BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
Imetolewa mara ya mwisho: 24.10.2008 0057 EAT
Maandamano kwa JK yapigwa marufuku
Na Rehema Mwakasese
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema haliko tayari kutoa kibali cha maandamano ya vuguvugu la kudai mabadiliko ya Katiba ikiwamo kumpunguzia Rais madaraka na kufutwa adhabu ya kifo.
Akizungumza jana na gazeti hili, Kamishna Msaidizi wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bw. Evarist Mangala, alisema Jeshi hilo halitatoa kibali kwa waaandaaji wa maandamano hayo kwa sababu Rais hayupo tayari kuyapokea.
Bw. Mangala alisema waandaaji hao walikwenda ofisini kwake juzi kuomba kibali hicho, lakini hawakuwa na kielelezo chochote ambacho kinaonesha Rais alikwishawakubalia kuyapokea.
"Walikuja hapa ofisini juzi na tukaongea nao na nilipotaka vielelezo vinavyoeleza Rais kuyapokea maandamano hayo hawakuwa navyo na pia hawakuwa na maelezo yoyote ambayo yanaonesha Rais kukubali. Kwa hiyo tukaona hakuna umuhimu wa kutoa kibali cha maandamano hayo," alisema Bw. Mangala
Alisema kuwa endapo wanaharakati hao wataandamana bila kibali, sheria itachukua mkondo wake kwani watakuwa wamevunja taratibu za nchi, hivyo aliwataka wasifanye maandamano hayo.
Maandamano hayo ambayo yamepewa jina la Mkusanyiko Mtakatifu wa Amani (MMA) yatashirikisha wananchi wa kawaida na wanaharakati ambapo hoja nyingine wanazotaka zitekelezwe ni pamoja na kutaka kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na sheria za uchaguzi ziangaliwe upya ili haki itendeke.
Pia wanataka Umoja wa Mataifa usaidie kuwafikisha mahakamani watu waliohusika na mauaji kisiwani Pemba Januari 27, 2001 ikiwa ni pamoja na waliofanikisha mauaji hayo bila kuzingatia haki za binadamu, yakiwamo ya Bulyanhulu, Shinyanga.
Maandamano kwa JK yapigwa marufuku
Na Rehema Mwakasese
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limesema haliko tayari kutoa kibali cha maandamano ya vuguvugu la kudai mabadiliko ya Katiba ikiwamo kumpunguzia Rais madaraka na kufutwa adhabu ya kifo.
Akizungumza jana na gazeti hili, Kamishna Msaidizi wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Bw. Evarist Mangala, alisema Jeshi hilo halitatoa kibali kwa waaandaaji wa maandamano hayo kwa sababu Rais hayupo tayari kuyapokea.
Bw. Mangala alisema waandaaji hao walikwenda ofisini kwake juzi kuomba kibali hicho, lakini hawakuwa na kielelezo chochote ambacho kinaonesha Rais alikwishawakubalia kuyapokea.
"Walikuja hapa ofisini juzi na tukaongea nao na nilipotaka vielelezo vinavyoeleza Rais kuyapokea maandamano hayo hawakuwa navyo na pia hawakuwa na maelezo yoyote ambayo yanaonesha Rais kukubali. Kwa hiyo tukaona hakuna umuhimu wa kutoa kibali cha maandamano hayo," alisema Bw. Mangala
Alisema kuwa endapo wanaharakati hao wataandamana bila kibali, sheria itachukua mkondo wake kwani watakuwa wamevunja taratibu za nchi, hivyo aliwataka wasifanye maandamano hayo.
Maandamano hayo ambayo yamepewa jina la Mkusanyiko Mtakatifu wa Amani (MMA) yatashirikisha wananchi wa kawaida na wanaharakati ambapo hoja nyingine wanazotaka zitekelezwe ni pamoja na kutaka kuwepo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na sheria za uchaguzi ziangaliwe upya ili haki itendeke.
Pia wanataka Umoja wa Mataifa usaidie kuwafikisha mahakamani watu waliohusika na mauaji kisiwani Pemba Januari 27, 2001 ikiwa ni pamoja na waliofanikisha mauaji hayo bila kuzingatia haki za binadamu, yakiwamo ya Bulyanhulu, Shinyanga.