Maamuzi yote Tanzania hufanywa na Rais, anajificha kwa Watendaji!

Maamuzi yote Tanzania hufanywa na Rais, anajificha kwa Watendaji!

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Kila kinachoendelea Tanzania Rais ndiyo anayetoa maamuzi na amri kuanzia kupandisha bei za mafuta, umeme, kukamata raia kuwaweka rumande na kuwaachia pia kama akina Mbowe, Sabaya & Co. mpaka hili la kufukuzwa kwa Watanzania kwenye ardhi yao kwa mitutu ya Bunduki ni rais ndiyo anafanya siyo Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa, Wilaya au hata Makamba na Nape wala Polisi hivyo kama lawama tupeleke penyewe na tujue ni nani anahusika, tusizingizie watu wengine.

Kama Waziri Mkuu anapewa amri afanye anavyofanya atakataa vipi ? Iweje raisi wa nchi haongelei chochote wala kusema chochote ?

Watanzani muda umefika wa kuanza kumhusha raisi wa nchi ambaye ndiye Bosi moja kwa moja kwa kila kinachoendelea kwenye nchi yetu kwani ni yeye tu ndiye anayeweza kuzuia, amkeni, rais hadanganywi wala kupotoshwa hata siku moja kwanza ni kinyume chake!
 
Back
Top Bottom