Mabegi ya mgongoni kwa watoto wa shule ni hatari kwa afya!

heavy school bag,huku kwetu tudaftari tuwili twa muandiko na hesabu na chupa ya maji huo uheavy utatoka wapi?
 
Wanafuzi wabebe ile mifuko ya shule maarafu kwa jina la 'Sport' au ile mingine inaitwa "my clear bag".
 
Nchi hii ina kaulimbiu ya hapa kazi tu
Hivyo, haya hawa vining'ina na vilembwe wanatakiwa wapige mzigo tu
Hapa kazi tuuuuuu
 
Duuh! Ila kwa sasa hasa hawa wa International School haizuiliki mtoto kutokuwa na begi kubwa sababu humo ndani wanabeba daftari za Class work labda tuseme sita na za Home Work nazo sita na hapo daftari zote ni zile za page 200 bila kusahau vitabu navyo hapo, maji ya kunywa sijui juice haijawekwa hapo yaani ni lazima mzigo uwe mkubwa.

Na ni ngumu kusema labda baadhi ya daftari ziachwe nyumbani au vitabu sababu vyote vinatumika.

Hiyo iliwezekana zamani tena kwa wale tuliosoma Kayumba.
 
Khaaa,, kwa kweli huu ni mwisho wa mfumo, mbona kipindi chetu huko nyuma hatukua na haya mambo na madaftari na wengine tulibeba na chakula?
 
If possible labda walimu wafanye kazi ya kuwapa watoto ratiba za masomo zije kwa wazazi kwamba wawe na kazi ya kuchambua masomo ya siku fulani na kuandaa hizo daftari na vitabu. Japo bado ni ngumu mnooo sababu kuna ile mwalimu fulani hayupo basi mungine anatumia mwanya ule kufundisha watoto kwa somo lingine ambalo halipo kwenye ratiba.

Pia ni ngumu wazazi kuwa na huo muda wa kubadilisha madaftari ya mtoto kila siku sababu wazazi wengi huwa wako busy kuliko kawaida.
 
Khaaa,, kwa kweli huu ni mwisho wa mfumo, mbona kipindi chetu huko nyuma hatukua na haya mambo na madaftari na wengine tulibeba na chakula?
Nadhani ni ile ya kwamba tulikuwa tunatumia daftari moja kuandikia darasani na hilo hilo kufanyia kazi za nyumbani. Pia ilikuwa vitabu hatununuliwi tunategemea vya shule yaani kama kuna maswali basi mwalimu agawe vitabu kwa makundi tukae duara tusome maswali kisha tuandike. Au aandike maswali ubaoni tucopy.
 
Kuna kadogoo kamoja huwa kanakujaga kusubiri school bus hapa stend, ukimuona akiwa na begi lake unaweza ukacheka. Ana kamwili kadogo halafu ni kafupi,begi ni kubwa kiasi kwamba linamgotea mapajani na akitembea lazima apinde mgongo kwa mbele ili akabiliane na uzito wa begi unaomvuta nyuma. Mungu awanusuru na balaa hili kwa kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…