Maalim na chaguzi tano za Zanzibar 1995 - 2015

Maalim na chaguzi tano za Zanzibar 1995 - 2015

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1576509499579.png

Jaws Corner
Uchaguzi wa Zanzibar 1995

Propaganda kuhusu Maalim na siasa za Zanzibar zimezoeleka nyakati kama hizi.

Yaandikwayo hupati kusikia lolote la maana kutoka kwao.

Haya wasemayo yanavutia watu kutaka kusikiliza kwa kuwa Maalim Seif katajwa.

Tufanye "deduction" kama "experiment" ndogo tu.

Maneno haya haya ndani ya video clips "substitute" jina la Maalim na mwanasiasa mwengine uangalie huo ujumbe utawavutia wasomaji wangapi.

Hakuna.

Hiki ndicho kipimo cha ukubwa wa Maalim katika siasa za Zanzibar.

Maalim kakabiliana katika uchaguzi na marais wote waliotawala Zanzibar baada ya vyama vingi kuruhusiwa mwaka wa 1992.

Hili si jambo dogo - Salmin Amour, Amani Karume na Dr. Shein.

Matokeo ya chaguzi zote hizo tano zinafahamika.

1576509699568.png

Kalenda ya CUF Uchaguzi wa 1995
Ikionyesha tarehe ya kupiga kura na Maalim kuingia Ikulu Zanzibar

Hii ni historia ya pekee kabisa.

Hofu iliyokuwapo hivi sasa na hii ni wazi.

Itakuwaje endapo Maalim atagombea 2020 na atashinda.

Tunaweza kuangalia "trend," kisha tukaweka juu yake "Law of Probability."

Jibu ni jepesi mno.
Sayansi haisemi uongo.

Tushajua nini matokeo ya Uchaguzi wa 2020 Zanzibar.

Shinikizo la siasa Zanzibar haipo kwa Maalim wala kwa Wazanzibari wapiga kura.

Wazanzibari wanajua kutumbukiza kura ndani ya sanduku.

Wazanzibari siku zote wameonyesha dhahiri nini wanataka.

Propaganda hizi mitandaoni zinaonyesha hofu iliyoko visiwani.

Lakini zaidi zinawasaidia wenye kutumia akili zao na elimu ya sayansi kuelewa hali halisi iliyoko na inavyoikabali CCM yote Bara na Visiwani.

Ikifikia hapa kunakuja na maswali.

Zanzibar itaendelea hivi hadi lini?

Njia nyepesi ya kummaliza Maalim Seif na ndoto ya Wazanzibari waliyonayo kwa nchi yao ni CCM kumshinda Maalim kwenye sanduku la kura bila ajua na kufuta uchaguzi.

Lakini hii kuwa Maalim hawezekani kushindika katika kura, matatizo na hizi propaganda hazitakwisha kamwe.

Maalim ataendelea kuwashughulisha. CCM wamepatwa na maradhi ya "wishful thinking."

Wangependa kumuona Maalim anaangukiwa na mbingu.

"Legacy," atakayoacha Maalim hakuna kiongozi ataifikia hata siku moja katika miaka hii ya karibuni.

Wapi duniani kumekuwa na "immigration" ya wanachama wote na kiongozi wao kwenda chama kingine kwa siku moja tu?

Hii ni "Exodus." Hii ni "phenomenon," ambayo inaeleza yale ambayo CCM wanajitahidi kujifanya kuwa hayapo.

Lakini ukweli ndiyo huu.

Yapo.

Salama ya CCM Zanzibar iko katika kupitisha sheria itakayomzuia Maalim kutogombea.

Lakini hili nalo lina hatari nyingi sana.

Hatari yake ni kuwa CCM Zanzibar itakuwa imejiongezea nyoya jingine kichwani.

Nyoya la hofu ya kumuogopa Maalim na Wazanzibari raia wapiga kura.

Manyoya haya yatawaelemea sana kichwani - kushindwa kushinda kwenye kura, kushindwa kwa GNU, kufuta uchaguzi, kumzuia Maalim kugombea...

Sasa tufike kuwa Zanzibar chama kinabakia CCM peke yake kwa ajili ya hofu ya kuwa CCM katika ushindani haijiwezi.

Inashindwa kila uchaguzi visiwani.

Hapo sasa tunafungua mlango wa vurugu.
 
Kwa mara ya kwanza you won a mind of a born again Christian.
Maalim wana mdhurumu sana ndio maana Shein hana amani ya mwili hadi roho, dhuluma aliyoifanya pamoja na CCM wote inamuumiza yeye anateketea ndani kwa ndani.
 
Kwa mara ya kwanza you won a mind of a born again Christian.
Maalim wana mdhurumu sana ndio maana Shein hana amani ya mwili hadi roho, dhuluma aliyoifanya pamoja na CCM wote inamuumiza yeye anateketea ndani kwa ndani.
Mzee Mohammed Said nasoma Sana maada zako lakini ya leo imenifanya nusuuzike nafsi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mara ya kwanza you won a mind of a born again Christian.
Maalim wana mdhurumu sana ndio maana Shein hana amani ya mwili hadi roho, dhuluma aliyoifanya pamoja na CCM wote inamuumiza yeye anateketea ndani kwa ndani.
Huo ndio ukweli usiyo fichika kwani aliye dhulumu hua analala usingizi lkn aliye dhulumiwa hua halali kila wakati anaswali na kumuomba mungu na kuzidisha ibada

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Zanzibar itaendelea hivi hadi lini?
Maneno haya madogo lakini yanaleta maana kubwa sana
???????????? zaidi ya mia na majibu yake ni mara mia
lakini hili moja linatosha kwa sasa
1. Tuna taka zanzibar yetu yenye mamlaka kamili nje na ndani ya nchi angalau yawe sawa na yale ya baada ya January 12.1964 na kabla april 26. 1964.

Agenda hii ni kwa chama chochote kilichotayari kutufikisha hapo,hata CCM Zanzibar wakiamua kuitekeleza agenda hii ,Watakuwa wamesha malizana na Maalim Seif na Wenzake kwenye Upinzani,lakini Wakiiacha ,basi wazanzibari hii ndo kiu yao. Si jengine,Atakaye kushika Maaraka Zanzibar atutekelezee hili,Iwe ACT,Iwe CUF iwe CHADEMA iwe yeyote.
 
Wazanzibari tutaitimiza ndoto hii iwe kweli,. ''TIME WILL TELL''
SUALA LA KUPIGA KURA ZANZIBAR HALINA TENA MAANA YOYOTE, KURA YANGU HAINA TENA THAMANI.
kama ilivyopoteza thamani kura ya 1963 iliyoleta uhuru wa 10/dec/1963.hatimae ikaleta mabadiliko ya Jan.12 1964.
Hivyo ndivyo inavyo elekea.Na Ndio Uhalisia unavyo lazimu kwa Taifa Kusimama kwa Miguu yake.
 
Maneno haya madogo lakini yanaleta maana kubwa sana
???????????? zaidi ya mia na majibu yake ni mara mia
lakini hili moja linatosha kwa sasa
1. Tuna taka zanzibar yetu yenye mamlaka kamili nje na ndani ya nchi angalau yawe sawa na yale ya baada ya January 12.1964 na kabla april 26. 1964.

Mamlaka ya Zanzibar yalipotea January 12 1964. hicho kipindi cha 12 January mpaka April 26 tayari ilikua inatawalia na Tanganyika nyuma ya pazia.

Uhuru wa Zanzibar ulidumu kutoka 10 Dec 1963 mpaka 11 Jan 1964.
 
Nditolo,
Kipi kilichokukosha ndugu yangu?
maalim seif sharifu hamad ni gwiji na mwamba haswaaa. kuna kichaa mmoja alienda zanzibar mwanzoni kabisa akiwa na ushamba wake uliokithiri ati akasema asilipwe malipo yake. asijue kwamba maalim kamzidi ujanja kabla hata yeye anachunga mifugo kwao na kiswahili chake kibovu kinachoumiza masikio
 
Kwenye uzi mwingine. Nimeshauri Maalim Seif agombee urais wa JMT na Zitto awe ngombea mwenza. Zanzibar watafutwe wana ACT wengine. Mara tano kwa Maalim inatosha.
 
Back
Top Bottom