansi ningependa kuelezea kwa kifupi kuhusu wanasayansi mashuhuri ambao waligundua mambo mbali mbali katika hii Dunia

Ukisoma historia za wanasayansi hao utagundua kuwa hakuna mwanasayansi ambae alilala usingizi akaamka na kugundua jambo Fulani

Au waliota ndoto ya ugunduzi , au walisoma kwa kumsikiliza tu mwalimu ndani ya chumba chenye pembe nne (darasa) na mara wakagundua jambo

Wanasayansi wote walitumia muda wao wote kujifunza kwa vitendo Tena kwa miaka kadhaa na kurudia experiments nyingi sana mpaka wakaweza kugundua mambo mbalimbali

Nitawataja wanasayansi kadhaa ambao walitumia muda wao mwingi kujifunza kwa vitendo na kwa kutumia idea za watu wengine waliotangulia wakaweza kugundua mambo mbalimbali

Archemedes - alitumia zaidi ya nusu ya miaka yake kujifunza na kufanya majaribio mbalimbali , ukisoma historia yake aligundua bouyancy force(upthrust), calculus, law of lever, odometer , pi (ambayo inatumika kutafuta area ya circles) nk

Galileo Galilei - aligundua simple pendulum, telescope,parabola, acceleration due to gravity nk, Galileo alitengeza telescope baada ya kujifunza kwa miaka mingi sana Tena kwa vitendo kuhusiana na lenses na hata alipotengeneza telescope alitumia kwa miezi kadhaa Kila siku kuangalia angani na akagundua kuwa Dunia na sayari nyingine zinalizunguka jua, hata alipofungwa kwa muda wa miaka Tisa aliendelea kufanya majaribio mbalimbali na kuchapisha maandiko yake

Sir Isaac Newton - universal law of gravitation and Newton"s laws of motion. Mchango wake umeleta mabadiliko makubwa katika ulimwengu wa sayansi. Alitumia muda wake mwingi kujifunza nje ya darasa na kufanya majaribio mengi .historia inasema apple lilianguka juu ya kichwa chake ikapelekea UDADISI kwa nini apple lianguke chini na lisiende juu

Pythogoras - huyu alizaliwa ugiriki lakini alikwenda Misri na akaishi huko kwa miaka zaidi ya 20 kwa ajili ya kujifunza Alikuja na kanuni ya pythogoras

Wako wengine wengi kama Bohr,Robert Hooke, Rutherford, Dalton,Faraday ,Eistein nk. Wapo wanasayansi walioishi Miaka ya karibuni pia katika Karne ya 19 na 20 na wakagundua mambo mbalimbali, lakini hii yote inatokana na kujifunza zaidi nje ya darasa kwa kufanya majaribio mengi zaidi


Sasa nikirudi kwenye mada yangu hapo juu

Sayansi katika nchi yetu inafundishwa kama hadithi ya abunuwasi zaidi

Huwezi kusimamia darasani ukaanza kufundisha sayansi kama story au kwa kutumia picha za kuchora na picha za vitabuni

Hii inapelekea wanafunzi wengi kuona Somo hili kama SoMo gumu sana.

Jambo hili linatufanya pia kukosa wataalam wa kutosha katika sekta mbalimbali kama ujenzi, afya, maji, nk
Ndii maana utasikia watu wakisema hatuna ma engineer katika nchi yetu.

Kwa nchi za wenzetu watoto wadogo kabisa wa chekechea wanaanza kujifunza sayansi kulingana na level zao.
Kwa madarasa ya shule ya msingi Wana topics nyingi sana ambazo wanaweza kujifunza kwa vitendo na hata mazingira yanaruhusu

Walimu waache kuandika notes nyingiiiii badala yake wawape watoto nafasi ya kujifunza kwa vitendo na kuwapa nafasi wanafunzi kutengeneza baadhi ya zana za kujifunzia badala ya kutumia manila Kila siku kuchora chora picha kwenye manila card

Mfano wa topics ambazo zitahitaji wanafunzi wa shule ya msingi kuingia MAABARA na kufanya majaribio na kutumia sayansi models kujifunza

Photosynthesis, archemedes principle, respiration,force,excretion, structure of leaves, digestion , reproduction in plants and animals,motion,acceleration,magnetism, electricity simple machines, ecosystem renewable energy,diffusion and osmosis,blood circulatory system,first aid,light energy,transfer of heat,temperature, aina za moto na jinsi ya kuzima, nervous system, types of food,acid and base nk

Hizo ni baadhi ya topics za shule ya msingi za sayansi katika shule zetu za Tanzania

Kwa kweli masomo ya sayansi hayana topic au sub topic ambayo mwalimu anatakiwa kueleza kwa mdomo
Kila topic na Kila sub topic inahitaji majaribio. Na hiyo ndio sayansi

Kuna models nyingi sana ambazo zinaweza kununuliwa na kuwekwa katika MAABARA hizo na wanafunzi wakaweza kutumia kujifunza kwa kuona

Pia baadhi ya topics wanafunzi wakatoka nje ya darasa na nje ya maabara na kujifunza kwani Kuna miti, mimea ,wadudu nk ambavyo viko nje wanafunzi wakajifunza.

Mwanafunzi anakimbia physics anasema physics ngumu halafu anaenda veta kusomea fundi umeme wakati anachokwenda kujifunza veta amekikimbia darasani

Lakini ni kwa sababu huko anakokwenda anajifunza kwa vitendo mwanzo mwisho

Lakini umeme anaojifunza veta unaanzia kwenye sayansi darasa la Tano na kuendelea ,pia anaukuta umeme Tena form two na form three na form four

Kujifunza sayansi ni gharama lakini hakuna jinsi ya kuepuka gharama hii kama tunataka kutengeneza wanasayansi mahiri

Kwa niaba ya Maarifa Time napenda kutumia picha zao nilizozikuta mtandaoni walitumia models kufundisha sayansi

Kuna model ya male reproductive system, Kuna model ya ecosystem nk

Models zingine hapo zimetengenezwa na walimu

Lakini sisemi walimu watengeneze models

Ila siku hizi models zinauzwa na zinapatikana

Kinachohitajika ni shule kununua na kuziweka maabara

Tuwafundishe watoto kuelewa na sio kukariri

Asanteni sana
Nawasilisha


Picha kwa hisani ya Maarifa- Time


IMG_20220814_110734_2.jpg
IMG_20220806_125220_488.jpg
IMG_20220806_093013_988.jpg
IMG_20220806_093013_008.jpg
IMG_20220810_140223_093.jpg
 
Upvote 5
Miaka ile niliyosoma..
Ni mpaka tulivyo fika form 4 ndio nikaiona maabara amboyo ilikuwa choka mbaya..
Humo humo ndio Physics, Biology na Chemistry...
Na kwenye physics tulifanya practical moja tu mwaka wote wa form 4 ya pendulum, na ndio nikakutata na formula ya
1660682864895.png
, ambayo nilitumia na kweli niliweza kupata acceleration due to gravity kwa jibu la 9.776m.s approx to 9.8m/s, ndio maana mpaka leo sisahau hii expirement...

Kwenye Chemisty form 4 , Mwl Mushi alitupeleka na kutuonyesha hii ni bunsen burner na hii ni beaker na kadhalika, kwisha mchezo, hakuna hata chemical reaction experiment yeyeto iliyofanyika, muda wote alitumia kutusimulia nembo ya pyrex iliyokuwa kwenye beaker inamaanisha nini...

Hakuna experiment yeyeto iliyowahi kufanyika ya Biology.....
 
Miaka ile niliyosoma..
Ni mpaka tulivyo fika form 4 ndio nikaiona maabara amboyo ilikuwa choka mbaya..
Humo humo ndio Physics, Biology na Chemistry...
Na kwenye physics tulifanya practical moja tu mwaka wote wa form 4 ya pendulum, na ndio nikakutata na formula ya View attachment 2325792, ambayo nilitumia na kweli niliweza kupata acceleration due to gravity kwa jibu la 9.776m.s approx to 9.8m/s, ndio maana mpaka leo sisahau hii expirement...

Kwenye Chemisty form 4 , Mwl Mushi alitupeleka na kutuonyesha hii ni bunsen burner na hii ni beaker na kadhalika, kwisha mchezo, hakuna hata chemical reaction experiment yeyeto iliyofanyika, muda wote alitumia kutusimulia nembo ya pyrex iliyokuwa kwenye beaker inamaanisha nini...

Hakuna experiment yeyeto iliyowahi kufanyika ya Biology.....
Hahahaha
Ni kweli unachoongea
Sasa fikiria kwa namna hyo uliyosoma
Kweli unawwza kuwa mwanasayansi mahiri?.Serikali unapaswa kuliangalia hili kwa mapana zaidi
 
Toa pesa upate vtu vizuri shule za msingi zenye maabara na maktaba nzuri za kusomea zipo tena kibao
Ila ukitaka serikal ikuwekee ivyo vtu shule za umma utakua unaionea sabu tunapenda vya bure
Tufanye kazi tuchangie pato la taifa na pato la taifa likiongezeka serikal itaweka facility zote izo mashuleni

Tunakoseaga sana kutoa ushauri bila ya tuonesha ni wapi tutapata pesa ya kufanya vtu ivyo. Toa ushauri au maoni lakn pia toa mbinu ni jinsi gan tunaweza vipata au kufanya vtu ivyo ulivyo shauri
 
Toa pesa upate vtu vizuri shule za msingi zenye maabara na maktaba nzuri za kusomea zipo tena kibao
Ila ukitaka serikal ikuwekee ivyo vtu shule za umma utakua unaionea sabu tunapenda vya bure
Tufanye kazi tuchangie pato la taifa na pato la taifa likiongezeka serikal itaweka facility zote izo mashuleni

Tunakoseaga sana kutoa ushauri bila ya tuonesha ni wapi tutapata pesa ya kufanya vtu ivyo. Toa ushauri au maoni lakn pia toa mbinu ni jinsi gan tunaweza vipata au kufanya vtu ivyo ulivyo shauri
Kama Kuna shule za msingi zenye maabara za sayansi Tanzania haziwezi kufika hata kumi
Kwa hyo unaposema zipo kibao Hilo si la kweli hata kidogo .pia issue ya elimu ni issue ya Serikali na ni lazima Serikali ishughulikie shule zake
Itoe pesa kwa ajili ya kuendeleza shule .sii mini niishauri Serikali ikachukue wapi pesa .
Ili tuweze kupata wataalamu wetu makini na mahiri lazima gharama itumike katika kuwekeza kwenye elimu.elimu na afya ni mambo ya kwanza kabisa Serikali inatakiwa kuyaangalia kama kweli tunataka kuendelea kama nchi
 
Habari za kazi wanajamvi,

Leo hii nimeona niandike kuhusiana na umuhimu wa kuwepo kwa MAABARA za kufanyia majaribio mbalimbali katika Somo la sayansi kwa shule za msingi hapa nchini kwetu Tanzania.

Sayansi ni Somo ambalo mwanafunzi anatakiwa kujifunza kwa vitendo zaidi kuliko kwa maelezo (theory)
MAABARA ni chumba maalumu kimetengwa katika shule kwa ajili ya majaribio ya kisayansi.

Katika shule za secondari sayansi imegawanyika katika sehemu tatu nazo ni Physics, chemistry na Biology
Shule za msingi wanafunzi Wana Somo la sayansi ambalo ndani yake limebeba masomo hayo matatu yaani Physics,chemistry na Biology.

Katika shule za msingi hakuna kabisa MAABARA ili kuruhusu watoto wetu kufanya majaribio mbalimbali ya kisayansi.

Lakini kama kweli tunataka Kumjenga mtoto awe mahiri katika masomo haya basi majaribio hayo ya kisayansi yanatakiwa yaanzie shule za msingi .

Katika level ya shule ya msingi wanafunzi wanasoma topics mbalimbali ambazo zinahutaji majaribio badala ya kusoma kwa kumsikiliza mwalimu tu.Wanafunzi wanatakiwa kufanya zaidi wao wenyewe. kusoma kwa vitendo kunasaidia sana katika kumkuza mtoto katika mambo yafuatayo
1. CURIOSITY(UDADISI)
2. CREATIVITY(UBUNIFU)
3. CRITICAL THINKING

Kabla sijaelezea ni majaribio Gani wanafunzi wa shule za msingi wanapaswa kuyafanya katika masomo Yao ya sayansi ningependa kuelezea kwa kifupi kuhusu wanasayansi mashuhuri ambao waligundua mambo mbali mbali katika hii Dunia

Ukisoma historia za wanasayansi hao utagundua kuwa hakuna mwanasayansi ambae alilala usingizi akaamka na kugundua jambo Fulani

Au waliota ndoto ya ugunduzi , au walisoma kwa kumsikiliza tu mwalimu ndani ya chumba chenye pembe nne (darasa) na mara wakagundua jambo

Wanasayansi wote walitumia muda wao wote kujifunza kwa vitendo Tena kwa miaka kadhaa na kurudia experiments nyingi sana mpaka wakaweza kugundua mambo mbalimbali

Nitawataja wanasayansi kadhaa ambao walitumia muda wao mwingi kujifunza kwa vitendo na kwa kutumia idea za watu wengine waliotangulia wakaweza kugundua mambo mbalimbali

Archemedes - alitumia zaidi ya nusu ya miaka yake kujifunza na kufanya majaribio mbalimbali , ukisoma historia yake aligundua bouyancy force(upthrust), calculus, law of lever, odometer , pi (ambayo inatumika kutafuta area ya circles) nk

Galileo Galilei - aligundua simple pendulum, telescope,parabola, acceleration due to gravity nk, Galileo alitengeza telescope baada ya kujifunza kwa miaka mingi sana Tena kwa vitendo kuhusiana na lenses na hata alipotengeneza telescope alitumia kwa miezi kadhaa Kila siku kuangalia angani na akagundua kuwa Dunia na sayari nyingine zinalizunguka jua, hata alipofungwa kwa muda wa miaka Tisa aliendelea kufanya majaribio mbalimbali na kuchapisha maandiko yake

Sir Isaac Newton - universal law of gravitation and Newton"s laws of motion. Mchango wake umeleta mabadiliko makubwa katika ulimwengu wa sayansi. Alitumia muda wake mwingi kujifunza nje ya darasa na kufanya majaribio mengi .historia inasema apple lilianguka juu ya kichwa chake ikapelekea UDADISI kwa nini apple lianguke chini na lisiende juu

Pythogoras - huyu alizaliwa ugiriki lakini alikwenda Misri na akaishi huko kwa miaka zaidi ya 20 kwa ajili ya kujifunza Alikuja na kanuni ya pythogoras

Wako wengine wengi kama Bohr,Robert Hooke, Rutherford, Dalton,Faraday ,Eistein nk. Wapo wanasayansi walioishi Miaka ya karibuni pia katika Karne ya 19 na 20 na wakagundua mambo mbalimbali, lakini hii yote inatokana na kujifunza zaidi nje ya darasa kwa kufanya majaribio mengi zaidi


Sasa nikirudi kwenye mada yangu hapo juu

Sayansi katika nchi yetu inafundishwa kama hadithi ya abunuwasi zaidi

Huwezi kusimamia darasani ukaanza kufundisha sayansi kama story au kwa kutumia picha za kuchora na picha za vitabuni

Hii inapelekea wanafunzi wengi kuona Somo hili kama SoMo gumu sana.

Jambo hili linatufanya pia kukosa wataalam wa kutosha katika sekta mbalimbali kama ujenzi, afya, maji, nk
Ndii maana utasikia watu wakisema hatuna ma engineer katika nchi yetu.

Kwa nchi za wenzetu watoto wadogo kabisa wa chekechea wanaanza kujifunza sayansi kulingana na level zao.
Kwa madarasa ya shule ya msingi Wana topics nyingi sana ambazo wanaweza kujifunza kwa vitendo na hata mazingira yanaruhusu

Walimu waache kuandika notes nyingiiiii badala yake wawape watoto nafasi ya kujifunza kwa vitendo na kuwapa nafasi wanafunzi kutengeneza baadhi ya zana za kujifunzia badala ya kutumia manila Kila siku kuchora chora picha kwenye manila card

Mfano wa topics ambazo zitahitaji wanafunzi wa shule ya msingi kuingia MAABARA na kufanya majaribio na kutumia sayansi models kujifunza

Photosynthesis, archemedes principle, respiration,force,excretion, structure of leaves, digestion , reproduction in plants and animals,motion,acceleration,magnetism, electricity simple machines, ecosystem renewable energy,diffusion and osmosis,blood circulatory system,first aid,light energy,transfer of heat,temperature, aina za moto na jinsi ya kuzima, nervous system, types of food,acid and base nk

Hizo ni baadhi ya topics za shule ya msingi za sayansi katika shule zetu za Tanzania

Kwa kweli masomo ya sayansi hayana topic au sub topic ambayo mwalimu anatakiwa kueleza kwa mdomo
Kila topic na Kila sub topic inahitaji majaribio. Na hiyo ndio sayansi

Kuna models nyingi sana ambazo zinaweza kununuliwa na kuwekwa katika MAABARA hizo na wanafunzi wakaweza kutumia kujifunza kwa kuona

Pia baadhi ya topics wanafunzi wakatoka nje ya darasa na nje ya maabara na kujifunza kwani Kuna miti, mimea ,wadudu nk ambavyo viko nje wanafunzi wakajifunza.

Mwanafunzi anakimbia physics anasema physics ngumu halafu anaenda veta kusomea fundi umeme wakati anachokwenda kujifunza veta amekikimbia darasani

Lakini ni kwa sababu huko anakokwenda anajifunza kwa vitendo mwanzo mwisho

Lakini umeme anaojifunza veta unaanzia kwenye sayansi darasa la Tano na kuendelea ,pia anaukuta umeme Tena form two na form three na form four

Kujifunza sayansi ni gharama lakini hakuna jinsi ya kuepuka gharama hii kama tunataka kutengeneza wanasayansi mahiri

Kwa niaba ya Maarifa Time napenda kutumia picha zao nilizozikuta mtandaoni walitumia models kufundisha sayansi

Kuna model ya male reproductive system, Kuna model ya ecosystem nk

Models zingine hapo zimetengenezwa na walimu

Lakini sisemi walimu watengeneze models

Ila siku hizi models zinauzwa na zinapatikana

Kinachohitajika ni shule kununua na kuziweka maabara

Tuwafundishe watoto kuelewa na sio kukariri

Asanteni sana
Nawasilisha


Picha kwa hisani ya Maarifa- Time


View attachment 2325658View attachment 2325660View attachment 2325662View attachment 2325663View attachment 2325664
Sayansi gani na wewe wakati kila kitu mna-import?
 
Toa pesa upate vtu vizuri shule za msingi zenye maabara na maktaba nzuri za kusomea zipo tena kibao
Ila ukitaka serikal ikuwekee ivyo vtu shule za umma utakua unaionea sabu tunapenda vya bure
Tufanye kazi tuchangie pato la taifa na pato la taifa likiongezeka serikal itaweka facility zote izo mashuleni

Tunakoseaga sana kutoa ushauri bila ya tuonesha ni wapi tutapata pesa ya kufanya vtu ivyo. Toa ushauri au maoni lakn pia toa mbinu ni jinsi gan tunaweza vipata au kufanya vtu ivyo ulivyo shauri
Mtoa mada ameleta wazo zuri na pia wewe umeonesha nia njema ya kufanya ili litekelezwe.

Ni vigumu kwa Serikali kuu kuandaa miundombinu ya shule katika kila idara, nadhani sisi wananchi kupitia jumuiya zetu tunaweza kuisaidia Serikali katika namna mbalimbali kulingana na mazingira.

Tukifanikiwa katika hili vijana wataweza kufanya vizuri katika masomo yao na pia tutapata wataalamu waliobobea zaidi. Ni suala la jamii yetu kupenda maendeleo ya elimu zaidi.
 
Na kwenye physics tulifanya practical moja tu mwaka wote wa form 4 ya pendulum, na ndio nikakutata na formula ya
1660682864895.png
, ambayo nilitumia na kweli niliweza kupata acceleration due to gravity kwa jibu la 9.776m.s approx to 9.8m/s, ndio maana mpaka leo sisahau hii expirement...
Je imechangia chochote katika kupiga hatua kwenye maisha yako?
Nashauri sambamba na haya yote watoto wawe wanachunguzwa in advance interests zao ni nini, na huko ndiko waelekezwe badala ya kuwashitukiza form 3 kuwa chagua science au arts au biashara
 
Toa pesa upate vtu vizuri shule za msingi zenye maabara na maktaba nzuri za kusomea zipo tena kibao
Ila ukitaka serikal ikuwekee ivyo vtu shule za umma utakua unaionea sabu tunapenda vya bure
Tufanye kazi tuchangie pato la taifa na pato la taifa likiongezeka serikal itaweka facility zote izo mashuleni

Tunakoseaga sana kutoa ushauri bila ya tuonesha ni wapi tutapata pesa ya kufanya vtu ivyo. Toa ushauri au maoni lakn pia toa mbinu ni jinsi gan tunaweza vipata au kufanya vtu ivyo ulivyo shauri
Kwani hela inayotoka kutengeneza miundombinu inatoka wap? Hata wananchi wafanye kazi kama punda mchana kutwa serikali itatoa budget kulingana na matakwa yaliyopo, na ukute fikra kama yako ndo inafanya wasieke budget za kutosha kwenye mambo mengi ya muhimu. hiyo ni suggestion inatolewa serikali izingatie Kwani tulikua tunajua kwamba tunaeza jenga barabara za mwendokasi? AirPort ya kifahari? Standard gauge? Hata kama serikali imeombea mkopo kitu wanafanya ni kuwekeza for the future the same way wanatakiwa kufanya kwenye Elimu.
 
Kwani hela inayotoka kutengeneza miundombinu inatoka wap? Hata wananchi wafanye kazi kama punda mchana kutwa serikali itatoa budget kulingana na matakwa yaliyopo, na ukute fikra kama yako ndo inafanya wasieke budget za kutosha kwenye mambo mengi ya muhimu. hiyo ni suggestion inatolewa serikali izingatie Kwani tulikua tunajua kwamba tunaeza jenga barabara za mwendokasi? AirPort ya kifahari? Standard gauge? Hata kama serikali imeombea mkopo kitu wanafanya ni kuwekeza for the future the same way wanatakiwa kufanya kwenye Elimu.
Fanya kazi Kama punda wewe. Cha blah blah
 
Mtoa mada ameleta wazo zuri na pia wewe umeonesha nia njema ya kufanya ili litekelezwe.

Ni vigumu kwa Serikali kuu kuandaa miundombinu ya shule katika kila idara, nadhani sisi wananchi kupitia jumuiya zetu tunaweza kuisaidia Serikali katika namna mbalimbali kulingana na mazingira.

Tukifanikiwa katika hili vijana wataweza kufanya vizuri katika masomo yao na pia tutapata wataalamu waliobobea zaidi. Ni suala la jamii yetu kupenda maendeleo ya elimu zaidi.
Wazo zuri
 
Kwani hela inayotoka kutengeneza miundombinu inatoka wap? Hata wananchi wafanye kazi kama punda mchana kutwa serikali itatoa budget kulingana na matakwa yaliyopo, na ukute fikra kama yako ndo inafanya wasieke budget za kutosha kwenye mambo mengi ya muhimu. hiyo ni suggestion inatolewa serikali izingatie Kwani tulikua tunajua kwamba tunaeza jenga barabara za mwendokasi? AirPort ya kifahari? Standard gauge? Hata kama serikali imeombea mkopo kitu wanafanya ni kuwekeza for the future the same way wanatakiwa kufanya kwenye Elimu.
Kweli kabisa
 
Back
Top Bottom