Maandamano Kenya ni Ukomavu wa Akili

Mfikirishi

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
8,939
Reaction score
10,403
Binadamu ni akili inayoishi ndani ya mwili! Na akili inahitaji elimu bora ili kuikomaza vizuri. Siasa na serikali ni mifumo ya kijanja janja sana. Inahitajika akili iliyokomaa kuweza kukabiliana nayo!

Maandamano yanayofanyika nchini Kenya hayana viongozi wa kisiasa! Ni vijana walioelimisha akili zao lakini mifumo ya wanasiasa imewatelekeza! Adui yao mkubwa ni wanasiasa na mifumo yao kandamizi! Wamekata tamaa! Hawana cha kupoteza! Wapo tayari kutafuta wanachokitaka!

Tunaweza kuwadharau kwa sababu zozote zile lakini vijana wa Kenya wanazidi kutu-prove wrong! Ndiyo! Wana ukomavu wa akili! Ndicho pekee unachoweza kusema. Najua wale wa "sisi tunataka amani" hawatanielewa!


Screenshot_20240621-033758.png
Screenshot_20240621-021541.png
Screenshot_20240621-021516.png
Pia soma:Nguvu ya Umma: Bunge lalazimika kubadilisha Muswada wa Sheria ya Fedha baada ya maandamano ya Wananchi
 
Wakiamua jambo lao wanalifanya....hawana unafiki....wote kwa pamoja wanashirikiana.
 
Kenya tokea kitambo wanajielewa, kwa sababu ya matabaka ktk jamii na wengi kuwa na maisha magumu

kumbuka enz za banana vs orange, mungiki
 
Kenya tokea kitambo wanajielewa, kwa sababu ya matabaka ktk jamii na wengi kuwa na maisha magumu

kumbuka enz za banana vs orange, mungiki
Maisha magumu unayatafsiri vipi ndugu.
Kwa mfano mtu kama Eric Omondi huwa anajitokeza front line kwenye maandamano naye utasema ana maisha magumu?
Mimi nadhani sababu kubwa ni kwamba raia wao wana awareness kubwa kutuzidi yaani vichwa vyao vinaelewa mambo kwa haraka kutuzidi.
Chukulia mfano tu kwetu Tanzania kusanya watu 100 uongee nao tena mjini Dar es salaam tuachane na mikoani hiyo ni kesi nyingine na kuwaelekeza kuhusu uhuru wa raia na haki zao halafu hesabu ni watu wangapi katika hao watu 100 watakaokuelewa,nina imani watakaokuelewa kidogo hawatozidi watu 10 waliobaki wataona umewapotezea muda wao wa kwenda kupiga deiwaka wapate chochote kitu cha kuendesha familia zao kwa siku moja au mbili baada ya hapo akili zao zimeridhika.
Wakati waandishi wa habari wa kenya pamoja na wasanii wote wanaungana kupinga vitendo vya aina yoyote vya unyanyasaji wasanii wa kwetu Tanzania wanageuka machawa wapewe nafasi ya kuimba tumeupiga mwingi wapate hela ya kula leo bila ya kuwaza ustawi wa familia zao au watoto wao kwa miaka ijayo.
Haya ukija kwa vyama vyetu vya pinzani na vyenyewe haviko serious kivile ni kama wamekaa kimtegomtego wakivizia maslahi fulani upande wao ndio maana unaweza ukaona kiongozi wa chama cha upinzani anaweza akaitisha maandamano halafu yeye mwenyewe anaenda kujificha kwenye hotel huku anayaangalia maandamano kupitia kwenye TV.
Kwa hili tukubali Wakenya wametuacha mbali sana.
 
Wanasemaga dua la kuku halimpati mwewe. Hapa vipi?
IMG-20240620-WA0029.jpg
 
Kenya ni lazima wafanye hivyo, kwa maana maisha yao hayana tofauti na kifo. Yaani kenya asilimia kubwa ya walala hoi hawoni tofauti kati ya kuwa hai na kufa. Ndiyo maana wanafanya mambo mengi ya hatari, kutia ndani kuandamana mbele ya vyombo vya dola vyenye silaha za moto.
 
Back
Top Bottom