Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Serikali ya Tanzania kwa sasa inaendeshwa na CCM. Kwa ivo kila jambo linalotendwa na serikali hapa nchini ni lazima iwe ni matokeo ya maelekezo ya CCM.
Hivi karibuni Serikali ya Marekani chini ya uongozi wa Donald Trump imezuia misaada Kwa nchi mbali mbali duniani kupitia shirika lake la misaada ulimwenguni la USAID.
Tanzania ni nchi mojawapo iliyoathirika na zuio hilo la Marekani. Tukio hilo limenifanya nitafakari kuhusu hoja ya mabeberu na siasa za Tanzania.
CCM huwa inaahidi kufanya mambo mbalimbali wakati wa Kampeni, kumbe 70% ya ahadi zinazotolewa na CCM wakati wa Kampeni huwa zinategemea misaada toka nchi za nje hasa zile wanazoziita za mabeberu.
Miradi mingi ya Kilimo, Elimu na Afya Kwa asilimia kubwa inategemea misaada ya mabeberu.
Kwa maana nyingine mabeberu huwasaidia CCM kuendesha nchi wakati huo huo CCM husema CHADEMA ndiyo rafiki wa hao mabeberu.
Bila mabeberu CCM itashindwa kuendesha nchi.
Hivi karibuni Serikali ya Marekani chini ya uongozi wa Donald Trump imezuia misaada Kwa nchi mbali mbali duniani kupitia shirika lake la misaada ulimwenguni la USAID.
Tanzania ni nchi mojawapo iliyoathirika na zuio hilo la Marekani. Tukio hilo limenifanya nitafakari kuhusu hoja ya mabeberu na siasa za Tanzania.
CCM huwa inaahidi kufanya mambo mbalimbali wakati wa Kampeni, kumbe 70% ya ahadi zinazotolewa na CCM wakati wa Kampeni huwa zinategemea misaada toka nchi za nje hasa zile wanazoziita za mabeberu.
Miradi mingi ya Kilimo, Elimu na Afya Kwa asilimia kubwa inategemea misaada ya mabeberu.
Kwa maana nyingine mabeberu huwasaidia CCM kuendesha nchi wakati huo huo CCM husema CHADEMA ndiyo rafiki wa hao mabeberu.
Bila mabeberu CCM itashindwa kuendesha nchi.