Mabeberu yameanza kushikwa sharubu?

Mabeberu yameanza kushikwa sharubu?

technically

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2016
Posts
12,706
Reaction score
52,355
Naona toka ile speach ya Mama ya kuwakemea watu wanaohoji watu kutekwa na kupotea pia kuwakemea kwamba wasitupangie Cha kufanya.

Sasa naona mabeberu yameongeza maradufu kuimulika Tanzania.

Kama mnakumbuka kipindi cha Magufuli walizusha na kuonyesha kwamba meli ya Korea kasikazini ilikuwa na bendera ya Tanzania maana yake ilikuwa imesajiliwa kufanya kazi Tanzania.

Chokochoko zimeanza tena baada ya speech Ile ya Rais wetu sasa mabeberu na vyombo vya habari vya magharibi vinahoji na kuhisi Tanzania imechukua mlengo wa siasa za mashariki.

Yaani china, urusi, na mashariki ya Kati!

Sipika wa bunge pia kashambuliwa kwenda urusi wakati ni nchi iliyowekewa vikwazo na nchi za magharibi.!!

Kinacholeta hatari ni kwamba Kuna Watanzania wanatumika na nchi za magharibi ili kuamua mlengo wa siasa za Tanzania.

Kibaya zaidi tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwakani je hawawezi kuweka mkono wao?

Kwanini tunachagua upande wa kuwa kwenye vita wakati tunajua kabisa ni ngumu kuwasaporti mahasimu wa magharibi na tukabaki salama?

Bandari tumewapa ngorongoro tumewapa na bado tunakuwa kwenye mlengo wao upande wa vita sizani Kama ni sahihi.

Tanzania ni nchi isiyofungamana na upande wowote tuendelee kuwa hivyo lakini tusijionyeshe Sana kwamba tupo upande Fulani itatugharimu pakubwa natoa angalizo vita hii inayoendelea ulaya na mashariki ya Kati sio ya kuingilia waacheni hao mabwana watamalizana wenyewe kwa wenyewe pia tunapotoa speech zetu hasa Viongozi wa juu lazima waelewe madhara ya speech zao dunia ni Kijiji Magufuli tulimwambia akashupaza shingo kilichofuata ni historia.

Idara za usalama lazima zibaki kwenye misimamo na misingi ya Taifa letu ya kutofungamana na upande wowote hivyo Kila tawala inapokuja iambiwe na ielewe hayo.

Marekani uchangia dollar 2.5 billion wastani wa trioni 6 kila mwaka wa bajeti je, China, Urusi na Waarabu kwa pamoja wanachangia kiasi gani?

Ukitaka kutawala nchi vizuri hakikisha unaunganisha watu wako hata ukitaka faminia yako inatulia weka chakula mezani hauwezi kushindwa kusimamia familia ukaanza kumsingizia jirani au ndugu yako.

Dhibiti utekaji, tengeneza katiba bora, tengeneza Sheria nzuri weka uchaguzi huru.

Magharibi utumia dosari zako kukuingilia.

Asalaam alykum!
 
Naona toka ile speach ya Mama ya kuwakemea watu wanaohoji watu kutekwa na kupotea pia kuwakemea kwamba wasitupangie Cha kufanya .

Sasa naona mabeberu yameongeza maradufu kuimulika Tanzania.

Kama mnakumbuka kipindi Cha Magufuli walizusha na kuonyesha kwamba meli ya Korea kasikazini ilikuwa na bendera ya Tanzania maana yake ilikuwa imesajiliwa kufanya kazi Tanzania..

Chokochoko zimeanza tena baada ya speech Ile ya Rais wetu sasa mabeberu na vyombo vya habari vya magharibi vinahoji na kuhisi Tanzania imechukua mlengo wa siasa za mashariki .

Yaani china, urusi, na mashariki ya Kati!!

Sipika wa bunge pia kashambuliwa kwenda urusi wakati ni nchi iliyowekewa vikwazo na nchi za magharibi.!!

Kinacholeta hatari ni kwamba Kuna Watanzania wanatumika na nchi za magharibi ili kuamua mlengo wa siasa za Tanzania .

Kibaya zaidi tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu mwakani je hawawezi kuweka mkono wao?

Kwanini tunachagua upande wa kuwa kwenye vita wakati tunajua kabisa ni ngumu kuwasaporti mahasimu wa magharibi na tukabaki salama?

Bandari tumewapa ngorongoro tumewapa na bado tunakuwa kwenye mlengo wao upande wa vita sizani Kama ni sahihi.

Tanzania ni nchi isiyofungamana na upande wowote tuendelee kuwa hivyo lakini tusijionyeshe Sana kwamba tupo upande Fulani itatugharimu pakubwa natoa angalizo vita hii inayoendelea ulaya na mashariki ya Kati sio ya kuingilia waacheni hao mabwana watamalizana wenyewe kwa wenyewe pia tunapotoa speech zetu hasa Viongozi wa juu lazima waelewe madhara ya speech zao dunia ni Kijiji Magufuli tulimwambia akashupaza shingo kilichofuata ni historia.

Idara za usalama lazima zibaki kwenye misimamo na misingi ya Taifa letu ya kutofungamana na upande wowote hivyo Kila tawala inapokuja iambiwe na ielewe hayo .

Marekani uchangia dollar 2.5 billion wastani wa trioni 6 Kila mwaka wa bajeti je china, urusi na waarabu kwa pamoja wanachangia kiasi gani?

Ukitaka kutawala nchi vizuri hakikisha unaunganisha watu wako hata ukitaka faminia yako inatulia weka chakula mezani hauwezi kushindwa kusimamia familia ukaanza kumsingizia jirani au ndugu yako.

Dhibiti utekaji, tengeneza katiba bora, tengeneza Sheria nzuri weka uchaguzi huru.

Magharibi utumia dosari zako kukuingilia.

Asalaam alykum!!
Akili yako bwana.
Pale ameulizwa kwa kuwa ni spika wa bunge la dunia sio kama spika wa bunge la jamhuri yetu.

Angekuwa si spika wao hata sidhani kuna ambaye angemuuliza
 
Back
Top Bottom