Mabasi yaendayo mikoani kuzidisha abiria; Hivi mnasubiri mpaka ajali itokee watu wafariki ndio mchukue hatua?

Mabasi yaendayo mikoani kuzidisha abiria; Hivi mnasubiri mpaka ajali itokee watu wafariki ndio mchukue hatua?

Mbalamwezi1

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2013
Posts
2,073
Reaction score
2,026
Kwenu wenye mamlaka, naandika ujumbe huu nikiwa ndani ya Basi la Saibaba kutoka Arusha kwenda Dar, basi hili ni la safari ndefu lakini linasimamisha abiria kama Daladala.

Hili ni Moja nililoshuhudia Mimi ila mabasi mengi yale yanayopaki stendi kuu ya Arusha yanafanya hivi, cha kushangaza hili basi limesimamishwa trafiki mwanamke hapa Makao Makuu ya Polisi (W) Arumeru na ameona kabisa basi Lina abiria wamesimama lakini hakuchukua hatua yoyote zaidi ya konda kushuka na kutia tu stori mbili tatu Kisha hao tukaondoka huku nikiweweseka kiwendawaImu.

Hii ni hatari kwa kwa kuwa ikitokea ajali hawa waliosimama kwenye korido ndio watakuwa wa kwanza kudhurika kwa kuwa hawana sehemu maalum za kishikililia.

Tusisubiri mpaka ajali itokee Kisha tuseme basi lilikuwa limebeba abiria zaidi ya uwezo wake!

Tafadhali askari wa barabarani tekelezeni wajibu wenu.

Pia soma KERO - Mabasi ya Abood (Dar - Moro -Dar) yanajaza abiria kupitiliza kama Daladala za Mbagala, hii si sawa
 
1717695211678.jpg
 
Hao abiria wanapakiwa na kusimamishwa hawana akili

Ova
 
Hiyo ndio changamoto ya kupanda mabasi ya gharama nafuu pasipo kufahamu kuwa nafuu ni gharama
 
Kwenu wenye mamlaka, naandika ujumbe huu nikiwa ndani ya Basi la Saibaba kutoka Ars kwenda Dar, basi hili ni la safari ndefu lakini linasimamisha abiria kama Daladala. Hili ni Moja nililoshuhudia Mimi ila mabasi mengi Yale yanayopaki stendi kuu ya Arusha yanafanya hivi, cha kushangaza hili basi limesimamishwa trafiki mwanamke hapa Makao Makuu ya Polisi (W) Arumeru na ameona kabisa basi Lina abiria wamesimama lakini hakuchukua hatua yoyote zaidi ya konda kushuka na kutia tu stori mbili tatu Kisha hao tukaondoka huku nikiweweseka kiwendawaImu.

Hii ni hatari kwa kwa kuwa ikitokea ajali Hawa waliosimama kwenye korido ndio watakuwa wa kwanza kudhurika kwa kuwa Hawana sehemu maalum za kishikililia. Tusisubiri mpaka AJALI itokee Kisha tuseme basi lilikuwa limebeba abiria zaidi ya uwezo wake! Tafadhali askari wa barabarani tekelezeni wajibu wenu.
Ulitakiwa uwapigie simu trafiki namba zimo ndani ya basi, trafiki huwa wanatangaza kubusu hilo ila nyie mnafuatilia sana uchambuzi wa Simba na Yanga muda wote.
 
Back
Top Bottom