Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
SERIKALI imepiga marufuku matangazo na mabango yaliyozagaa barabarani yanayotangaza kuwa tunaongeza nguvu za kiume kwa kuwa yanapotosha jamii na kuharibu watoto nchini. Hayo yalisemwa jana katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika Viwanja vya Benjamini Mkapa Shule ya Uhuru jijini Dar es Salaam.
Serikali imesema matangazo hayo yanapotosha jamii na kuharibu watoto Kwa kuwa watoto wanajikita kwenda huko na kujikuta wanaharibika na kuharibu kizazi tulichokuwa nacho.
Akisoma hotuba hiyo kwa niaba ya Serikali ,Julius Mndolwa alisema kuwa matangazo hayo yanaharibu watoto kwa kuwa watoto wanakwenda kwa waganga hao ili kujaribu na baadae kuharibika kwa kuwa yamekuwa yakiwaletea matatizo kwa kushawishika na ngono muda wote.
Hivyo wenye mabango hayo wanatakiwa wachukue tahadhari mana wanatarajia waanze msako wa kuwasaka wanaohusika na matangazo hayo.
Vilevile amesema kuwa waganga hao huwa hawachagui wateja wa kuwahudmia mana wao nia yao ni pesa hata watoto wadogo wanaofika sehemu hizo huwapa dawa hizo na kuharibu watoto.
Amesema lengo la kuzuia mabango hayo ni kuboresha kizazi cha Tanzania na kupata maadili yaliyo mema ya kutohatarisha maisha ya watoto.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2263474&&Cat=1
Serikali imesema matangazo hayo yanapotosha jamii na kuharibu watoto Kwa kuwa watoto wanajikita kwenda huko na kujikuta wanaharibika na kuharibu kizazi tulichokuwa nacho.
Akisoma hotuba hiyo kwa niaba ya Serikali ,Julius Mndolwa alisema kuwa matangazo hayo yanaharibu watoto kwa kuwa watoto wanakwenda kwa waganga hao ili kujaribu na baadae kuharibika kwa kuwa yamekuwa yakiwaletea matatizo kwa kushawishika na ngono muda wote.
Hivyo wenye mabango hayo wanatakiwa wachukue tahadhari mana wanatarajia waanze msako wa kuwasaka wanaohusika na matangazo hayo.
Vilevile amesema kuwa waganga hao huwa hawachagui wateja wa kuwahudmia mana wao nia yao ni pesa hata watoto wadogo wanaofika sehemu hizo huwapa dawa hizo na kuharibu watoto.
Amesema lengo la kuzuia mabango hayo ni kuboresha kizazi cha Tanzania na kupata maadili yaliyo mema ya kutohatarisha maisha ya watoto.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=2263474&&Cat=1