Maandalizi ya utoaji tuzo za michezo tanga yakamilika

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Maandalizi ya utoaji tuzo za wanamichezo kwa msimu wa 2022/2023 zitakazotolewa Juni 12, 2023 jijini Tanga yamekamilika ambapo wachezaji mbalimbali watapokea tuzo zao huku Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma.

Hafla hiyo ya utoaji tuzo itahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali na taasisi zisizo za Serikali akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu, Rais wa Shirikisho la Mpira Tanzania (TFF) Bw. Wales Karia, wageni mbalimbali, wananchi wa viunga vya jiji la Tanga pamoja na wilaya za Mkoa wa Tanga na mikoa jirani.

 
Wekeni updstes hapa ya watu waliopata tuzo
 
hakuna anayefatilia upuuzi huu atupe majibu kinaendelea nini huko
 
Reactions: K11
Mnaofuatilia hii kitu bado tuzo hazijaanza?
 
Dah! Sasa mbona karibia tuzo zote zinachukuliwa na Yanga!! Hii siyo fair hata kidogo. TFF wanawapendelea Yanga! 🙄
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…