Maandamano ya Utupu Kampala: Wanawake Watatu Wakamatwa kwa Kelele za Kupinga Ufisadi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648

Polisi nchini Uganda wamewakamata wanawake kadhaa waliokuwa wakifanya maandamano ya utupu kupinga ufisadi nchini humo.

Wanawake hao, baadhi wakiwa na vifua wazi, na mabango, walikamatwa walipokuwa wakielekea Bungeni huku wakipiga kelele za kupinga ufisadi na serikali.



Waandamanaji hao wametambulika kama Praise Aloikin, mwanafunzi wa sheria katika Chuo Kikuu cha Makerere, Norah Tshetshe, na Kemitoma Siperia Mollie, kiongozi wa zamani wa serikali ya wanafunzi.

Kwa mujibu wa Luke Owoyesigyire, ambaye ni Msemaji wa Polisi, amesema watatu hao wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi (CPS) Kampala kwa mashtaka ya kusababisha usumbufu.


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…