Mabasi ya wanafunzi ya CRDB yahujumiwa

Mabasi ya wanafunzi ya CRDB yahujumiwa

GeniusBrain

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
4,315
Reaction score
309
CRDB: Kwa sasa hatuwezi kuizungumzia Uda

Na Jimmy Mfuru, 23rd March 2012

Wakati Shirika la Usafiri Dar es salaam (Uda), linasema mradi wa mabasi ya wanafunzi yaliyotolewa na Benki ya CRDB, unajiendesha kwa hasara na kufanya mabasi kusimama kutoa huduma kwa wanafunzi Jijini Dar es salaam, benki hiyo imesema kwa sasa hawawezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa wanalifanyia kazi.Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Kampuni ya Simon Group, Robert Kisena, ambae ni mbia katika Uda, alinukuliwa na NIPASHE kuwa mabasi hayo yanajiendesha kwa hasara na kuishauri benki hiyo ili mabasi hayo yaweze kujiendesha nyakati za mchana yabebe abiria wa kawaida.

Akizungumza na NIPASHE jana jijini Dar es Salaam, Afisa Uhusiano wa CRDB, Nasibu Kalamba, alisema kwa sasa benki hiyo haiwezi kuzungumzia suala hilo kwa kuwa linafanyiwa kazi.

"Kwa sasa Benki haiwezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa bado linafanyiwa kazi," alisema Kalamba.Benki ya CRDB ilitoa mabasi matano mwaka 2010 ambayo yalizinduliwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kwa ajili kusaidia kubeba wanafunzi jijini Dar es Salaam ili kupunguza kero, lakini mabasi hayo kwa sasa yamesimama kwa zaidi ya miezi miwili bila kutoa huduma.CHANZO: NIPASHE
 
huu haukuwa mradi wa kibiashara, ilikuwa ni donation kusaidia wanafunzi wa DSM kwahiyo huo mradi ni liability ya crdb

kisena asitegemee faida kwenye mabasi ya wanafunzi
 
Kwani mapatano ilikuwa mradui ufanye kwa faida au kutoa msaada wka wanafunzi wanaoteseka kwa shida ya usafiri? Huyu Kisena hiyo habari ya hasara anaitioa wapi wakati lengo la CRDB kutoa mabasi na UDA kukubali kuyapokea na kuyaendesha ilikwua ni kusaidia wanafunzi. Kwa nini UDA isikatae tangu mwanzo kwa kigezo kwua itapata hasara?
 
Yaani nilikuwa ninajiuliza haya mabasi mbona siyaoni cku hizi..! Nikahisi yale yale ya Mabasi ya wanafunzi ya wakati uleee.. Mradi ambao uliuliwa na baadhi ya Viongozi wa Chama kimoja cha siasa hapa Tanzania..
 
Hesabu za 150/= zilikuwa hazitoshi
 
Niseme tu kwamba kwa sasa hakuna mradi wowote wa umma unawezafanikiwa Tanzania chini ya Serikali ya CCM! Viongozi wote walafi na hawajali masilahi ya wananchi!
 
Hii nchi kazi tunayo, tunahitaji maombi mazito.
 
Kama hii serekali ya ccm inashindwa kusimamia kamradi kadogo kihivyo hivi tutafika kweli?

Na hii simon group ni mnyama gani serekali inashindwa kuwaajibisha?

Halafu Jk anasema wanamuonea wanasema yeye ni dhaifu.
 
Huu mradi toka mwanzo ulikuwa unaharufu ya hujuma. Hebu tambieni nani aliyewapa ushauri wa kibiashara hawa CRDB wakanunue mabasi aina ya TATA eti ndio yatadumu? Bei yenyewe ilikuwa ni ya kuruka eti basi moja zaidi ya m 100 hi si kweli.

hawa jamaa hawakuwa serius na uwekezaji huu, hata kama ilikuwa ni kuwasaidia wanafunzi lazima uwe mradi ambao ni sustainable au ulikuwa kwaajili ya mtoto fulani kwa hiyo kesha maliza shule na mabasi kwisha kazi yake?

CRDB mnajiaibisha tulitegemea mngeweza hata kuwa washauri wa serikali katika uwekezaji kumbe nanyi hope less. Mbona mabasi ya shule za binafsi yanaoperate kila siku?

Ushauri.

Kama unataka kupunguza nauli ambayo inamfanya mwanafunzi amudu usafiri basi lazima uwe una revolve fund ya kufidia hilo gepu ili biashara hiyo ya kumsaidia mwanafunzi iwe endelevu

Katika faida ya bank kila mwaka kuwe na fungu la kujazia hiyo deficity katika uendeshaji wa mabasi ya wanafunzi

Kuwe na matembezi ya hisani au dinner party za kuchangia usafiri kwa wanafunzi, si tu kwa Dar mnaweza enda hata katika mikoa yenye tatizo kama hilo.

Wazazi wawafaidika katika hiyo business wawe wachangiaji katika sehemu ya uendeshaji si tu katika nauli hata katika michango ya hiari.

Nawakilisha
 
Toka awali CRDB walikuwa wana lengo la kujitangaza na sio kusaidia wanafunzi. Ni nani awezaye kuendesha mabasi kwa nauli za sh 150? Tuwe wakweli!
 
Kunakosekana proposal ya kufanya mradi wa mabasi ya wanafunzi yajiendeshe yenyewe hata uvccm walichemsha nadhani bado hatujapata mchanganuo unaostahiki kutatua tatizo hilo,wengi wana nia ila njia hawana.......
 
Back
Top Bottom