DOKEZO Maafisa Afya Dodoma pitieni Soko la Sabasaba msimu huu wa mvua, vyakula vinapangwa chini kukiwa na matope

DOKEZO Maafisa Afya Dodoma pitieni Soko la Sabasaba msimu huu wa mvua, vyakula vinapangwa chini kukiwa na matope

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Hili ni Soko la Sabasaba Jijini Dodoma mvua zinaponyesha mara nyingi kumekuwa na hali ya matope kwa baadhi ya maeneo na hivyo kuwa kero lakini pia usalama wa vyakula unakuwa hatarini.

Nimepita sokoni hapo jana, nimekuta akina mama wamepanga mboga zao chini wakiwa wametandika mfuko lakini nyingine zipo karibu na matope na nyingine zinarushiwa uchafu zikiwa hapohapo.

Maafisa Afya wapo, wanafanya nini sijui! Ni muhimu kuchukua hatua za haraka kurekebisha hali hii, ikiwezekana wanaoweka bidhaa chini wawe na utaratibu wa kuwekewa meza ili kuwa mbali na matope na uchafu uliopo kwenye ardhi.
 
Ndani ya soko lile Kuna kilabu Cha pombe za kienyeji asee ilinipa ukakasi mno kuona vile
 
Dodoma Eneo Tajwa Ni Chafu Kama Jaruba La Mpunga
 
Uongozi wa jiji uko kwenye usingizi mzito...
 
Ki ukweli ni aibu.Dar kuna soko la ndizi mabibo huwa ni chafu lakini hili soko la Sabasaba ni zaidi ya choo.Mvua ikinyesha wenye vyoo vya kulipia na nyumba za jirani wanatapisha vyoo.Kinyesi kinapita katikati ya wachuuzi,hasa wakina Mama wanaopanga bidhaa chini.

Tena bila aibu,soko hili lipo karibu kabisa na jiji ambapo ofisi za Afya zipo hapo.Mnatia aibu
 
CCM Iliwapa Uji Watu Kwenye Sherehe Zao Dodoma, Miaka 48
 
Hili ni Soko la Sabasaba Jijini Dodoma mvua zinaponyesha mara nyingi kumekuwa na hali ya matope kwa baadhi ya maeneo na hivyo kuwa kero lakini pia usalama wa vyakula unakuwa hatarini.

Nimepita sokoni hapo jana, nimekuta akina mama wamepanga mboga zao chini wakiwa wametandika mfuko lakini nyingine zipo karibu na matope na nyingine zinarushiwa uchafu zikiwa hapohapo.

Maafisa Afya wapo, wanafanya nini sijui! Ni muhimu kuchukua hatua za haraka kurekebisha hali hii, ikiwezekana wanaoweka bidhaa chini wawe na utaratibu wa kuwekewa meza ili kuwa mbali na matope na uchafu uliopo kwenye ardhi.
 

Attachments

  • VID-20250128-WA0031.mp4
    28.2 MB
Back
Top Bottom