Mabadiliko ya sheria ya Mazingira yazingatie kudhibiti makelele katika majiji Makubwa

Mabadiliko ya sheria ya Mazingira yazingatie kudhibiti makelele katika majiji Makubwa

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Kama ambavyo tumewahi kujadili hapa JF kuhusu makelele yaliyokithiri katika miji yetu. Ipo haja katika mabadiliko ya sheria za mazingira ambayo yatajadiliwa bungeni kuhakikisha hivi vipaza sauti bubu katika masoko, fremu za maduka na vibiashara ndogondogo zinadhibitiwa.

Kwa sasa wauza sumu ya panya, wauza nguo, wauza nyama, wauza nguo kila mmoja unakuta ana spika yake inaita biashara, yaani ni vurugu mtindo mmoja hakuna utulivu kabisa. Hii inasababisha ukosefu wa utulivu kwa watu na misongo ya mawazo.

Pia katika vituo vya madaladala
unakuta Walokole na Maspika yao, ni kuunguruma mtindo mmoja. Naamini katika taratibu za mipango miji, shughuli za Ibada zimetengewa maeneo maalum japo kwa dharura za hapa na pale zinaweza kufanyika ktk viwanja kadha wa kadha.

Kuhusu adhana za Waislamu, kama ile ya Alfajiri iwe strictly ni kuhusu adhana, isizidi dakika 3. Na pia Kiwango cha sauti ambacho spika za msikitini kiwe kile ambacho hakina madhara kwa masikio ya watu.

Haya mamiziki ya matangazo yanayopitishwa barabarani katika magari ya matangazo huku kukiwa na wasanii wakiimba na kucheza ili kutangaza bidhaa fulani yadhibitiwe, haya yanakosesha sana watu utulivu.

Haya mabodaboda yanayofunga spika za miziki nayo yazuiwe, ni hatari kwa usalama barabarani.

Mabar yanayopiga miziki ktk makazi ya watu nayo itafutwe namna ya kudhibiti hiyo hali.

Pengine watu hawaelewi kuwa utulivu wa kiakili wa watu unasaidia ktk productivity. Ukivuruga utulivu wa watu hata nchi haiwezi kuendelea.

Haya makelele mijini yatafutiwe dawa!
 
Mzee baba kuepusha hizo kero tafuta na jenga nyumba yako pembezoni mwa mji ambapo utakuwa na shamba na mifugo yako, ikifika ijumaa unaenda zako shamba kujipumzisha! Matajiri wenzako mjini ndio tunafanya hivyo
 
Hiyo yote ni kutokana na ubovu wa mipango miji yaani unakuta ndani ya makaz ya watu Kuna Kanisa, msikiti, baa mara kiwanda yaan full fujo.
 
Kama ambavyo tumewahi kujadili hapa JF kuhusu makelele yaliyokithiri katika miji yetu. Ipo haja katika mabadiliko ya sheria za mazingira ambayo yatajadiliwa bungeni kuhakikisha hivi vipaza sauti bubu katika masoko, fremu za maduka na vibiashara ndogondogo zinadhibitiwa.

Kwa sasa wauza sumu ya panya, wauza nguo, wauza nyama, wauza nguo kila mmoja unakuta ana spika yake inaita biashara, yaani ni vurugu mtindo mmoja hakuna utulivu kabisa. Hii inasababisha ukosefu wa utulivu kwa watu na misongo ya mawazo.

Pia katika vituo vya madaladala
unakuta Walokole na Maspika yao, ni kuunguruma mtindo mmoja. Naamini katika taratibu za mipango miji, shughuli za Ibada zimetengewa maeneo maalum japo kwa dharura za hapa na pale zinaweza kufanyika ktk viwanja kadha wa kadha.

Kuhusu adhana za Waislamu, kama ile ya Alfajiri iwe strictly ni kuhusu adhana, isizidi dakika 3. Na pia Kiwango cha sauti ambacho cha Spika za msikitini kiwe kile ambacho hakina madhara kwa masikio ya watu.

Haya mamiziki ya matangazo yanayopitishwa barabarani katika magari ya matangazo huku kukiwa na wasanii wakiimba na kucheza ili kutangaza bidhaa fulani yadhibitiwe, haya yanakosesha sana watu utulivu.

Haya mabodaboda yanayofunga spika za miziki nayo yazuiwe, ni hatari kwa usalama barabarani.

Mabar yanayopiga miziki ktk makazi ya watu nayo itafutwe namna ya kudhibiti hiyo hali.

Pengine watu hawaelewi kuwa utulivu wa kiakili wa watu unasaidia ktk productivity. Ukivuruga utulivu wa watu hata nchi haiwezi kuendelea.

Haya makelele mijini yatafutiwe dawa!
Tanzania kuna kifo Cha taaluma ya Mipango-miji, hivyo hayo uliyoeleza hayawezekani kutekelezwa Kama unavyofikiri.
Mipango-miji ni Kama msingi kwenye ujenzi wa nyumba, ukishakosea suala hili Kamwe haitaweza kufanya jambo lingine vizuri na likatengemaa. Never.

Kumbuka: Nyumba imara na bora huanzia na hatua ya ujenzi wa msingi imara.
 
Tanzania kuna kifo Cha taaluma ya Mipango-miji, hivyo hayo uliyoeleza hayawezekani kutekelezwa Kama unavyofikiri.
Mipango-miji ni Kama msingi kwenye ujenzi wa nyumba, ukishakosea suala hili Kamwe haitaweza kufanya jambo lingine vizuri na likatengemaa. Never.

Kumbuka: Nyumba imara na bora huanzia na hatua ya ujenzi wa msingi imara.

Hivi ilikuwaje mkoloni wa Kijerumani aliweza kupanga miji tena enzi hizo za kale ika CCM na serikali zake washindwe kitu basic kama hiki?
 
Hivi ilikuwaje mkoloni wa Kijerumani aliweza kupanga miji tena enzi hizo za kale ika CCM na serikali zake washindwe kitu basic kama hiki?

"Black people are not complete human beings because they don't have a good brain to govern the society as White people. They are still under the process of becoming the complete human beings."

Pieter W. Botha, a former President of South Africa during the Apartheid era.
 
Siku hizi hata vijijini ni kero. Walokole hawaheshimu watu kabisa, makanisa yao yanakesha na yako kwenye makazi.
 
Back
Top Bottom