Mabere Marando na utetezi wa Manji

Mabere Marando na utetezi wa Manji

BIN BOR

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2010
Posts
1,013
Reaction score
407
Huyu Manji ni fisadi na wengi tunajua hilo. Huyu Manji anatetewa na Mabere Marando aliye mwanasheria wa CDM. Chadema inakemea ufisadi. Sasa uadilifu wa Mabere uko wapi, au pesa mbele maadili nyuma? Naamini Dr. Slaa ataisoma hii. Tusifumbiane macho pale tunapokwenda vibaya.
 
Marando yupi?? Yupo marando mwanasheria na marando mwanasiasa. hata kama ni yuleyule lakini ni watu wawili tofauti.
 
Marando yupi?? Yupo marando mwanasheria na marando mwanasiasa. hata kama ni yuleyule lakini ni watu wawili tofauti.

Kikwete rais na Kikwete mkwere ni watu wawili tofauti? Ndio maana nikasema uadilifu nyuma, pesa mbele......
 
Mara ya kwanza nilishangaa. lakini cha kuelewa ni kwamba Mengi katika matangazo aliyoyatoa kupitia ITV alimwita manji fisadi papa na alipokwenda mahakamani wakili wa Mengi ( Michael Ngalo ) akawasilisha nyaraka za makampuni ya manji yaliyokwapua fedha kutoka Kagoda .Manji akitumia kampuni yake ya Quality Finance.

Sasa sheria ya makampuni inamtambua mmiliki wa biashara na kampuni yake kama watu wawili tofauti.hivyo basi Mengi kumwita manji fisadi papa halafu akaenda mahakamani kutumia nyaraka za kampuni ya manji kuna walakini kisheria.Hivyo Marando anamtetea manji kama personal na sio makampuni yake yaliyofanya ufisadi.
 
Hili jambo limekuwa likinisumbua kwa muda mrefu sana.... I am starting to suspect hii opposition tuliyo nayo kusema kweli. Tusikute ni kukosekana kwa opportunities upande mwingine ndo watu wakahamia upinzani, huku mioyo yao bado haijabadilika.
Leo hii, Mabere Marando ndo anaongoza kukataa nyaraka eti lazima ziwe zimethibitishwa na ofisi husika.... This is very wrong especially as ni mtu wa upinzani na wakati wa kampeni alijionyesha yeye ni hodari wa kuwataja mafisadi hadharani...
 
Marando yuko kazini na ana familia inayomtegemea kupata mlo.Sasa sidhani yeye ingekuwa rahisi kuacha tenda ya kazi ambayo kasomea miaka yote hio kisa mambo ya siasa.

Kama wakina Mengi wana ushahidi wa kutosha watashinda kesi kama hawana inamana wameshindwa kesi na Marando katimiza wajibu wake kama wakili na atakuwa kalipwa hela halali za kazi aliofanya.
 
Marando yuko kazini na ana familia inayomtegemea kupata mlo.Sasa sidhani yeye ingekuwa rahisi kuacha tenda ya kazi ambayo kasomea miaka yote hio kisa mambo ya siasa.

Kama wakina Mengi wana ushahidi wa kutosha watashinda kesi kama hawana inamana wameshindwa kesi na Marando katimiza wajibu wake kama wakili na atakuwa kalipwa hela halali za kazi aliofanya.

Kwa hiyo kama ni kuendekeza njaa basi Rostam akiwa na kesi Marando anaweza kumtetea?
 
Marando yuko kazini na ana familia inayomtegemea kupata mlo.Sasa sidhani yeye ingekuwa rahisi kuacha tenda ya kazi ambayo kasomea miaka yote hio kisa mambo ya siasa.

Kama wakina Mengi wana ushahidi wa kutosha watashinda kesi kama hawana inamana wameshindwa kesi na Marando katimiza wajibu wake kama wakili na atakuwa kalipwa hela halali za kazi aliofanya.

Kwa hiyo kesho si ajabu ukasikia Marando mwanasheria wa CCM, eti kwa sababu ana familia. Obama ni mwanasheria na kampuni yake haitoi utetezi kwa shauri lolote lenye maslahi ya kuwajenga republicans na hata wao hawa-consult kampuni hiyo kwa sababu hizo hizo. Kwa maneno mengine unataka kusema hata katika Chadema Marando alifuata mshahara na si itikadi. Na alikuwa mgombea wa uspika. Sina chuki na Marando lakini hapa kuna suala uadilifu na kama ningeandika kichwa cha habari ningesema kiongozi wa CDM atetea fisadi wa CCM. Kama ni familia, hata Nyerere alikuwa nayo wakati anaacha ualimu na kufanya siasa. CHADEMA INAPAMBANA NA MAFISADI NA SIO KUWAPAMBA.
 
Mkuu, hiyo ndio hypocrisy ya baadhi ya wanasiasa wasiosimamia morals wanazoziamini... binafsi nafahamu kila lawyer ana moral conducts zake na mabere kwa kuwa chadema na kutetea manji ni contradictory

he needs to uphold CDM standards by not represent Manji
 
Kwa hiyo kesho si ajabu ukasikia Marando mwanasheria wa CCM, eti kwa sababu ana familia. Obama ni mwanasheria na kampuni yake haitoi utetezi kwa shauri lolote lenye maslahi ya kuwajenga republicans na hata wao hawa-consult kampuni hiyo kwa sababu hizo hizo. Kwa maneno mengine unataka kusema hata katika Chadema Marando alifuata mshahara na si itikadi. Na alikuwa mgombea wa uspika. Sina chuki na Marando lakini hapa kuna suala uadilifu na kama ningeandika kichwa cha habari ningesema kiongozi wa CDM atetea fisadi wa CCM. Kama ni familia, hata Nyerere alikuwa nayo wakati anaacha ualimu na kufanya siasa. CHADEMA INAPAMBANA NA MAFISADI NA SIO KUWAPAMBA.


Kwahio Marando angekuwa daktari na Manji anaumwa mngemlaumu kumtibu Manji kwa vile atalipwa kwa hela za ufisadi?


Kama Mengi ana ushahidi wa kutosha atashinda haijalishi nani anamtetea Manji.


Mbona nyie bado mnatumia mtandao wa vodacom? hamjui kama mnawalisha mafisadi? sasa kwanini yeye asifanye kazi yake?
 
Kwahio Marando angekuwa daktari na Manji anaumwa mngemlaumu kumtibu Manji kwa vile atalipwa kwa hela za ufisadi?


Kama Mengi ana ushahidi wa kutosha atashinda haijalishi nani anamtetea Manji.


Mbona nyie bado mnatumia mtandao wa vodacom? hamjui kama mnawalisha mafisadi? sasa kwanini yeye asifanye kazi yake?

Marando alichofanya ni wrong. Kubali kataa. Chadema wanabidi wawe makini la sio watakuwa hawana credibility wakiimba wimbo wa ufisadi.
Imagine angeshinda uspika? Speaker Marando amtetea Manji. No way!!
 
Kwa hiyo kama ni kuendekeza njaa basi Rostam akiwa na kesi Marando anaweza kumtetea?


Tatizo tumekaa tunapoteza mda kuwaita mafisadi bila kuchukua hatua yoyote.Mafisadi wanaendelea na maisha yao bila wasi wasi. Wenye ushahidi wanaweza kuwapeleka mahakamani hatuwezi kuendelea miaka nenda tunapiga kelele na kusimamisha maisha ya watu wengine kisa hao mafisadi.

Hawa mafisadi wote ni wafanya biashara kwanini sisi wananchi tusigomee biashara zao kama tunamsimamo lakini tuko tayari kumyooshea kidole MARANDO kwa kufanya kazi yake ya uwakili hili apate pato?


Au huoni kwa sisi wananchi kuendelea kununua bidhaa za mtu yoyote anayetuhumiwa kwa ufisadi ni kuendelea kuwatajirisha?
 
Kwahio Marando angekuwa daktari na Manji anaumwa mngemlaumu kumtibu Manji kwa vile atalipwa kwa hela za ufisadi?


Kama Mengi ana ushahidi wa kutosha atashinda haijalishi nani anamtetea Manji.


Mbona nyie bado mnatumia mtandao wa vodacom? hamjui kama mnawalisha mafisadi? sasa kwanini yeye asifanye kazi yake?

Itawezekanaje kwa daktari bingwa wa macho kupasua moyo? Tafuta mfano mwingine.
 
Tatizo tumekaa tunapoteza mda kuwaita mafisadi bila kuchukua hatua yoyote.Mafisadi wanaendelea na maisha yao bila wasi wasi. Wenye ushahidi wanaweza kuwapeleka mahakamani hatuwezi kuendelea miaka nenda tunapiga kelele na kusimamisha maisha ya watu wengine kisa hao mafisadi.

Hawa mafisadi wote ni wafanya biashara kwanini sisi wananchi tusigomee biashara zao kama tunamsimamo lakini tuko tayari kumyooshea kidole MARANDO kwa kufanya kazi yake ya uwakili hili apate pato?


Au huoni kwa sisi wananchi kuendelea kununua bidhaa za mtu yoyote anayetuhumiwa kwa ufisadi ni kuendelea kuwatajirisha?

Kwa hiyo unaanza ku-justfy ule usemi....if you can't fight them, join them???
Marando amechemsa na ni ameshaanza kuwa a big liability for Chadema. Marando ni kansa na soon ataiangamiza Chadema for his selfishness. Kubali kataa lakini huo ndio ukweli
 
Marando alichofanya ni wrong. Kubali kataa. Chadema wanabidi wawe makini la sio watakuwa hawana credibility wakiimba wimbo wa ufisadi.
Imagine angeshinda uspika? Speaker Marando amtetea Manji. No way!!

Na sisi wananchi pia tuna makosa kuendelea kutumia/kununua bidhaa za hawa mafisadi , tuache kuwategemea wanasiasa tu kwenye kila kitu na sisi pia tunaitaji kuchangia pale inapowezekana.


Marando wakili na hio ndio kesi ilimfuata. Kwanini mengi hakumuajili Marando hili wamshitaki Manji kama alikuwa na ushahidi wote?

Kazi ya uakili unaweza kuwa kwenye upande wowote utaokufuata mwanzo kwa vile ndio njia yako uliochagua ya kukuingizia kipato.
 
Nipe sababu za msingi na uthibitisho unaoonyesha kwamba manji ni fisadi au na wewe umesikia tu kwa watu!subiri kesi iishe mahakamani iwapo mahakama itathibitisha kuwa manji ni fisadi ndipo utoe hizo lawama kwa marando!!mimi naona hapo umechanganya siasa na kazi halisi ya mtu malando akiwa kama mwananchi wa kawaida watoto wake wanahitaji kuvaa,kula na elimu so sioni sababu ya wewe kumzuia kufanya kazi kwa kuwa unakua kama umeshamhukumu manji kama fisadi kitu ambacho si kweli kesi bado haijaisha!
Huyu Manji ni fisadi na wengi tunajua hilo. Huyu Manji anatetewa na Mabere Marando aliye mwanasheria wa CDM. Chadema inakemea ufisadi. Sasa uadilifu wa Mabere uko wapi, au pesa mbele maadili nyuma? Naamini Dr. Slaa ataisoma hii. Tusifumbiane macho pale tunapokwenda vibaya.
 
Nipe sababu za msingi na uthibitisho unaoonyesha kwamba manji ni fisadi au na wewe umesikia tu kwa watu!subiri kesi iishe mahakamani iwapo mahakama itathibitisha kuwa manji ni fisadi ndipo utoe hizo lawama kwa marando!!mimi naona hapo umechanganya siasa na kazi halisi ya mtu malando akiwa kama mwananchi wa kawaida watoto wake wanahitaji kuvaa,kula na elimu so sioni sababu ya wewe kumzuia kufanya kazi kwa kuwa unakua kama umeshamhukumu manji kama fisadi kitu ambacho si kweli kesi bado haijaisha!

Kwa hiyo kama ana njaa ya kulisha familia yake ni haki kumtetea Rostam akiwa na kesi tena ya ufisadi?
 
Na sisi wananchi pia tuna makosa kuendelea kutumia/kununua bidhaa za hawa mafisadi , tuache kuwategemea wanasiasa tu kwenye kila kitu na sisi pia tunaitaji kuchangia pale inapowezekana.


Marando wakili na hio ndio kesi ilimfuata. Kwanini mengi hakumuajili Marando hili wamshitaki Manji kama alikuwa na ushahidi wote?

Kazi ya uakili unaweza kuwa kwenye upande wowote utaokufuata mwanzo kwa vile ndio njia yako uliochagua ya kukuingizia kipato.

Kwa hiyo kesi ya Mramba na Yona ikimfuata aichukue kwa sababu ya kuingiza kipato?
 
Itawezekanaje kwa daktari bingwa wa macho kupasua moyo? Tafuta mfano mwingine.

Kivipi sasa? mfano wangu umelenga ajira kwamba mtu hutakiwi kuchagua unayemuhudumia.

Kesi hii ni MANJI VS MENGI na sio MANJI VS CHADEMA, kama ingekuwa MANJI VS CHADEMA hapo ndio tungemshangaa Marando kwa kuendana kinyume na chama chake. Nyinyi mmeichukulia kesi kisiasa na ndio maaana mnamshangaa MARANDO lakini hii kesi ni ya watu binafasi wawili na imetokea kwamba upande mmoja umemuajili MARANDO kuwa wakili wake.
 
Kivipi sasa? mfano wangu umelenga ajira kwamba mtu hutakiwi kuchagua unayemuhudumia.

Kesi hii ni MANJI VS MENGI na sio MANJI VS CHADEMA, kama ingekuwa MANJI VS CHADEMA hapo ndio tungemshangaa Marando kwa kuendana kinyume na chama chake. Nyinyi mmeichukulia kesi kisiasa na ndio maaana mnamshangaa MARANDO lakini hii kesi ni ya watu binafasi wawili na imetokea kwamba upande mmoja umemuajili MARANDO kuwa wakili wake.

Kwa hiyo ikija kesi ya ROSTAM v/s SLAA Marando achukue kesi?
 
Back
Top Bottom