Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,147
- 2,008
Siku ya Afya ya Akili Duniani ni Siku ya Kimataifa maalumu kwa kutoa Elimu ya masuala ya Afya ya Akili, Uhamasishaji na Utetezi dhidi ya Unyanyapaa wa Kijamii pamoja na athari zake kwa wale walioathirika na Walezi wao
Shirika la Afya Duniani (WHO) linataja kuwa kabla ya janga la COVID19, takriban mtu 1 Kati ya 8 Duniani kote walikumbwa na matatizo ya kiakili, hata hivyo Msaada sahihi wa miundombinu na kiuchumi kwa ajili yao, ulikosekana
Matatizo ya afya ya akili yapo katika maisha yetu, familia, sehemu za kazi na jamii, na kuathiri kila mtu.
Dalili za matatizo ya akili ni pamoja na:
•Kuwa na hasira kupindukia
•Kukosa furaha katika maisha
•Kuwa na wasiwasi wa kupindukia
•Kukosa usingizi
•Kuwa na msongo mkali wa mawazo
Ni lazima tufanye kadiri tuwezavyo kuzuia magonjwa ya akili - kama watu binafsi na kama jamii
Ni muhimu kuendelea kutoa wito kwa serikali za kitaifa na za mitaa kuweka kipaumbele katika kupunguza mambo yanayojulikana kuwa hatari kwa afya ya akili ya watu Kama Ugumu wa Maisha, Migogoro ya Kijamii na Kimapenzi, Unyanyapaa wa Watu wenye Mahitaji Maalum pamoja na dhana au Mila potofu katika jamii
Pia kuimarisha wale wote wanashughulika na kulinda afya za akili kuanzia mtu Mmoja Mmoja hadi mashirika binafsi na kuunda nyenzo zinazohitajika kwa watu kustawi
Siku ya Afya ya Akili Duniani pia ni nafasi ya kuzungumza kuhusu afya ya akili kwa ujumla, jinsi tunavyohitaji kuitunza, na jinsi ilivyo muhimu kuzungumza kuhusu tunavyojisikia na kupata usaidizi ikiwa unatatizika
CHANZO: WHO, Mental Health Foundation
Shirika la Afya Duniani (WHO) linataja kuwa kabla ya janga la COVID19, takriban mtu 1 Kati ya 8 Duniani kote walikumbwa na matatizo ya kiakili, hata hivyo Msaada sahihi wa miundombinu na kiuchumi kwa ajili yao, ulikosekana
Matatizo ya afya ya akili yapo katika maisha yetu, familia, sehemu za kazi na jamii, na kuathiri kila mtu.
Dalili za matatizo ya akili ni pamoja na:
•Kuwa na hasira kupindukia
•Kukosa furaha katika maisha
•Kuwa na wasiwasi wa kupindukia
•Kukosa usingizi
•Kuwa na msongo mkali wa mawazo
Ni lazima tufanye kadiri tuwezavyo kuzuia magonjwa ya akili - kama watu binafsi na kama jamii
Ni muhimu kuendelea kutoa wito kwa serikali za kitaifa na za mitaa kuweka kipaumbele katika kupunguza mambo yanayojulikana kuwa hatari kwa afya ya akili ya watu Kama Ugumu wa Maisha, Migogoro ya Kijamii na Kimapenzi, Unyanyapaa wa Watu wenye Mahitaji Maalum pamoja na dhana au Mila potofu katika jamii
Pia kuimarisha wale wote wanashughulika na kulinda afya za akili kuanzia mtu Mmoja Mmoja hadi mashirika binafsi na kuunda nyenzo zinazohitajika kwa watu kustawi
Siku ya Afya ya Akili Duniani pia ni nafasi ya kuzungumza kuhusu afya ya akili kwa ujumla, jinsi tunavyohitaji kuitunza, na jinsi ilivyo muhimu kuzungumza kuhusu tunavyojisikia na kupata usaidizi ikiwa unatatizika
CHANZO: WHO, Mental Health Foundation