29 December 2024
Dar es Salaam
Maandamano ya Jubilei Jimbo Kuu jijini Dar es Salaam 2025
View: https://m.youtube.com/watch?v=hDK2Hmt-zN8 yaliyoanzia kanisa la St Peters lililopo Oysterbay Mbuyuni hadi kanisa kuu la St Joseph eneo la Posta katika ya jiji la Dar es Salaam eneo la Posta.
Huko Tabora pia Kardinali Protase Rugambwa, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Tabora, Tanzania alisema Tarehe 29 Desemba 2024 ni ufunguzi wa Maadhimisho ya Jubilei kuu ya Miaka 2025 ya Ukristo, tayari kukutana na Kristo Yesu, Lango la Matumaini na Wokovu. Huu ni mwaka wa neema na rehema. Watu wa Mungu Jimbo kuu la Tabora wanaitwa na kutumwa kuwa ni watu wa shukrani katika upendo, imani na matumaini, tayari kumwiga Bikira Maria aliyeshiriki kwa namna ya pekee katika mpango wa Mungu wa kumkomboa mwanadamu.
Kardinali Protase Rugambwa anawaalika watu wa Mungu kushiriki kikamilifu katika mchakato wa ujenzi wa Kanisa kwa nguvu zao na rasilimali walizokirimiwa na Mungu, kwani wanapaswa kuwajibika.
Bikira Maria Mama wa Mungu na Mkombozi wa ulimwengu, awasindikize katika maisha na utume wao. Waamini waweke nia kwa mwaka 2025 ili weweze kufanya mapenzi ya Mungu na waendelee kuombea amani kwa Tanzania, amani kwa Mataifa yote duniani. Mwenyezi Mungu alete amani kule kwenye machafuko, kutoelewana, magomvi na vita. Waamini wamwombe Emanueli, Mfalme wa amani aweke mkono wake na amani yake itawale.
Dar es Salaam
Maandamano ya Jubilei Jimbo Kuu jijini Dar es Salaam 2025
View: https://m.youtube.com/watch?v=hDK2Hmt-zN8 yaliyoanzia kanisa la St Peters lililopo Oysterbay Mbuyuni hadi kanisa kuu la St Joseph eneo la Posta katika ya jiji la Dar es Salaam eneo la Posta.
Huko Tabora pia Kardinali Protase Rugambwa, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Tabora, Tanzania alisema Tarehe 29 Desemba 2024 ni ufunguzi wa Maadhimisho ya Jubilei kuu ya Miaka 2025 ya Ukristo, tayari kukutana na Kristo Yesu, Lango la Matumaini na Wokovu. Huu ni mwaka wa neema na rehema. Watu wa Mungu Jimbo kuu la Tabora wanaitwa na kutumwa kuwa ni watu wa shukrani katika upendo, imani na matumaini, tayari kumwiga Bikira Maria aliyeshiriki kwa namna ya pekee katika mpango wa Mungu wa kumkomboa mwanadamu.
Kardinali Protase Rugambwa anawaalika watu wa Mungu kushiriki kikamilifu katika mchakato wa ujenzi wa Kanisa kwa nguvu zao na rasilimali walizokirimiwa na Mungu, kwani wanapaswa kuwajibika.
Bikira Maria Mama wa Mungu na Mkombozi wa ulimwengu, awasindikize katika maisha na utume wao. Waamini waweke nia kwa mwaka 2025 ili weweze kufanya mapenzi ya Mungu na waendelee kuombea amani kwa Tanzania, amani kwa Mataifa yote duniani. Mwenyezi Mungu alete amani kule kwenye machafuko, kutoelewana, magomvi na vita. Waamini wamwombe Emanueli, Mfalme wa amani aweke mkono wake na amani yake itawale.