Maandamano Kenya: Uhuru Kenyatta atoa wito viongozi kufanya mazungumzo na Wakenya

Maandamano Kenya: Uhuru Kenyatta atoa wito viongozi kufanya mazungumzo na Wakenya

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1719350918231.png

Uhuru Kenyatta​

Rais wa mstaafu wa Kenya, Uhuru Kenyatta ametoa tamko kuhusu maandamano yanayoendelea dhidi ya Muswada wa Fedha.

Kiongozi huyo wa zamani wa taifa alituma salamu zake za rambirambi kwa Wakenya waliopoteza maisha yao wakati wa maandamano ya Jumanne, akisema ilikuwa haki yao ya kikatiba kuandamana.

"Nawajia nikiwa na moyo mzito nikiwa na huzuni kwa kupoteza maisha kutokana na hali ya sasa inayotawala nchini. Ni haki ya Wakenya kuandamana kama inavyotambuliwa na Katiba ya Kenya 2010. Pia ni jukumu la viongozi kuwasikiliza wale wanaowaongoza," alisema Uhuru.

Uhuru aliendelea kuwataka wananchi kuwa watulivu na kuhimiza viongozi wakumbatie mazungumzo na watu.

"Kama rais wenu wa zamani, nimehisi uzito wa kuwaongoza Wakenya. Kwa hivyo naomba hekima na ustaarabu vianzishwe na amani na maendeleo yawe mali yetu sote kama watoto wa Kenya," alisema.

Rais huyo wa zamani alithibitisha uungaji mkono wake kwa Wakenya na kuwataka viongozi "Waongee na watu na si kwa watu."

"Ninaomba amani na uelewa kwa kila Mkenya na kwa sote tukumbuke kuwa Kenya ni kubwa kuliko mmoja wetu; hakuna kitu kilichochongwa kwenye jiwe ambacho hakiwezi kubadilishwa," alisema.

PIA SOMA
- LIVE - Yanayojiri Maandamano Kenya: Waandamanaji wafika Bungeni, wawili wauawa kwa risasi

- Waandamanaji Nairobi wavamia jengo la Bunge baada ya kuwashinda nguvu polisi, yasemwa waandamanaji 10 wameuawa kwa kupigwa risasi halisi
 
Kenyataa naomba umwache huyo zakayo dikteta yeye si much know na anafkiri kwamba jeshi linaweza kuua harmless raia elfu kumi kwa wakati mmoja, wewe mwache aonje joto ya jiwe, kwanza hakuheshimu, na mwannzon alikusumbua kwa kumharass mama yako mzazi, na familia yako ila ulikuja front na ukamuambia aje ila akaufyata hakujua au hajui wewe ni mtoto wa mjini, mtoto wa rais wa kwanza kenya aliepigania uhuru wa kenya, mtoto mwenye konekshen kubwa na za hatari dunia nzima, anataka kua kama wewe ni kwamba haiwezekani,
Achana nae
 
Kenyatta apige kimya ili Zakayo akose wakumbebesha lawama kuwa ni mchochezi wa maandamano

Hii kitu ishachangamka hakuna haja ya kusukuma tena, ishashika mteremko na haiko kwenye gia soon inamvaa MTU nakumtoa mafuta ya kichwani 😁
 
Jamani vijana wakitanzania tuandamame kupinga wizi WA Mali za umma na upumbavu wa bunge la CCM
 
Vijana waTanzania tuandamane kukomesha cartels zilizopo nchini chini ya kikwtletwe
 
Maneno ya hekima ruto ya chukue. Itasaidia






KAZI ni kipimo cha UTU
 
Back
Top Bottom