we jamaa uvyama umekutia roho mbaya sana. Hivi ukiwa ccm ndio na akili zinakauka?Chadema wanaamini wao huwa hawafi inaskitisha sana
RIP Mzee Azzan, wana mageuzi na Wanaotaka mabadiliko tumepata pigo kubwa sana. Poleni familia, Wana wa Pemba, waTanzania na ACT-WAZALENDO .Marehemu Maalim Seif Mohamed Azzan amefariki dunia usiku wa kuamkia leo kisiwani Pemba. Marehemu ni miongoni mwa waasisi wa harakati za mageuzi na kuwaunganisha wazanzibari, kupigania haki na demokrasia ya vyama vingi.
Maalim Seif Azzan amewahi kuwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka jimbo la Pandani, wilaya ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba katika Bunge la kwanza la vyama vingi mwaka 1995-2000.
Mpaka mauti yanamkuta Marehemu alikuwa Afisa utwala wa chama cha ACT-Wazalendo kanda ya Pemba.
Chadema wanaamini wao huwa hawafi inaskitisha sana
RIP Mzee Azzan, wana mageuzi na Wanaotaka mabadiliko tumepata pigo kubwa sana. Poleni familia, Wana wa Pemba, waTanzania na ACT-WAZALENDO .
Toka maktaba :
28 Feb 2021
HAZINA ZA MAALIM: Mazungumzo na msaidizi wake mkuu kisiwani Pemba
Bwana Seif Mohammed Azzan aliwahi kuwa mbunge wa jimbo la Pandani (1995 - 2000) na baada ya kuacha ubunge, akaamuwa kujitolea maisha yake yote kuwa msaidizi mkuu wa Maalim Seif Sharif Hamad (Rahimahullah) kisiwani Pemba. Leo anazungumzia mafunzo yanayoweza kuchukuliwa kutoka maisha ya Maalim Seif kwa kizazi cha sasa na kijacho.
Source: Gumzo la Ghassani