Machache kuhusu babu yangu, Salum Abdallah

Machache kuhusu babu yangu, Salum Abdallah

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MACHACHE KUHUSU BABU YANGU SALUM ABDALLAH

Hiyo picha ya Loco Shed Tabora hapo chini ndipo akifanya kazi babu yangu Salum Abdallah maarufu Baba Popo kuanzia 1947 had 1964.
Alihamia Tabora kutoka Dar es Salaam baada ya Loco Shed kuhamishwa kutoka Dar es Salaam mwaka huo wa 1947.

1955 yeye na Kassanga Tumbo walianzisha chama Tanganyika Railway African Union (TRAU).
Salum Abdallah akiwa President na Kassanga Tumbo Secretary.

TRAU ina historia kubwa sana katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

TRAU ilifanya mgomo mwaka wa 1960 uliodumu siku 82.
Salum Abdallah aliongoza mgomo huo wa wafanyakazi wa Railway uliodumu miezi mitatu.

Kwa miezi mitatu treni na mabasi ya Railway yalisimama hadi Waingereza waliposalimu amri na kuwaita viongozi wa wafanyakazi katika meza ya majadiliano.

Uhuru ulipopatikana babu yangu akapambana kwa fikra na msimamo wa Nyerere kuhusu vyama vya wafanyakazi Nyerere akitaka viwekwe chini ya TANU na viongozi wa vyama vya wafanyakazi pamoja na babu yangu wakipinga wazo hilo.

Yalipotokea maasi ya wanajeshi tarehe 20 Januari 1964 baada ya maasi kuzimwa na jeshi la Waingereza, Nyerere aliwakamata viongozi wote wa vyama vya wafanyakazi na kuwaweka kizuizini.

Babu yangu alifungwa kwenye jela ya Uyui, Tabora na alipotoka kizuizini Tanganyika Railway African Union (TRAU) chama alichokiasisi mwaka wa 1955 kilikuwa kimepigwa marufuku pamoja na vyama vingine vya wafanyakazi na badala yake kimeundwa chama cha National Union of Tanganyika Workers (NUTA) kwa juhudi kubwa za Rashid Kawawa na Michael Kamaliza.

Babu yangu alihama Tabora na kwenda Urambo kupisha shari kwani zilienezwa taarifa za uongo kuwa yeye alikuwa katika kundi pamoja na Victor Mkello (kiongozi wa wafanyakazi wa mashamba ya mkonge) na Kassanga Tumbo walikuwa wamekula njama ya kupindua serikali na kumuua Rais Nyerere.

Babu yangu akajikita katika ukulima wa tumbaku Urambo huku akiendelea na ukulima wake wa miaka yote Kakola na Uyui Tabora.
Fredrick Mchauru aliendelea na utumishi katika serikali ya kikoloni na uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961 alishika nyadhifa mbalimbali katika serikali huru kama zilizvyoelezwa katika makala zilizochapwa na Raia Mwema.

Kama mimi nisingeaandika kitabu cha Abdul Sykes huenda historia hii ya babu yangu na wazalendo wengine isingejulikana na historia ambazo zingesomwa ndiyo hizi za watu kama Fredrick Mchauru na wengineo.

Salum Abdallah alifariki mwaka wa 1974 akiwa na umri kama miaka 80 akiwa mkimya sana kwa kuwa hapakuwa tena pale mjini na barza zilizokuwa zikijadili siasa kama miaka ya 1950 wakati wa kudai uhuru.

Siasa ilikuwa sasa jambo la kutisha watu wakihofu kukamatwa na kuwekwa gerezani.

Babu yangu akiungulia ndani kwa ndani kwa chuki dhidi ya TANU chama alichokiendea mbio na kuhudhuria mikutano yake yote ya siri mwaka wa 1953 pamoja na wazee wenzake akina Maulidi na Abdallah Kivuruga, Rajab Saleh Tambwe, Abubakar Mwilima kuwataja wachache, na kuwa mmoja wa waasisi wake mjini Tabora mwaka wa 1955.

Siku zote yeye baada ya kuona vyama vya wafanyakazi vimekwa chini ya TANU na serikali yake aliwaona viongozi wapya wa vyama hivi vibaraka wa serikali hawataweza kupigania haki za wafanyakazi kwa dhati.





Picha: Kulia ni Christopher Kassanga Tumbo anaefuata ni Salum Abdallah.
 
Kipindi cha miaka hiyo watu wengi walisekwa rumande na serikali. Hali hiyo na mambo mengine chungu nzima ilipelekea hata mimi babu yangu pia kuhama mkoa na kwenda mikoa ya kaskazini kuanza maisha mapya na hatimaye kusahau yaliyopita.
 
MACHACHE KUHUSU BABU YANGU SALUM ABDALLAH

Hiyo picha ya Loco Shed Tabora hapo chini ndipo akifanya kazi babu yangu Salum Abdallah maarufu Baba Popo kuanzia 1947 had 1964.
Alihamia Tabora kutoka Dar es Salaam baada ya Loco Shed kuhamishwa kutoka Dar es Salaam mwaka huo wa 1947.

1955 yeye na Kassanga Tumbo walianzisha chama Tanganyika Railway African Union (TRAU).
Salum Abdallah akiwa President na Kassanga Tumbo Secretary.

TRAU ina historia kubwa sana katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

TRAU ilifanya mgomo mwaka wa 1960 uliodumu siku 82.
Salum Abdallah aliongoza mgomo huo wa wafanyakazi wa Railway uliodumu miezi mitatu.

Kwa miezi mitatu treni na mabasi ya Railway yalisimama hadi Waingereza waliposalimu amri na kuwaita viongozi wa wafanyakazi katika meza ya majadiliano.

Uhuru ulipopatikana babu yangu akapambana kwa fikra na msimamo wa Nyerere kuhusu vyama vya wafanyakazi Nyerere akitaka viwekwe chini ya TANU na viongozi wa vyama vya wafanyakazi pamoja na babu yangu wakipinga wazo hilo.

Yalipotokea maasi ya wanajeshi tarehe 20 Januari 1964 baada ya maasi kuzimwa na jeshi la Waingereza, Nyerere aliwakamata viongozi wote wa vyama vya wafanyakazi na kuwaweka kizuizini.

Babu yangu alifungwa kwenye jela ya Uyui, Tabora na alipotoka kizuizini Tanganyika Railway African Union (TRAU) chama alichokiasisi mwaka wa 1955 kilikuwa kimepigwa marufuku pamoja na vyama vingine vya wafanyakazi na badala yake kimeundwa chama cha National Union of Tanganyika Workers (NUTA) kwa juhudi kubwa za Rashid Kawawa na Michael Kamaliza.

Babu yangu alihama Tabora na kwenda Urambo kupisha shari kwani zilienezwa taarifa za uongo kuwa yeye alikuwa katika kundi pamoja na Victor Mkello (kiongozi wa wafanyakazi wa mashamba ya mkonge) na Kassanga Tumbo walikuwa wamekula njama ya kupindua serikali na kumuua Rais Nyerere.

Babu yangu akajikita katika ukulima wa tumbaku Urambo huku akiendelea na ukulima wake wa miaka yote Kakola na Uyui Tabora.
Fredrick Mchauru aliendelea na utumishi katika serikali ya kikoloni na uhuru ulipopatikana mwaka wa 1961 alishika nyadhifa mbalimbali katika serikali huru kama zilizvyoelezwa katika makala zilizochapwa na Raia Mwema.

Kama mimi nisingeaandika kitabu cha Abdul Sykes huenda historia hii ya babu yangu na wazalendo wengine isingejulikana na historia ambazo zingesomwa ndiyo hizi za watu kama Fredrick Mchauru na wengineo.

Salum Abdallah alifariki mwaka wa 1974 akiwa na umri kama miaka 80 akiwa mkimya sana kwa kuwa hapakuwa tena pale mjini na barza zilizokuwa zikijadili siasa kama miaka ya 1950 wakati wa kudai uhuru.

Siasa ilikuwa sasa jambo la kutisha watu wakihofu kukamatwa na kuwekwa gerezani.

Babu yangu akiungulia ndani kwa ndani kwa chuki dhidi ya TANU chama alichokiendea mbio na kuhudhuria mikutano yake yote ya siri mwaka wa 1953 pamoja na wazee wenzake akina Maulidi na Abdallah Kivuruga, Rajab Saleh Tambwe, Abubakar Mwilima kuwataja wachache, na kuwa mmoja wa waasisi wake mjini Tabora mwaka wa 1955.

Siku zote yeye baada ya kuona vyama vya wafanyakazi vimekwa chini ya TANU na serikali yake aliwaona viongozi wapya wa vyama hivi vibaraka wa serikali hawataweza kupigania haki za wafanyakazi kwa dhati.





Picha: Kulia ni Christopher Kassanga Tumbo anaefuata ni Salum Abdallah.

Pole sana al akhi said. Waislamu walinyanyasika sana kipindi hicho, na waislamu ndio sababu ya yeye kuongoza. Kwa maana "walimchagua aongoze" kwa ufahamu wangu.

Allah awarehemu ndugu zetu waliotangulia!
 
Ndugu zangu,

Binafsi huwa natafakari halafu naamini kwamba kuna wakati mambo ilibidi yafanyike ili nchi isonge mbele kama ambavyo alivyokuja Magufuli (pamoja simkubali) kuvunja mazoea ya aina ya fulani ya uongozi na siasa tuliyokuwa nayo maana hayakuwa yanaonyesha tamati wala faida yeyote kwa manufaa ya taifa letu na vizazi vinavyotufuatia.

Ni kweli kabisa wazazi wetu walipigwa ban kujihusisha na siasa tena wengine hata kuuwawa au kukimbia nchi yao pale ambapo walikuwa na mawazo tofauti na Nyerere, lakini, unafika wakati unajiuliza tungefika wapi katika kujenga umoja wa kitaifa baada ya kuachiwa huo uhuru tukajitawala??

Haya machafuko yangeishaje? Unawaza kwamba tayari kulianza malalamiko dhidi ya mtawala ambaye watu wenyewe walimpa madaraka awaongoze lakini bado waliompa madaraka walitaka kuendeleza majadiliano ya pembeni na kutaka hoja na mawazo yao yakubalike bila kupingwa na mtawala huyo tena na kutaka kuunda vyama pinzani. Je, huo Uhuru tungeupractise vipi si ingekuwa kila siku wanapinduana tu?

Jaribu kupata mfano, Marehemu mzee Tuntemeke Sanga aliporudi Nyerere hakuwa mchoyo alimuita na kumtambua kama msomi na kumtaka wakae atumie usomi na exposure yake kujenga Tanzania mpya kwa maana utumishi wake ulikuwa unahitajika, cha ajabu yeye yasemekana alitaka urais pekee sababu aliona amesoma zaidi ya wote, je tungeendelea na watu kama hawa leo tungekuwa wapi?

Sisemi kwamba Nyerere alifanya sahihi, pia sisemi kwamba nao waliofungwa na wengine kuwekwa kizuizini hawakuwa na hoja za maana sababu nao walikuwa watu wenye mchango mkubwa sana kwa mawazo na pesa hata nguvu zao katika kuitakia mema nchi yetu lakini tufike mwisho tujiulize haya matukio ya ubishani na ujuaji na kutotaka kutii na kushirikiana na mtawala mliyemuweka yangeishia tamati ipi???

Nasema haya nikiwa naangalia hoja za ukanda, kwa maana ya kwamba kila makabila yanataka kuonyesha yalikuwa mstari wa mbele katika kudai Uhuru kupitia machifu wao nk, pia naangalia hoja za udini kwa kuangalia waislam, wakristo wakatoliki, waanglikana, wahindi nk ambao kila mmoja kwa namna yake anataka kuonyesha alikuwa mstari wa mbele kwenye mapambano ya kudai Uhuru wa taifa letu na wanaonyesha kutoridhishwa kwa maana ya kupata fadhila.

Labda swali naloliacha, Kama wewe ungekuwa Nyerere kwa wakati ule na hali Ile nchi unapewa haina pesa, haina jeshi lake, haina mfumo au mifumo rasmi haina sheria zetu maana tunatumia za mkoloni ambazo hazikuwa friendly je ungefanyaje? At the same time unataka muungane muwe kitu kimoja Ila kila mmoja uliyekuwa nae anataka kukugeuka na kuanzisha mapambano mapya ya wenyewe kwa wenyewe ingali mshakuwa huru?????
 
Back
Top Bottom