Maana Halisi ya "Lockdown"...

Maana Halisi ya "Lockdown"...

Mfiaukweli

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2018
Posts
5,636
Reaction score
8,777
Wandugu, kuna misconception miongoni mwa Watanzania wengi niliokutana nao (na michango inayoletwa hapa) kuhusu lockdown (kuzuia watu wao kutoka majumbani kwao kwa kiwango fulani) ikiwa ni moja ya hatua za kupambana na COVID 19 pandemic. Nchi zote ambazo zimetangaza kuwa hadi sasa zimefanikiwa kuzuia maambukizi mapya ya coronavirus zikiwemo Taiwan na New Zealand zilitumia njia hii.

Kuna nchi ambazo ziliingia kwenye lockdown (hazijtangaza kuwa coronavirus free hadi sasa) zimeanza kulegeza zuio la watu kukaa majumbani mwao. Kuna nchi nyingine (ikiwemo Tanzania) ambazo hazikuingia kwenye lockdown.

Kinyume na imani ya Watanzania walio wengi (niliokutana nao au kusikia michango yao) lockdown haimaanishi kuwa watu wanazuwiwa kutoka majumbani mwao 100%. Haimaanishi pia kutofanya kazi au kuzuia magari ya mizigo. Watu walio kwenye lockdown wanaruhusiwa kutoka ili kufanya shughuli muhimu kwa mfano; kwenda bank, pharmacy, supermarket etc, etc.

Hitimisho: Tanzania sasa hivi ipo kwenye Lockdown ya kulazimishwa na majirani zetu (sasa hivi ni kama 70%). Malawi nao wakifunga mpaka wao na sisi tutakuwa tupo kwenye 98% lockdown - Msumbiji hatuna biashara kubwa sana nao inayohusisha usafirishaji wa mizigo. Tungechukua hatua hiyo wenyewe tungekuwa kwenye hali bora zaidi kuliko tutakayokuwa nayo tuendako.

Let's wait and see.
 
Chadema walikuwa wanalilia lockdown Kwasababu wana lipwa na serikali

Sisi Watanzania tuliowengi tunachapa kazi

Umeelewa kilichoandikwa lakini? Wewe ni mfano halisi (living example) ya wale wasioelewa maana ya lockdown.
 
Kwani wakati wanaingia kwenye LOCKDOWN walisema wataweka LOCKDOWN DAIMA NA MILELE ???
 
Wamachinga na mabodaboda watakuwa kazini kwenye lock down? Watu wataruhusiwa kwenda kupalilia au kuvuna mazao yao shambani kwenye lock down? Ukiruhusu supermarket mijini ni waTZ wangapi wanapata mahitaji yao huko? Eti ufunge magenge na masoko, wewe unatania!!!
 
Wamachinga na mabodaboda watakuwa kazini kwenye lock down? Watu wataruhusiwa kwenda kupalilia au kuvuna mazao yao shambani kwenye lock down? Ukiruhusu supermarket mijini ni waTZ wangapi wanapata mahitaji yao huko? Eti ufunge magenge na masoko, wewe unatania!!!

Sent using Jamii Forums mobile app

Wapi nilipoandika kuwa masoko na magenge yafungwe? Are you hallucinating?
 
Wapi nilipoandika kuwa masoko na magenge yafungwe? Are you hallucinating?

When I read any statement, I do read both along and between the lines. Did you say that masoko na magenge yatakuwa exempted from lock down?
 
When I read any statement, I do read both along and between the lines. Did you say that masoko na magenge yatakuwa exempted from lock down?

I never mentioned hospitals and police stations either, does your reading between the lines tell you that they have to be closed as well during lockdown?
 
Wandugu, kuna misconception miongoni mwa Watanzania wengi niliokutana nao (na michango inayoletwa hapa) kuhusu lockdown (kuzuia watu wao kutoka majumbani kwao kwa kiwango fulani) ikiwa ni moja ya hatua za kupambana na COVID 19 pandemic. Nchi zote ambazo zimetangaza kuwa hadi sasa zimefanikiwa kuzuia maambukizi mapya ya coronavirus zikiwemo Taiwan na New Zealand zilitumia njia hii.

Kuna nchi ambazo ziliingia kwenye lockdown (hazijtangaza kuwa coronavirus free hadi sasa) zimeanza kulegeza zuio la watu kukaa majumbani mwao. Kuna nchi nyingine (ikiwemo Tanzania) ambazo hazikuingia kwenye lockdown.

Kinyume na imani ya Watanzania walio wengi (niliokutana nao au kusikia michango yao) lockdown haimaanishi kuwa watu wanazuwiwa kutoka majumbani mwao 100%. Haimaanishi pia kutofanya kazi au kuzuia magari ya mizigo. Watu walio kwenye lockdown wanaruhusiwa kutoka ili kufanya shughuli muhimu kwa mfano; kwenda bank, pharmacy, supermarket etc, etc.

Hitimisho: Tanzania sasa hivi ipo kwenye Lockdown ya kulazimishwa na majirani zetu (sasa hivi ni kama 70%). Malawi nao wakifunga mpaka wao na sisi tutakuwa tupo kwenye 98% lockdown - Msumbiji hatuna biashara kubwa sana nao inayohusisha usafirishaji wa mizigo. Tungechukua hatua hiyo wenyewe tungekuwa kwenye hali bora zaidi kuliko tutakayokuwa nayo tuendako.

Let's wait and see.
Kufunga mipaka siyo lockdown.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom