Maandiko haya mbona kama yana ukakasi na mashaka makubwa?

Maswqli yako 6 na 7 ni kufuru.

Nikupe kipande cha ushahri. Ukimuomba Mungu akufunulie ufahamu wa maandiko yake Matakatifu atafanya hivyo. Elewa kuwa Moabu na Waamoni walikuja kufutwa baadaye maana uzao wao ulipatikana kupitia matendo haramu. Ingawa Torati ilikuja baadaye sana baada ya Lutu. Zaidi ya miaka 400 lakini dhambi yao ilidumu na walipatilizwa kupitia upanga wa Israeli...
 
Biblia haisemi kuwa hicho kitendo Ni kitendo kizuri,ndio maana hicho kizazi kilichotokea hapo Ni kizazi kilicholaaniwa.ndio maana huko mbeleni biblia inakataza mahusiano ya kimaprnzi Kati wa ndugu wa karibu
 
Kwanza Lutu sio nabii,sio kila character anayetokea kwenye Biblia ni Nabii,wengi ni maarufu lakini sio manabii wala mitume.

Nyie kama mmeamua kumpa Unabii mpeni hatushangai lakini vitabu vya kale kabisa vinatupa habari ya Lutu. Lutu kimsingi hakuwa mtu mbaya na ndio maana yeye na familia yake walisalimika isipokuwa mkewe aliyegeuka jiwe la chumvi.

Matendo yalitajwa kufanywa na Binti za Lutu ndio kama hayo na kwa kukusaidia tu baada ya hao mabinti kupata mimba kila mmoja alijifungua mtoto wa kiume ambao ni mmoja ndio kizazi cha Waammoni na mwingine ndio ameleta kizazi cha Wamoabi.Haya mataifa mawili ndiyo kati ya mataifa yaliyowasumbua Wanawaisrael kinoma na ilikuwa ni matokeo ya hiyo laana waliyoitafuta mama zao.

Sasa anayebisha atueleze Waamoni na Wamoabi asili yao ni wapi?
 
Biblia inaweza gawanywa mara nne namna ya kuisoma ili uelewe vizuri,inaweza gawanywa katika makundi kama ifuatavyo

1.Nyakati za Ujinga(Anguko la mwanadamu)
Hiki nikipindi kabla Mungu hajaweka sheria kali ya kumuongoza binadamu ndio maana matukio kama ya Lutu kuzaa na binti zake haikuwa shida ni makusudi tu ya Mungu mwenyewe na hicho nikipindi kabla ya torati.

2.Nyakati za sheria(Torati) ya Musa Mungu alikuwa akiwaandaa watu wake waachane na mambo machafu waliyokuwa wakitenda utumwani ili wafike caanan wakiwa safi, Ndip tunaona katazo la kula baadhi ya wanyama lakin nyuma ya hapo watu walikuwa wanakula hovyo tu.Na ukisoma Walawi 18:6 nakuendelea utaona ni chukizo kwa Mungu kufanya kama Lutu.

3.Neema kwa mataifa
Hiki ndicho kipindi tulichonacho sasa ambapo Injili inahubiliwa hado uchochoroni, yaani watu wa mataifa ndio wanashauku kubwa zaidi kumtafuta na kumhubiri Kristo kuliko hata ilikotokea hiyo imani..Tunaishi kwa neema ya kristo kila dhambi ina msamaha kasoro kukufuru roho mtakatifu.Lakin enzi ya Musa mzinzi alipigwa mawe hadi kifo.

4.Nyakati za Ufufuo na kunyakuliwa
Ndicho kipindi kinachokuja mbele yetu..
Kwahiy ili uisome Bible vizuri kwanza ujue mambo hayo....
 
Ni kweli na ukiangalia kipindicho hicho kilikuwa cha nabii Ibrahim why atokee na rutu at the same time
 
Kumtetea Mtume kwa kuleta ajenda za Lutu ni uchizi,we ushawahi kukuta mkristu yeyote anamtaja Lutu kama Nabii?Lutu ni character tu kama Character wengine wengi ambao ni mashuhuri lakini hawana jambo,kuna akina Lutu hao,akina Yefta,akina Samson na wengine wengi ambao nyie kwa kutokujua kwenu mmeamua kuwapa Unabii.

Biblia haiwezi kupepesa macho kwa sababu inasema ukweli,eti kwa sababu ni ndugu yake Ibrahimu so Biblia ifiche habari za aibu kuhusu yeye. Hapana.

Ulichoandika kuhusu Mungu kwenye Wakorinto ni mfano mdogo sana wa kundi kubwa lenye upeo mdogo sana na hivyo kukujibu na kukuelezea ni kupoteza muda.
 
Sijaelewa Mtume na Lutu wanahusiana vipi hadi uwalinganishe hapo.

Kushabikia vita za kidini ni kuonyesha udhaifu wako wa kiimani, kila mtu abaki na anachokiamini.

Upendo utawale[emoji3577]
Tunafunzana na kueleweshana mkuu ndio maana kuna Sunday school na madrasa..kwaajil ya kufunza watoto so kama kipindi ulikosa ukiwa mtoto Jf ni shule tosha kama unataka kujifunza
 
Tunafunzana na kueleweshana mkuu ndio maana kuna Sunday school na madrasa..kwaajil ya kufunza watoto so kama kipindi ulikosa ukiwa mtoto Jf ni shule tosha kama unataka kujifunza
Biblia haifundishwi kwa kutoa mistari au mstari mmoja then uutafsiri
 
Sawa lete Madini huku ukishushia na vipande vya maandiko ili kuthibitisha comment yako.
 
Biblia haisemi kuwa hicho kitendo Ni kitendo kizuri,ndio maana hicho kizazi kilichotokea hapo Ni kizazi kilicholaaniwa.ndio maana huko mbeleni biblia inakataza mahusiano ya kimaprnzi Kati wa ndugu wa karibu
Sawa, nimekuelewa. Nashkuru tuumeelewana hicho kitendo cha Lutu na Bintize hakijakubaliwa.
 
Endelea kujifunza biblia shida ni kwamba unajifunza kwa lengo la kutafuta mapungufu.

Kitu ambacho utamaliza kuisoma ukibaki na ujinga wako.

#MaendeleoHayanaChama
Nipe hoja, nifunze ili niielewe na sio kuniletea blabla. Kwani nilichokiandika ndani ya Bible hakipo?
 
Kwahiyo Lutu na Binti zake siku ya kiama wataenda Motoni au Mbinguni kwenye uzima wa milele?
 
hakuna ukakasi hapo. Biblia iko tofauti na vitabu vingine vya dini. haifichi uovu wa mtu. Watoto waliozaliwa hapo ndiyo jamii za wamoabu na waamaleki ambapo ukisoma pentachuchs na hata vitabu vya samweli na wafalme utaona ni mojawapo ya jamii ambazo ziliwasumbua sana Waisraeli, na Mungu aliwaamuru Waisraeli wawaangamize ikiwa ni pamoja na wana wa kanaani-wahiti,wahivi, wayebusi nk.

issue ya lutu inaonyesha jinsi incest-hasa paternal na maternal ilivyo mbaya isivyokubalika mbele za Mungu. Na zao lake linaweza kuwa zao la watu waovu sana. Maana jamii hizo ndizo zilikuwa zinatoa hata watoto wao kafara kwa kuwachoma moto kwa miungu wao kemoshi-mungu wa wamoabu na milkomu wa amoni.

by the way jamii hizo ndiyo present day east of jordani river-nchi ya jordan na baadhi ya palestina
 
Kwahiyo Lutu ana dhambi au hana dhambi? Ni wa Motoni au Mbinguni kwa mujibu wa Biblia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…