Leoa asubuhi katika pitapita zangu nimeingia kama Beki mbili tofauti lakini cha kushangaza hakuna watu kabisa kama ilivyozoeleka kama zamani ambao mtu unaweza kukaa kwenye foleni hata masaa matatu. Nilipofika Accessbank kuuliza kulikoni kwa sababu watu walijaa sana wakanieleza kuwa gharama zao ni nafuu sana na hata ukiweka fedha zako kwa muda maalum wanatoa faida kwa kiwango kikubwa. Mfano:- ukiweka Tshs.50,000,000 kwa siku 30 unapewa faida ya 13.9%, miezi miwili 14.2%, miezi mitatu 14.5%, Miezi sita 14.8%, Miezi tisa 15.1%, Mwaka 15.4%. Hii ni tofauti kabisa na faida wanayotoa Benki zingine kama NMB au CRDB. Nilipouliza hii ni Benki ya wapi wakanieleza ni ya Kijerumani na ni Benki poa sana. Ninazishauri Benki zingine zibadilike vinginevyo watakuja kukimbiwa na wateja wao kama watakapokuja kufahamu AccessBank.