Maamuzi magumu atakayoyafanya mzee warioba ni yapi?

Maamuzi magumu atakayoyafanya mzee warioba ni yapi?

Nduna Likapo

Member
Joined
Apr 25, 2013
Posts
97
Reaction score
19
Wanajamvi siku 2 sasa zimepita toka Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba atoe tamko mbele ya waandishi wa habari na akisisitiza kauli yenye utata na giza nzito ya kwamba Tume yake itafanya maamuzi magumu kutokana na kuwepo na maoni mengi yanayotofautiana toka kwa wananchi.Kauli hii ni tata inayohitaji mjadala wa kina kwa usalama wa taifa letu.Binafsi baada ya kufanya tathimini nimeshindwa kumuelewa mzee Warioba kwa yafuatayo.(1) Ni maamuzi yapi magumu watakayoyafanya kwenye katiba ya watanzania?haya maamuzi magumu hayatakuwa na harufu ya kulibeba kundi flani katika jamii?je hayo maamuzi hatakuwa na mkono wa wanasiasa na watawala?Watanzania tumeshafanya maamuzi magumu na kwa kutoa maoni kwa yale tunayoyataka na tume itimize wajibu wake na sio kutuzungusha na kauli zenye utata.Namuheshimu sana Mzee warioba na tume yake,Lakini wao kama tume hawatakiwa kuja na kauli zenye giza kwa wananchi,kazi ya tume ni kukusanya na kuyaratibu maoni ya watanzania na sio kufanya maamuzi magumu tusiyoyajua watanzania ni yapi.Huu ni Mtazamo wangu,Sijui wewe unafikiria nini kuhusu maamuzi magumu ya Mzee Warioba na Tume yake.Mungu ibariki Tanzania.
 
Maamuzi hayo yako kwenye maeneo ya Muungano (kuna watu wanataka Muungano wa Mkataba) na Dini (kuna watu wanataka OIC na Mahakama za Kadhi ziingizwe kwenye Katiba)!
 
Time will tell, let us wait and see,we don't need to speculate .
 
Mi naona anaharibu tu mchakato wa katiba mpya hana lolote la maana anaendeshwa kwa remote
 
Kwani akikubali oic kuna tatizo gani wajameni,maadamu watu wametoa maoni yao?.
 
Tufanye subila ndugu, ila Kama hatutaweza simama imara kupata katiba nzuri, tutaendelea kutaabika mpaka kiama.
 
Mkuu Nduna Likapo
Heshima kwako! Kauli hiyo ni pana lakini naona Mzee Warioba amejitahidi kuonyesha mwanga wa kile tume yake itakachofanya.

Ni ukweli kuwa katiba itakayoandikwa haiwezi kubeba maoni yote yaliyotolewa na wananchi. Ukifanya hivyo nadhani waweza pata kitabu ya upana toka pwani ya ziwa victoria hadi ziwa nyasa. Ni lazima yapembuliwe na kuchukua the best, huu ni uamuzi mgumu.

Si kila maoni yaliyotolewa na wananchi ni constitutional affair, mengine ni uratibu tu wa sheria zingine za nchi. Haya itabidi yaachwe na pengine wapatiwe watu wa law reform. Huu ni uamuzi mgumu.

Lakini pia lazima tukubali si kila maoni yanaweza ku_favour national interests at best. Kukubali mengine yaweza kuwa ni kudhoofisha taifa na kuhatarisha usalama. Kuna maoni yanaligawa zaidi taifa kuliko kudumisha umoja, kuna maoni yapo zaidi kubeba groups za watoa maoni kuliko taifa. Kuchanganua haya pia kwa tume ni uamuzi mgumu.

Ile tume imeundwa na watu wa different backgrounds, wengi wana weledi wa kutosha wakiwamo wakongwe wa sheria na sayansi jamii. Ni vema wakapewa muda na jamii ikaacha speculations. Wanajamii wengi wapo too eager kujua mustakabali wa maoni yao lakini process nzima ni too clear watu wawe na subira tu. Taifa kwanza watanzania!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nduna Likapo
Heshima kwako! Kauli hiyo ni pana lakini naona Mzee Warioba amejitahidi kuonyesha mwanga wa kile tume yake itakachofanya.

Ni ukweli kuwa katiba itakayoandikwa haiwezi kubeba maoni yote yaliyotolewa na wananchi. Ukifanya hivyo nadhani waweza pata kitabu ya upana toka pwani ya ziwa victoria hadi ziwa nyasa. Ni lazima yapembuliwe na kuchukua the best, huu ni uamuzi mgumu.

Si kila maoni yaliyotolewa na wananchi ni constitutional affair, mengine ni uratibu tu wa sheria zingine za nchi. Haya itabidi yaachwe na pengine wapatiwe watu wa law reform. Huu ni uamuzi mgumu.

Lakini pia lazima tukubali si kila maoni yanaweza ku_favour national interests at best. Kukubali mengine yaweza kuwa ni kudhoofisha taifa na kuhatarisha usalama. Kuna maoni yanaligawa zaidi taifa kuliko kudumisha umoja, kuna maoni yapo zaidi kubeba groups za watoa maoni kuliko taifa. Kuchanganua haya pia kwa tume ni uamuzi mgumu.

Ile tume imeundwa na watu wa different backgrounds, wengi wana weledi wa kutosha wakiwamo wakongwe wa sheria na sayansi jamii. Ni vema wakapewa muda na jamii ikaacha speculations. Wanajamii wengi wapo too eager kujua mustakabali wa maoni yao lakini process nzima ni too clear watu wawe na subira tu. Taifa kwanza watanzania!

umeeleza vizuri sana mkuu but unadhani kulikuwa naumuhimu kwa mzee Warioba kuongea vile katika wakati huu?kwa nini wasingefanya mambo kimya kimya na kwa uweledi na mwisho wa siku inaonekana kama wanatumia defence mechanism.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom