VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,137
- 17,908
Usiri wa watuhumiwa wa mabomu ya Arusha unatisha sasa. Watu wamekufa Olasiti na Soweto. Watu wamejeruhiwa. Watu waliteseka na kulia mno juu ya jambo hili. Wapo walioachwa wakiwa juu ya kadhia hii.Na watoto yatima. Na kadhalika na kadhalika. Siri ya nini tena katika kadhia hii ya Arusha? Wananchi wote wa Tanzania wanaisubiri Serikali yao ifanye jambo la faraja na la kisheria juu ya milipuko ile ya Arusha. Si wakati wa sinema za mtu kutoka nje na kusema halafu ajibanze tena ndani.
Jeshi letu la Polisi liliunda Tume ya uchunguzi.Bado hatujaisikia imegunduaje. Yawezekana waliokamatwa sasa ni matokeo ya uchunguzi huo. Hatuna hakika. CHADEMA walidai kuwa na mkanda wa video wa kadhia ya Soweto.Wamegoma kuutoa hadi leo.Mkanda umekuwa siri. Polisi wamelazimisha kuupata mkanda huo wa CHADEMA bila mafanikio. Sehemu hiyo ya sinema ikaisha.
Sasa, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mulongo anasema kuwa 'walioingiza mabomu na kulipua Arusha' wamepatikana.Yaani wametiwa nguvuni. Mulongo anasema kuwa bado wanahojiwa na Polisi kupata taarifa zaidi zizungukazo suala hili kwa ujumla wake.Haiko wazi walikamatwa lini. Hata kama ni washukiwa wa uhalifu wa aina gani,bado wana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda unaotambuliwa na sheria za nchi. Ni saa 24 tangu kukamatwa kwao.Lakini tayari tumeshajua kuwa mabomu husika yalitoka katika nchi ya Balozi-wa-Chama yaani China. Hapa pia usiri umetanda.
Mkuu wa Mkoa analiongelea jambo hili kama nani hasa? Anahusikaje nalo kiutendaji? Kweli hakuna watendaji wahusika wa suala hili? Kuwatangaza waliokamatwa si nafasi ya kujipatia sifa. Ni jambo serious tukizingatia madhila waliyoyapata watu wa Arusha kule Olasiti na Soweto.
Wahusika wa Jeshi la Polisi wajitokeze sasa na waweke wazi nini hasa kinaendelea juu ya jambo hili.Usiri utatupa wasiwasi.Utatupunguza imani. Tutaichukulia kesi itakayofuata kama ni mchezo uliopangwa na kupangika. Halitakuwa jambo jema.Hatutaki iwe hivyo. Wahusika jitokezeni na mtueleze.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Jeshi letu la Polisi liliunda Tume ya uchunguzi.Bado hatujaisikia imegunduaje. Yawezekana waliokamatwa sasa ni matokeo ya uchunguzi huo. Hatuna hakika. CHADEMA walidai kuwa na mkanda wa video wa kadhia ya Soweto.Wamegoma kuutoa hadi leo.Mkanda umekuwa siri. Polisi wamelazimisha kuupata mkanda huo wa CHADEMA bila mafanikio. Sehemu hiyo ya sinema ikaisha.
Sasa, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mulongo anasema kuwa 'walioingiza mabomu na kulipua Arusha' wamepatikana.Yaani wametiwa nguvuni. Mulongo anasema kuwa bado wanahojiwa na Polisi kupata taarifa zaidi zizungukazo suala hili kwa ujumla wake.Haiko wazi walikamatwa lini. Hata kama ni washukiwa wa uhalifu wa aina gani,bado wana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda unaotambuliwa na sheria za nchi. Ni saa 24 tangu kukamatwa kwao.Lakini tayari tumeshajua kuwa mabomu husika yalitoka katika nchi ya Balozi-wa-Chama yaani China. Hapa pia usiri umetanda.
Mkuu wa Mkoa analiongelea jambo hili kama nani hasa? Anahusikaje nalo kiutendaji? Kweli hakuna watendaji wahusika wa suala hili? Kuwatangaza waliokamatwa si nafasi ya kujipatia sifa. Ni jambo serious tukizingatia madhila waliyoyapata watu wa Arusha kule Olasiti na Soweto.
Wahusika wa Jeshi la Polisi wajitokeze sasa na waweke wazi nini hasa kinaendelea juu ya jambo hili.Usiri utatupa wasiwasi.Utatupunguza imani. Tutaichukulia kesi itakayofuata kama ni mchezo uliopangwa na kupangika. Halitakuwa jambo jema.Hatutaki iwe hivyo. Wahusika jitokezeni na mtueleze.
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam