Machimbo ya Kariakoo Mkononi Mwako

Machimbo ya Kariakoo Mkononi Mwako

Samedi Amba

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
227
Reaction score
178
Habari WanaJF,
Natumaini tumeanza siku vizuri. Hata kama kuna mambo hayaendi, shukuru hata kwa uhai. Mungu yupo atakupambania...

Bila kupoteza muda, ningependa kuwashirikisha wazo, na naomba feedback. Kama mfanyabiashara, siku zote unatafuta pa kununua vitu kwa bei ndogo ili uweze kuuza kwa faida inayoeleweka.

Huenda unatafuta machimbo ya bidhaa za biashara.

Nimejikaza nikakusanya zaidi ya machimbo 300 Kariakoo ambapo unaweza kununua vitu kwa bei nafuu. (natazamia kufikia 1000+ hadi mwisho wa mwezi huu).

Sasa, nikaamua kutengeneza mfumo mdogo ambao utakusaidia kwa njia hii hapa:
  1. Utaingia kwenye mfumo (tutatumia web kwa sasa, apps zitakuja baadaye)
  2. Utachagua biashara unazotaka. Kwa mfano, sandals za kike.
  3. Utapata orodha ya machimbo, ila information utakayoona itakuwa ni jina na location ya biashara.
  4. Utachagua machimbo unayotaka kwa kuclick.
  5. Utapewa bei jumlishi ya machimbo yote ulochagua. (kila chimbo kitakuwa na bei
  6. Utalipia kwa njia unayopenda. Ama kwa simu au credit card (crypto baadaye).
  7. Utatumiwa list ya machimbo kwa njia ya SMS (jina na namba za simu) au email (Majina ya biashara, namba za simu, na location ya biashara). Tutafanya mpango wa Whatsapp baadaye.
Hiyo ndo idea yangu. Ila, nlikuwa na maswali kwako, mfanya biashara:
  • Je, ni nini kinakosekana hapo juu? Unahisi unaweza kuhitaji details zipi za chimbo ambazo hazipo hapo juu?
  • Kwa sasa, ili kupelekwa kwenye chimbo na mwamba hapo Kariakoo, utalipia 5,000. Kwenye mfumo kama huu, unaweza kutoa sh. ngapi kuelekezwa kwenye chimbo husika?
Ni hayo tu. Nasubiri maoni yako.

Pamoja sana,
Amba Jnr.
 
Price Range | Ya bidhaa husika kwenye Chimbo husika | Sababu kariakoo ya sasa inakuhitaji uwe unajua Price range kabla, ili mnunuzi uwe salama.
Na pia, unapendekeza kuwa tuwe na bidhaa zote anazouza mfanyabiashara, or tu target bidhaa muhimu?
 
Ok ok, kuna uzi wa kitambo sana huku watu walitaja machimbo mengi for free.
Hili nalifahamu. Ila, USP (Unique Selling Point) ni hii hapa:

1. Binafsi katika pitapita zangu, nimegundua that the information is very redimentary/basic. Sawa, utapata jina la biashara na namba ya simu, lakini you still don't have a taste ya biashara unayotaka ku-engage nayo.

2. Biashara hubadilika, na location huchange. kwa mfano, watu huhama, na hufunga biashara, na information hubadilika sana. Our initiative itasaidia kukeep information ya machimbo current, fresh and up-to-date.

3. Our information is comprehensive, specific, targeted and on-demand. Nikitaka viatu, napata information about viatu, and the latest info for that matter. Na pia kuwa na link ya mtandao ambapo bidhaa za duka zipo posted. Nikija next month, ntakuta data imetanuka kwa sababu tunareserch na kuongeza machimbo kila kukicha. Tunatumia wadau mbalimbali, bila kutegemea uzoefu wa mtu mmoja tu.

4. Tunasikiliza wateja na kutafuta machimbo kulingana na wanachokitafuta wao. In that case, basi product inakuwa kwa manufaa ya mtafutaji mmoja mmoja. Tunajenga mfumo na mtandao, sio kuhabarisha tu.
 
Bidhaa nyingi zilizokuwa zinafatwa kariakoo sasa hv mikoani zipo labda utofauti wa bei na utakuwa ni mdogo sana!!
Mfanyabiashara mdogo utoke mkoani ulipie nauli,chakula,malazi,mizigo ni hasara
 
Bidhaa nyingi zilizokuwa zinafatwa kariakoo sasa hv mikoani zipo labda utofauti wa bei na utakuwa ni mdogo sana!!
Mfanyabiashara mdogo utoke mkoani ulipie nauli,chakula,malazi,mizigo ni hasara
Hii ndo failure ya plan hii. Atafeli vibaya sana jamaa. Watu wengi hawafanyi intensive research. Jamaa awe makin sana mana utapeli uko nje nje kupitia hili. Na mbaya zaidi ili iwe na mantiki lazima iweze kufikia highest level of customer satisfactions. Mana walengwa wake wakubwa ni watu wanaotoka remoteness areas.
 
Hili nalifahamu. Ila, USP (Unique Selling Point) ni hii hapa:

1. Binafsi katika pitapita zangu, nimegundua that the information is very redimentary/basic. Sawa, utapata jina la biashara na namba ya simu, lakini you still don't have a taste ya biashara unayotaka ku-engage nayo.

2. Biashara hubadilika, na location huchange. kwa mfano, watu huhama, na hufunga biashara, na information hubadilika sana. Our initiative itasaidia kukeep information ya machimbo current, fresh and up-to-date.

3. Our information is comprehensive, specific, targeted and on-demand. Nikitaka viatu, napata information about viatu, and the latest info for that matter. Na pia kuwa na link ya mtandao ambapo bidhaa za duka zipo posted. Nikija next month, ntakuta data imetanuka kwa sababu tunareserch na kuongeza machimbo kila kukicha. Tunatumia wadau mbalimbali, bila kutegemea uzoefu wa mtu mmoja tu.

4. Tunasikiliza wateja na kutafuta machimbo kulingana na wanachokitafuta wao. In that case, basi product inakuwa kwa manufaa ya mtafutaji mmoja mmoja. Tunajenga mfumo na mtandao, sio kuhabarisha tu.
We jamaa unapatikana mkoa gani ili nione how best you think to implement
 
Price Range | Ya bidhaa husika kwenye Chimbo husika | Sababu kariakoo ya sasa inakuhitaji uwe unajua Price range kabla, ili mnunuzi uwe salama.
It can't work safely. Unless wafanyabiashara walipe kwake ili awanunulie yeye awatumie mana kuna dogo aliwahi Fanya pilot ya hii akafeli
 
Niko Morogoro mkuu. Ila implementation plan ndo hiyo. Kuwa free kuikosoa hapa, kwa faida ya wengine pia. Ila, kama unataka mawasiliano zaidi, namba ni 0742308110
So what you think on the customer satisfaction? Unajua bei zinapanda na kushuka?. Customer kalipia kapata namba then akatapeliwa.. utafanyaje kumsaidia?
 
Niko Morogoro mkuu. Ila implementation plan ndo hiyo. Kuwa free kuikosoa hapa, kwa faida ya wengine pia. Ila, kama unataka mawasiliano zaidi, namba ni 0742308110
Unajua utofauti wa bidhaa zilizopo na ubora wake?. Mm nimefanya biashara y uwinga kariakoo kwa muda wa miaka kama miwili hivi.
Hata uwe kariakoo kila siku huwezi jua kila kitu na plan hii inahitaji umakini wa Hali ya juu mana ujanja ujanja wa wabongo kariakoo ndo kwake. Exclude vifaa vya simu na bidhaa za huwa na chapa. Chapa kwa wanaozijua ndio inadetermine bei husika. Kuna sehem rado inauzwa mpaka 15 lakin kiuhalisia ni kopi chafu. Nakucheki nione
 
S
So what you think on the customer satisfaction? Unajua bei zinapanda na kushuka?. Customer kalipia kapata namba then akatapeliwa.. utafanyaje kumsaidia?
Swali zuri. User discretion. Kuna haja ya kujiridisha na unayenunua kwake. Tutafanya our best kujaribu kupata details za kutosha kuhusu kila chimbo. Hata hivyo, tunafahamu kuwa ubinadamu upo, na kuna vigezo fulani vinapaswa kutumiwa kujiridhisha.

Tutaweka verification badge at some point, na kuruhusu user reviews and ratings za machimbo ili wateja wapya wanapokuja waweze kujudge chimbo from past experience za wanunuzi waliotangulia.

Nahisi that's all we can do.
 
Kwa nilivyoelewa bidhaa yako wewe unayouza ni 'information'. Na unaiuza sababu info hizo ni scarce.
Wafanyabiashara wakiamua kujitangaza wao wenyewe moja kwa moja kwa mteja, we hapo utakuwa unauza nini?
Unatambua kwamba mawinga ni washindani wako kwenye hilo wazo? Tofauti yao ni kwamba wao wanalink ya wateja wachache (idadi kadhaa) na wakati mwingine mawinga wananunua mzigo, wanafunga na kumtumia mteja ambae yuko sehemu yoyote Tanzania. Hapa kuna creation kubwa ya value kwa customer. Wewe uta offer nini cha ziada kushindana na mawinga?
Nikiangalia mfumo wa Alibaba unawezekana na kuendelea kuwepo sababu amejitahidi kuweka vitu kama trade assurance kwa consumer so usalama wa bidhaa, quality na hela humfanya consumer aendelee kutumia huduma yao.
 
S

Swali zuri. User discretion. Kuna haja ya kujiridisha na unayenunua kwake. Tutafanya our best kujaribu kupata details za kutosha kuhusu kila chimbo. Hata hivyo, tunafahamu kuwa ubinadamu upo, na kuna vigezo fulani vinapaswa kutumiwa kujiridhisha.

Tutaweka verification badge at some point, na kuruhusu user reviews and ratings za machimbo ili wateja wapya wanapokuja waweze kujudge chimbo from past experience za wanunuzi waliotangulia.

Nahisi that's all we can do.

Hili wazo litapigwa vita na mawinga kuliko kawaida. Jipange piga kazi tu
He cant do the best ,kama hayuko tayari kujifunza kwa walioshindwa. Kama anabisha aingie ground mana Hana tofauti na alibaba. Hii ni local alibaba tu.

Lazima uwe makin mana utapeli uko nje nje na promotion ya web yako inyooke kwelikweli mana hutakuwa na kitu kipya. Hili wazo ni kama umeliongeza hatua kadhaa tu za jamaa mmoja anaitwa kelvin kibenje. Na yeye sio mhusika moja kwa moja wa kufatilia mzigo wako mpaka ufike. Na hii idea iko mezani kwa sasa katika ofisi yake.. nina hof mkuu ulikoitoa mpka akuiandika hapa. By the way! From begin inaweza kutoa sauti ya wewe winga mana bei ni confused sana. Muhimu tu watu walipe kwako ili uwanunulie nje ya hapo umefeli.


Anza na case study ya jamaa flani hivi wanaitwa sarafu.
 
Kwa nilivyoelewa bidhaa yako wewe unayouza ni 'information'. Na unaiuza sababu info hizo ni scarce.
Wafanyabiashara wakiamua kujitangaza wao wenyewe moja kwa moja kwa mteja, we hapo utakuwa unauza nini?
Unatambua kwamba mawinga ni washindani wako kwenye hilo wazo? Tofauti yao ni kwamba wao wanalink ya wateja wachache (idadi kadhaa) na wakati mwingine mawinga wananunua mzigo, wanafunga na kumtumia mteja ambae yuko sehemu yoyote Tanzania. Hapa kuna creation kubwa ya value kwa customer. Wewe uta offer nini cha ziada kushindana na mawinga?
Nikiangalia mfumo wa Alibaba unawezekana na kuendelea kuwepo sababu amejitahidi kuweka vitu kama trade assurance kwa consumer so usalama wa bidhaa, quality na hela humfanya consumer aendelee kutumia huduma yao.
Huyu ni local alibaba. Anakatiza katikati ya mteja na mfanyabiashara. Potential clients wake ni new traders only mana hawatakuwa na haja ya kutoka huko walipo kuja dar. Hao wengine wote wana wauzaji wao wanaowaamini. Na Huyu atajibu maswali ya machimbo ya kweli ambayo hayajitangazi... Mm sikubaliani nae anasema atoe namba tu plan iishie hapo! Ni big failure sabab hata kelvin kibenje anatoa hizo namba
 
Back
Top Bottom