Maadhimisho ya 56 ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara

Maadhimisho ya 56 ya siku ya Uhuru wa Tanzania Bara

KYANYINIMARAIGA

Senior Member
Joined
Oct 21, 2016
Posts
192
Reaction score
126
Kwanza kabisa nitanguize pongezi kwa Watanzania kwa kuadhimisha miaka 56 ya Uhuru.Ni jambo la kujivunia kwa Watanzania ,kwani katika kipini hiki nchi yetu imekuwa na amani,ushirikiano na maendeleo ya kila aina.Mwenyezi Mungu tunakuomba uwape afya waasisi wa Taifa hili na uwarehemu wale waliotangulia mbele ya haki.Tunakuomba uwajalie uadilifu,weledi na afya viongozi na wanachi wote tuzidi kulinda uhuru wetu na amani.
Pili nawaomba wale wote waliobahatika kuuona utawala wa kikoloni na pia kushuhudia "Union Jack" ikishushwa tupeane salamu na pia maneno machache ya kukumbukwa katika matukio hayo mawili(utawala wa kikoloni na adha zake na siku ya uhuru na furaha zake).Hii ni kwa faida ya kizazi ambacho hakikubahatika kuona matukio hayo..
 
Kwanza kabisa nitanguize pongezi kwa Watanzania kwa kuadhimisha miaka 56 ya Uhuru.Ni jambo la kujivunia kwa Watanzania ,kwani katika kipini hiki nchi yetu imekuwa na amani,ushirikiano na maendeleo ya kila aina.Mwenyezi Mungu tunakuomba uwape afya waasisi wa Taifa hili na uwarehemu wale waliotangulia mbele ya haki.Tunakuomba uwajalie uadilifu,weledi na afya viongozi na wanachi wote tuzidi kulinda uhuru wetu na amani.
Pili nawaomba wale wote waliobahatika kuuona utawala wa kikoloni na pia kushuhudia "Union Jack" ikishushwa tupeane salamu na pia maneno machache ya kukumbukwa katika matukio hayo mawili(utawala wa kikoloni na adha zake na siku ya uhuru na furaha zake).Hii ni kwa faida ya kizazi ambacho hakikubahatika kuona matukio hayo..
Mkoloni alikuwa na ubaya gani?
 
Kwani tanzania bara ilotawaliwa na nani?
Tanganyika ndiyo iliyotawaliwa na wakoloni.Baada ya kupata Uhuru tuliungana na Zanzibar .usahihi ni Uhuru wa Tanganyika 9.12.1961.baada ya Muungano hakuna nchi inaitwa Tanganyika ila kuna Tanzania.
 
Shukurani kwako kuleta uzi huu. Hata hivyo kwa faida ya vizazi vyetu, hakukuwa na uhuru wa Tanzania bara. Watendee haki wazee wetu waliojitoa kuhangaika kwa ajili yetu na vizazi vyetu. Wao walipigania Tanganyika na siyo Tanzania
 
Mkoloni alikuwa na ubaya gani?
Pamoja na mambo mengine mazuri aliyokuwa nayo lakini ubaya ulizidi nahasa:

Mkoloni alimunyima huru wa kujitawala na kuamua mambo yake Mwananchi.
Mkoloni alidhalilisha wananchi katika ardhi yao
mkoloni aliendesha uchumi wa nchi kwa maslahi yake
Mkoloni alikuwa mbaguzi( hebu tazama mfumo wa makazzi katika miji yetu yote utakuta sehemu inaitwa "uzunguni" ,angalia mfumo wa elimu kwa wakati uleangalia mfumo wa hospitali kwa wakati ule,angalia mfumo wa maaraja ya usafiri kwenye vyombo vya usafiri.angalia mahoteli .angalia viwanja vya michezo nk
(na wewe sasa onyesha uzuri wake)
 
Tunaposema Tanzania Bars sijui wenzetu wa Mafia na Ukerewe wanajisikiaje??


RIP Rev. Mtikila
 
[emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji7]
 
Ni jambo Jema kabisa. Pamoja nakuwa na matatizo ya hapa na pale katika nch hii bt bado tuko pamoja, Mungu ni mwemaa
 
Kumbukumbu zangu hazinikumbushi kuna nchi inaitwa Tanzania Bara iliwahi kupata Uhuru!!!
Yaani mpaka inasikitisha kwanini wasiseme uhuru wa tanganyika,hivi ukisema tanganyka ni dhambi?
 
Yaani mpaka inasikitisha kwanini wasiseme uhuru wa tanganyika,hivi ukisema tanganyka ni dhambi?
Down Memory Lane(TSN ARCHIVES)
"leading Tanganyika nationalist Mwalimu Julius Nyerere displays a placard(complete Independence 1961) that pronounces the country's envisaged full political independence in 1961,.He subsequently became pioneer President first of Tanganyika and subsequently Tanzania."
 
Tanganyika na baada ya muungano ikaitwa Tanzania

Lakini kwa ufahamu wangu Tanzania ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Sasa utasemaje ilitwa Tanganyika haikubadilisha jina, muungano ndo ulitoa jina la Tanzania. Hebu tusaidiane kuwekana sawa hapo.
 
Back
Top Bottom